Posts

Showing posts from April, 2019

YAHYA ZAYD ACHEZA SAA NZIMA LAKINI ISMAILIA YAPIGWA 1-0 NA HARAS EL HODOOD

Image
Na Mwandishi Wetu, CAIRO MSHAMBULIAJI chipukizi wa kimataifa wa Tanzania, Yahya Zayd usiku wa jana amecheza kwa karibu saa nzima timu yake, Ismailia ikichapwa 1-0 na Haras El Hodood katika mchezo wa Ligi Kuu ya Misri Uwanja wa Gehaz El Reyada mjini Cairo. Pamoja na kuwa wenyeji, Ismailia hawakufurukuta wakiadhibiwa na Haras El Hodood na wapinzani wenzao wa zamani wa Simba SC ya Dar es Salaam kwa bao pekee la mshambuliaji kinda wa miaka 21 kutoka Nigeria, Edu Moses dakika ya 28. Zayd aliyejiunga na Ismailia msimu huu kutoka Azam FC ya nyumbani, Tanzania alitolewa dakika ya 58, nafasi yake ikichukuliwa na Karim Bambo. Yahya Zayd usiku wa jana amecheza kwa karibu saa nzima Ismailia ikichapwa 1-0 na Haras El Hodood katika Ligi Kuu ya Misri Hata hivyo, mabadiliko hayo hayakuweza kuinusuru Ismailia kupoteza 10 katika msimu huu, hivyo kubaki na pointi zake 37 baada ya kucheza mechi 29 na sasa ipo nafasi ya saba. Baada ya ushindi wa jana, Haras El Hodood sasa wanasogea nafasi ya 15 kat

AJAX YAITANDIKA TOTTENHAM HOTSPUR 1-0 PALE PALE LONDON

Image
Kipa Hugo Lloris wa Tottenham Hotspur akijaribu bila mafanikio kuokoa mpira uliopigwa na Donny van de Beek kuipatia bao pekee la ushindi Ajax dakika ya 15 ikiwalaza wenyeji 1-0 katika mchezo wa kwanza wa Nusu Fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya usiku wa kuamkia leo Uwanja wa Tottenham Hotspur mjini London. Timu hizo zitarudiana Mei 8 na mshindi wa jumla atakuwa atakutana na mshindi wa jumla baina ya Barcelona na Liverpool kwenye fainali Juni 1   PICHA ZAIDI GONGA HAPA  

SIMBA SC KUCHEZA MECHI YA KIRAFIKI NA SEVILLA YA HISPANIA MEI 23 UWANJA WA TAIFA

Image
Na Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF) limetangaza timu ya Simba ya Tanzania kucheza mchezo wa kirafiki wa Kimataifa na Sevilla ya Hispania Mei 23,2019 Uwanja wa Taifa. Afisa Habari na Mawasiliano wa TFF, Clifford Mario Ndimbo amesema kwamba Simba imetajwa kucheza mchezo huo dhidi ya Sevilla kwa kigezo cha Klabu ya Tanzania iliyofanya vizuri katika mashindano ya SportPesa Cup kwa timu zinazodhaminiwa na SportPesa. Sevilla waliopo kwenye Ligi Kuu ya Hispania La Liga wataingia Tanzania Mei 21,2019 tayari kwa mchezo huo. Katibu Mkuu wa TFF Kidao Wilfred amesema kigezo kikubwa kilichotumika kuchagua timu ya kucheza mchezo huo ni timu ya Tanzania iliyofanya vizuri katika mashindano ya SportPesa ambapo Simba ilifikia hatua ya nusu fainali. Amesema ratiba ya Ligi Kuu imebana kimetumika kigezo cha mashindano ya SportPesa kumpata muwakilshi wa kucheza na Sevilla. Mkurugenzi wa Utawala na Udhibiti wa SportPesa Tarimba Abas awali kulikuwa na wazo la kuzikutanish

SIMBA SC 1-0 JKT TANZANIA (LIGI KUU TANZANIA BARA)

