Posts

SIMBA SC YAAFIKI KUCHEZA ZANZIBAR MARUDIANO NA BERKANE

Image
KLABU ya Simba SC imeafiki kucheza mechi ya marudiano ya Fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya RSB Berkane ya Morocco Uwanja wa New Amaan Complex, Zanzibar. Awali mechi hiyo ilipangwa kufanyika  Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam Jumamosi wiki hii — lakini CAF ikaagiza uhamishiwe Zanzibar, ingawa awali Simba walipinga. Taarifa ya CAF iliyosainiwa na Katibu wa Bodi hiyo ya kandanda barani, Mkongo mwenye Uraia wa Uswisi pia, Veron Mosengo-Omba sababu za mabadiliko hayo ni Uwanja wa Benjamin Mkapa ambao upo katika marekebisho wakati huu kutokuwa tayari kwa mchezo huo Mei 25. Barua hiyo ya Mosengo-Omba iliyoelekezwa kwa Katibu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) imesema kwamba taarifa za kina na za Kitaalamu za wakaguzi wa CAF zinaonyesha Uwanja huo hautakuwa tayari kwa matumizi ya mchezo huo mkubwa wiki ijayo, hususan kutokana na tatizo kubwa la Pitch yake na mvua zinazoendelea hivi sasa Dar es Salaam. Mechi hiyo itaanza Saa 10:00 jioni na Simba unatakiwa kushind...

KYLLIAN MBAPPE NDIYE MFALME MPYA WA MABAO HISPANIA

Image
MSHAMBULIAJI Mfaransa, Kylian Mbappé Lottin jana alifunga bao lake la 29 katika msimu wa La Liga , Real Madrid ikiibuka na ushindi wa 2-0 dhidi ya Sevilla Uwanja wa Ramón Sánchez Pizjuán Jijini Sevilla. Mbappe alie katika msimu wake wa kwanza baada ya kuwasili kutoka Paris Saint-Germain alifunga bao hilo dakika ya 75 akimalizia pasi ya kiungo mkongwe Mcroatia, Luka Modrić – kabla ya kiungo wa Kimataifa wa England, Jude Bellingham kufunga bao la pili dakika ya 87 akimalizia pasi yamshambuliaji Gonzalo García. Mbappe anaendelea kuongoza kwa mabao yake 29, kati ya hayo saba amefunga kwa penalty akifuatiwa na mshambuliaji mkongwe wa Kimataifa wa Poland, Robert Lewandowski mwenye mabao 25. Kwa ujumla Mbappe amekwishafunga mabao 40 katika mechi 54 za msimu wake huu wa kwanza Hispania baada ya kujiunga na Los Blancos – idadi ambayo inapitwa na Ronaldo Lima pekee aliyefunga mabao 47 akiwa Barcelona msimu wa 1996/1997. Mbappe amefunga kwenye michuano mikubwa, mbali na mabao 29 ya  La Lig...

PEDRO AIPOKONYA TONGE MDOMONI INTER MILAN, 2-2 NA LAZIO

Image
MSHAMBULIAJI mkongwe wa Kispaniola, Pedro Eliezer Rodríguez (37)Ledesma jana aliipokonya tonge mdomoni Inter Milan akiifungia Lazio bao la kusawazisha dakika ya 90 katika sare ya 2-2 kwenye mchezo wa Serie A Uwanja wa Giuseppe Meazza Jijini Milan. Pedro alifunga pia bao la kwanza la Lazio pia, nalo likiwa la kusawazisha dakika ya 72 baada ya Inter Milan kutangulia na bao la beki Mjerumani Yann Aurel Ludger Bisseck mwenye asili ya Cameroon dakika ya 45'+2, kabla ya beki mwingine, Mholanzi, Denzel Justus Morris Dumfries kufunga la pili dakika ya 79.   Kwa matokeo hayo, Inter Milan inafikisha pointi 78 na inabaki nafasi ya pili ikizidiwa pointi moja na Napoli baada ya wote kucheza mechi 37. Lazio inafikisha pointi 65 nafasi ya sita. MSIMAMO WA SERIE A BAADA YA MECHI ZA JANA: #   Team MP W D L F A D P Last 5 matches H2H 1 Napoli 37 23 10 4 57 27 +30 79 D D W W W 2 Inter Milan 37 23 9 5 77 35 +42 78 D W W L L 3 Atalant...