REAL MADRID YAREJEA KILELENI LA LIGA BAADA YA KUICHAPA BARCA 2-1


TIMU ya Real Madrid imeweka hai matumaini ya ubingwa baada ya ushindi wa 2-1 dhidi ya Barcelona usiku wa kuamkia leo Uwanja wa Alfredo Di Stéfano Jijini Madrid.
Mabao ya Real Madrid yamefungwa na Karim Benzema dakika ya 13 na Toni Kroos dakika ya 28, wakati la Barcelona lilifungwa na Oscar Mingueza dakika ya 60.
Kwa ushindi huo katika mchezo wa 30, Real inafikisha pointi 66, sawa na Atletico Madrid yenye mechi moja mkononi na kupanda kileleni, wakati Barcelona inaangukia nafasi ya tatu ikibaki na pointi zake 65 za mechi 30


Comments

Popular posts from this blog

NYOTA WA KIKOSI CHA SIMBA KILICHOFIKA FAINALI KOMBE LA CAF 1993, DAMIAN KIMTI AFARIKI DUNIA