Image

ZAHERA - INGEKUWA ULAYA TUNGESHATANGAZWA MABINGWA

Image

VIDEO: TFF WALIVYOTOA SABABU RASMI ZA KUIPIGA CHINI YANGA KUCHEZA NA SEVILLA

Image

VIDEO: KOCHA SIMBA APANDWA NA MZUKA BAADA YA MECHI NA JKT

Image

VIDEO: DIAMOND AANDIKA UJUMBE MZITO KWENDA KWA TANASHA

Image

SIMBA YAPEWA RASMI UBINGWA LIGI KUU

Image
Kutokana na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya JKT Tanzania jioni ya jana, unaambiwa mashabiki wengi wa timu ya Simba wamesema ubingwa wa ligi msimu huu utatua kwao. Jeuri hiyo imekuja kutokana na ushindi huo uliowafanya kuifikishia Simba alama 72 huku watani zao wa jadi Yanga wakiwa na 77. Wengi wameeleza kuwa kwa Simba hii ya sasa wana asilimia kubwa ya kutetea taji lao licha ya kuwa na mechi kadhaa ngumu zilizosalia ikiwemo ya Tanzania Prisons na Mtibwa Sugar pia Azam FC. Simba ilikuwa na viporo vingi kutokana na ushiriki wake wa mashindano ya kimataifa uliosababisha mechi zake za ligi kurundikana na mara baada ya kutolewa ilibidi waanze kuvicheza. Mpaka sasa wekundu hao wa Msimbazi wamepoteza mechi mbili pekee msimu huu ikiwa ni dhidi ya Mbao FC na Kagera Sugar.

HUKO JANGWANI YANGA WAPINGANA NA TFF JUU YA SIMBA KUCHEZA NA SEVILLA

Image
Baadhi ya mashabiki na wanachama wa klabu ya Yanga wamelitupia lawama Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kuipangia Simba kucheza na Sevilla ya Spain. Hatua hiyo imekuja mara baaa ya TFF kuthibitisha kuwa Simba itakipiga na Sevila kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam ukiwa ni mchezo wa kirafiki kuelekea msimu ujao. Mashabiki na wanachama hao wamesema kuwa awali ilielezwa kulipaswa kufanyike mechi baina ya watani wa jadi ili mshindi ndiyo acheze na Sevilla. TFF kwa kushirikiana na SportPesa wameamua kuwachagua Simba kucheza na Sevilla kwa kuangalia ubora wa miaka ya hivi karibuni. Rekodi zinaonesha kuwa Simba ndiyo wamekuwa bora zaidi katika Ligi Kuu Bara kwa miaka ya hivi karibuni ukilinganisha na timu zingine.

DAKIKA 7 ZA NYONGEZA SIMBA VS JKT ZAWA GUMZO, YANGA WAHOJI

Image
Baada ya kikosi cha Simba kuibuka na ushindi wa bao 1-0 katika dakika za mwisho jana dhidi ya JKT Tanzania, gumzo kubwa ni kuhusiana na dakika saba za mwisho zilizoongezwa na Mwamuzi wa mchezo huo. Simba iliibuka na ushindi huo kupitia bao la Hassan Dilunga aliyefunga katika dakika ya mwisho kabisa zikiwa zimeongezwa hizo saba ambao zimeleta hoja kubwa haswa kwa mashabiki wa upande wa pili ambao ni Yanga. Kupitia mitandao na hata vijiweni kumeonekana mashabiki wengi wa Yanga wakihoji imekuwaje mechi hiyo iongezewe dakika saba na wengi wao wakiamini hazikuwa zinastahili. Asilimia kubwa wamesema kuwa ni kama kulikuwa na upendeleo wa kuitafutia Simba matokeo wakiamini mechi ilikuwa inamalizika kwa matokeo ya 0-0. Malalamiko hayo yamekuja ikiwa Simba na Yanga zinawania ubingwa wa Ligi Kuu Bara huku wekundu hao wa Msimbazi wakiwa bado na viporo vya mechi wakielekea kuvikamilisha.

