SIMBA SC YAAFIKI KUCHEZA ZANZIBAR MARUDIANO NA BERKANE

KLABU ya Simba SC imeafiki kucheza mechi ya marudiano ya Fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya RSB Berkane ya Morocco Uwanja wa New Amaan Complex, Zanzibar. Awali mechi hiyo ilipangwa kufanyika Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam Jumamosi wiki hii — lakini CAF ikaagiza uhamishiwe Zanzibar, ingawa awali Simba walipinga. Taarifa ya CAF iliyosainiwa na Katibu wa Bodi hiyo ya kandanda barani, Mkongo mwenye Uraia wa Uswisi pia, Veron Mosengo-Omba sababu za mabadiliko hayo ni Uwanja wa Benjamin Mkapa ambao upo katika marekebisho wakati huu kutokuwa tayari kwa mchezo huo Mei 25. Barua hiyo ya Mosengo-Omba iliyoelekezwa kwa Katibu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) imesema kwamba taarifa za kina na za Kitaalamu za wakaguzi wa CAF zinaonyesha Uwanja huo hautakuwa tayari kwa matumizi ya mchezo huo mkubwa wiki ijayo, hususan kutokana na tatizo kubwa la Pitch yake na mvua zinazoendelea hivi sasa Dar es Salaam. Mechi hiyo itaanza Saa 10:00 jioni na Simba unatakiwa kushind...