MUONEKANO WA GAZETI LA CHAMPIONI KATIKA UKURASA WA MBELE LEO JUMATANO

Image
MUONEKANO WA GAZETI LA CHAMPIONI KATIKA UKURASA WA MBELE LEO JUMATANO

VIDEO: TAZAMA HIGHLIGHTS ZA MECHI YA SIMBA VS JKT IKWEMO DAKIKA 7 ZA NYONGEZA

Image

PIERRE: AMBER LULU ALINIFANYA MWENYEWE, ALIANGUKA AKAZIMIA – VIDEO

Image

BABA D AFUNGUKA KUFANYA KOLABO NA DIAMOND

Image
BABA wa msanii wa Bongo Fleva Naseeb Abdul ‘Diamond Platinumz’, mzee Abdul Juma leo ametembelea ofisi za Global Group zilizoko Sinza-Mori, jijini Dar es Salaam. Baba D alitembelea vitengo vya Magazeti Pendwa, Global TV Online na Radio Global Online kushuhudia shughuli mbalimbali ambapo amesema atajadili na mwanaye ili aweze kufanya naye kolabo. Akizungumza katika mahojiano na Global Radio, amesema: “Nitaongea na mwanangu, jambo hilo halina matatizo, kwani  kuku ni wako huwezi ukakaa nje ukampiga kwa manati,” alisema msanii huyo ambaye sasa anatamba na wimbo wa  Dudu La Yuyu.

VIDEO: BAO LA SIMBA DHIDI YA JKT TANZANIA HILI HAPA, DAKIKA 7 ZA NYONGEZA

Image

BAO LA DAKIKA YA MWISHO LAIPA USHINDI SIMBA SC IKIILAZA JKT TANZANIA PUNGUFU 1-0

Image
Na Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM SIMBA SC imeendeleza wimbi la ushindi katika Ligi Kuu ya Tanzania Bara baada ya kuichapa 1-0 JKT Tanzania Uwanja wa Uhuru mjini Dar es Salaam jioni ya leo. Kwa ushindi huo, Simba SC inafikisha pointi 72 baada ya kucheza mechi 28 na kuendelea kushika nafasi ya pili, nyuma ya watani wao wa jadi, Yanga SC wenye pointi 77 za mechi 33. Sifa zimuendee mfungaji wa bao hilo pekee dakika ya sita kati ya saba za nyongeza baada ya kutimia dakika 90 za kawaida, kiungo Hassan Dilunga aliyetokea benchi kipindi cha kwanza kuchukua nafasi ya Nahodha, John Raphael Bocco. Lakini pongezi haswa zimuendee mpishi wa bao hilo, mshambuliaji wa kimataifa wa Uganda, Emmanuel Arnold Okwi aliyewavuruga mabeki wa JKT kwa chenga kabla ya kumpenyezea mpira mfungaji.  Na Okwi alipiga bao hilo akitoka kukosa mabao zaidi ya matatu ya wazi kwenye mchezo uliochezeshwa na Heri Sasii aliyesaidiwa na washika vibendera Hellen Mduma na Shaffi Mohammed wote wa Dar es Salaam. Nahocha Joh

TPL : SIMBA0-0 JKT TANZANIA, UWANJA WA UHURU

Image
MCHEZO unaoendelea kwa sasa Uwanja wa Uhuru ni kati ya wenyeji Simba wakimenyana na JKT Tanzania. Kwa sasa ni kipindi cha pili na hakuna mbabe ambaye ameona lango la mpinzani wake kwa sasa. JKT Tanzania wanafanya mashambulizi kwa kushtukiza kuliandama lango la Deogratius Munish. Mashabiki waliojitokeza hapa Uhuru sio wengi sana kutokana na leo kuwa siku ya kazi. Nahodha wa Simba John Bocco alitolewa kipindi cha kwanza nafasi yake imechukuliwa na kiungo Hasan Dilunga

JPM AANIKA KINACHOUTESA MOYO WAKE – VIDEO

Image
RAIS  John Magufuli ameeleza masikitiko yake kufuatia timu za soka za taifa ambazo ni timu ya wakubwa (Taifa Stars) na timu ya vijana chini ya umri wa miaka 17, Serengeti Boys,  kufungwa na timu za mataifa mengine katika michuano mbalimbali ambayo imechezwa hivi karibuni. Magufuli amesema hayo leo Aprili 30, 2019 wakati wakiwahutubia wananchi wa Kyela mkoani Mbeya ikiwa ni siku chache baada ya Serengeti Boys kuondolewa kwenye michuano ya Afcon U17, iliyokuwa ikichezwa hapa nchini na kusema  kitendo cha kufungwa kwa timu hizo kimekuwa kikimnyima raha huku akimtaka waziri wa micghezo, Dkt Harrison Mwakyembe kufuta aibu hiyo ya kufungwa kila mara. “Kukatika kwa umeme kunaumiza sana, unakuta unaangalia mpira umeme unakatika halafu goli linaingia, na Waziri wa Michezo anatoka huku Mbeya, ingawaje kwenye timu ya vijana ameniangusha sana. Katika vitu ambavyo huwa vinaniudhi ni kufungwa timu zangu, huwa inaniuma mno, yani watu milioni 55, mnafungwa na timu ya nchi yenye watu milioni 33, hii

MAMBOSASA ALIVYONASA WEZI MAFUTA YA TRANSFOMA – VIDEO

Image

KIKOSI CHA SIMBA KITAKACHOANZA LEO DHIDI YA JKT TANZANIA

Image
KIKOSI cha Simba kitakachoanza Leo dhidi ya JKT Tanzania Uwanja wa Uhuru Kikosi kitakachoanza Deogratius Munish Zana Coulibary Mohamed Hussen Yusufu Mlipili Erasto Nyoni James Kotei Clatous Chama Mzamiru Yassin John Bocco Meddie Kagere Emmanuel Okwi Kikosi cha akiba Aishi Manula Nicholas Gyan Paul Bukaba Said Ndemla Hassan Dilunga Mohamed Rashid Rashid Juma

KUMEKUCHA UCHAGUZI YANGA, MGOMBEA AAHIDI KUREJESHA TIMU KWA WANANCHI, KUIBADILISHA YANGA KUWA KAMA ULAYA

MGOMBEA wa nafasi ya Mwenyekiti wa klabu ya Yanga, Dr Mshindo Msolla amesema kuwa uzoefu wake wa michezo kwa muda wa miaka 40 utamsaidia kuweza kutekeleza mipango ya klabu kwa wakati na hesabu zake ni kuirudisha timu kwa Wananchi. Yanga inatarajia kufanya uchaguzi wake Mei 5 mwaka huu na leo kampeni zimezinduliwa rasmi kwa wagombea ili kupata viongozi wapya kwa ngazi ya Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti na Wajumbe wa Kamati ya Utendaji ndani ya Yanga. Akizungumza leo wakati wa uzinduzi wa kampeni hizo makao makuu ya Yanga, Msolla amesema kuwa amedhamiria kuleta mabadiliko ndani ya Yanga ili kutatua changamoto ya ombwe la uongozi ambalo lilikuwa linaathiri ufanisi wa klabu. "Kwa kipindi kirefu kumekuwa na changamoto ya kiuongozi na matokeo yake changamoto hiyo imefanya kuwe na ombwe la uongozi, nimeamua kugombea nafasi ya Mwenyekiti wa klabu kwa sababu nina uzoefu wa kutosha hasa baada ya kuwa kwenye tasnia ya mpira kwa muda wa miaka 40 katika nyanja mbalimbali. "Nitahakikisha

AZAM FC WALIA NA UZOEFU WA WACHEZAJI

Image
KOCHA wa Azam FC, Meja Abdul Mingange amesema kuwa uzoefu umewaponza wachezaji wake hali iliyowafanya wakafungwa bao 1-0 na Yanga kwenye mchezo wao wa ligi uliochezwa jana uwanja wa Uhuru. Azam FC ilifungwa bao hilo na Mrisho Ngasa ambaye alikuwa mchezaji wao wa zamani dakika ya 13 na lilidumu mpaka mwisho wa mchezo na kuwafanya wapoteze pointi tatu muhimu. Akizungumza na Saleh Jembe, Mingange amesema kuwa walijipanga kiasi cha kutosha kupata ushindi kwenye mchezo wao ila walizidiwa uzoefu na wapinzani wao ambao walidhamiria kushinda. "Haikuwa mipango yetu kupoteza mchezo wetu mbele ya Yanga, tulijipanga kiasi cha kutosha kushinda ila uzoefu wa wachezaji wangu ukatufelisha kwenye mchezo wetu. "Yanga ni timu kubwa na ina wachezaji wengi ambao wanauzoefu na ligi tofauti na sisi, licha ya kutengeneza nafasi nyingi kwenye mchezo wetu tulishindwa kupata matokeo kutokana na kushindwa kuzitumia nafasi tulizotengeneza," amesema Mingange. Azam FC wanasalia nafasi ya tatu w

TANZANIA PRISONS: TUNAISIMAMISHA YANGA KIBABE

Image
BEKI Kisiki wa timu ya Tanzania Prison, Salum Kimenya amesema kuwa mkakati wao ni kuona wanashinda mchezo wao unaofuata dhidi ya Yanga utakaochezwa Uwanja wa Taifa, Mei 2. Kimenya amekuwa akitimiza majukumu yake ndani ya kikosi cha Prisons ambapo mpaka sasa kwa upande wa mabeki yeye ni namba moja kwa kutupia nyavuni akiwa amefanya hivyo mara saba. Akizungumza na Saleh Jembe, Kimenya amesema kuwa tayari kikosi chao kimetia kambi Dar kwa ajili ya kuzoea mazingira na kujiandaa na mchezo wao muhimu kwao. "Tumejipanga na tupo hapa kwa muda mrefu kujiandaa kuikabili Yanga, nina imani kwa maandalizi ambayo tunayoyafanya tutapata matokeo na hatuna mashaka yoyote. "Ushindani kwa sasa ni mkubwa nasi tunapambana ili kuona msimu ujao tunaoendelea kubaki kwenye ligi hizo ndizo hesabu zetu kwa sasa mashabiki watupe sapoti," amesema Kimenya. Yanga wanakumbukumbu ya kupoteza mchezo wa kwanza uliochezwa Uwanja wa Sokoine, walipoteza kwa kufungwa mabao 3-1.

KIPIGO CHA SERENGETI BOYS CHAMKASIRISHA RAIS MAGUFULI, AIPA TAHADHARI TAIFA STARS

Image
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, John Pombe Magufuli amesema kuwa ameboreka na kitendo cha timu ya Taifa ya Vijana, Serengeti Boys kufungwa mabao mengi katika ardhi ya nyumbani. Akizungumza leo wakati wa hotuba mbele ya wananchi wa mkoa wa Mbeya wilayani Kyela ambapo yupo kwenye ziara ya kikazi, Magufuli amesema hajafurahishwa na timu ya vijana kufungwa mabao mengi uwanja wa nyumbani. "Mashindano tumeaandaa wenyewe, uwanja wa kwetu wenyewe, tumefungwa mabao mengi kwelikweli, hili ni jambo la ajabu, tupo watu zaidi ya milioni tano na utashangaa tumefungwa na timu ambayo ina watu chini ya milioni 5, bora ungechukua timu ya Kyela naamini isingefungwa. "Sasa hili linapaswa liangaliwe kwa usawa, ninatamani siku moja niwe Waziri wa Michezo na nikiwa Waziri wa Michezo timu nitaipanga mwenyewe, kwa hili la kupigwapigwa kwa timu yetu ya Taifa mnaniboa kweli na sijui timu ya wakubwa nayo itakwenda kufungwa? ila sio mbaya huenda kufungwa fungwa nako ni vizuri," amesema

MO AWAPA MILIONI 240 WACHEZAJI WAWILI SIMBA

Image
SIMBA Wamebakiza pointi tano tu wawang’oe wapinzani wao Yanga katika nafasi ya kwanza kwenye msimamo. Sasa ili kukoleza vita ya kuwashusha, nyota wa kikosi hicho kilicho chini ya uwekezaji wa bilionea kijana Mohamed Dewji ‘Mo’, leo Jumatatu watapewa kiasi cha Sh milioni 240 kwa ajili ya kuongeza motisha. Simba walipata pointi tisa katika mechi nne walizocheza Kanda ya Ziwa, ambapo Emmanuel Okwi na John Bocco walikuwa nguzo kwenye upatikanaji wa pointi hizo huku kila mmoja wao akiweka kambani mabao matatu. Simba kwa sasa wanakamata nafasi ya pili kwenye msimamo wa Ligi Kuu Bara wakiwa na pointi 69, zikiwa ni pointi tano nyuma ya Yanga ambao wapo kileleni wakiwa na pointi 74. Chanzo kutoka ndani ya Simba kimeliambia Championi Jumatatu, kuwa kiasi hicho cha Sh milioni 240 watakachopewa kwa ajili ya kuongeza upambanaji wa kusaka ubingwa kinatokana na ushindi wa michezo minne kati ya mitano iliyopita. “Kuanzia kesho (leo) Jumatatu, wachezaji watawekewa fedha zao za bonasi baada ya kush

RASMI SIMBA SASA KUMENYANA NA SEVILLA KUTOKA HISPANIA, TFF YATAJA SABABU

Image
IMEELEZWA kuwa mabingwa wa Ligi Kuu Tanzania, Simba watamenyana na kikosi cha Sevilla ambao ni Mabingwa mara tano wa UEFA kutoka nchini Hispania ambacho kinashiriki La Liga. Mchezo huo wa kihistoria unatarajiwa kuchezwa Mei 23 Uwanja wa Taifa Dar ambapo Sevvila watakuwa kwenye ziara ya kimichezo ya siku tatu inayokwenda kwa jina la 'La Liga World SportPesa Challenge' inayodhaminiwa na kampuni ya kubashiri ya SportPesa. Mkurugenzi wa Utawala na Utekelezaji wa SportPesa Tanzania Abbas Tarimba amesema kuwa hilo ni lengo la kukuza na kuboresha michezo Tanzania. Katibu Mkuu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) Wlilfred Kidao amesema kuwa sababu ya kuichagua Simba kumenyana na Sevilla ni kutokana na timu hiyo kumaliza ikiwa nafasi ya tatu kwenye michuano ya SportPesa Super Cup ikiwa ni nafasi ya juu zaidi kwa timu za Tanzania.

BREAKING NEWS: SIMBA KUWAVAA VIGOGO WA HISPANIA DAR, NI SEVILLA, INATANGAZWA LEO

Image
Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), limeipitisha Simba kuwavaa moja ya vigogo wa Ulaya, Sevilla. Sevilla ni moja ya kikosi bora barani Ulaya kutoka nchini Hispania na kinatarajia kuwa na ziara nchini, mwishoni mwa Mei. Habari kutoka ndani ya TFF, zimeeleza kuwa shirikisho hilo limetoa nafasi kwa Simba kutokana na kuwa mabingwa watetezi lakini waliokuwa wawakilishi wa Tanzania waliofika robo fainali ya michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika. Sevilla inaletwa nchii na wadhamini wakuu wa Simbana Yanga, kampuni ya kubeti ya SportPesa ambayo sasa ni kampuni maarufu zaidi ya michezo hiyo nchini.

YANGA YAFICHUA KILICHOIPONZA AZAM FC KUPIGWA JANA UWANJA WA UHURU

Image
KOCHA Mkuu wa Yanga, Mwinyi Zahera amesema kuwa kilichoiponza timu ya Azam FC kupoteza mchezo wa jana ni kutumia nguvu nyingi uwanjani hali iliyowafanya wakapoteza nafasi walizotengeneza. Kwenye mchezo uliochezwa jana uwanja wa Uhuru, Azam ilifungwa bao 1-0 na Yanga lililopachikwa na Mrisho Ngassa dakika ya 13. Akizungumza na Saleh Jembe, Zahera amesema kuwa alikisoma kikosi cha Azam namna kinavyocheza na mbinu zake hali iliyomfanya kuunda kikosi cha ushindi mapema. "Nilikiandaa kikosi kwa muda kidogo hasa baada ya kufuatilia Azam FC, ni timu nzuri ina wachezaji wazuri ila wanashindwa kutulia na kutumia akili, hapo ndipo niliwaweza na baada ya bao kuingia waliongeza matumizi ya nguvu. "Utaona namna wachezaji wangu walivyokuwa wakidondoka sababu haikuwa kuchoka ilikuwa ni nguvu za wachezaji wa Azam FC, ila kama wangetumia akili ulikuwa mchezo mgumu kwangu," amesema Zahera. Uhindi huo unaifanya Yanga kujikita kileleni na pointi zake 77 baada ya kucheza michezo 33 na

SIMBA YAZIPIGIA HESABU POINTI TATU ZA JKT TANZANIA LEO

Image
KOCHA Mkuu w a Simba, Patrick Aussems amesema kuwa wapo tayari kwa ajili ya mchezo wa leo dhidi ya JKT Tanzania utakaopigwa uwanja wa Uhuru majira ya saa 10:00. Simba itashuka kwa mara ya kwanza uwanja wa Uhuru msimu huu ikiwa na kumbukumbu ya kushinda mabao 2-0 mchezo wa kwanza mbele ya JKT uliochezwa uwanja wa Mkwakwani Tanga. "Kazi kubwa kwa sasa ni kuona tunapata matokeo chanya mbele ya wapinzani wetu, tunawaheshimu na tunajua ushindani ulivyo ila hakuna namna lazima tupambane. "Ushindani kwa sasa kwenye ligi ni mkubwa na kila timu ni bora ninaamini wachezaji wangu watapambana, mashabiki wajitokeze kutupa sapoti," amesema Aussems.

YANGA YAWEKA REKODI YA AINA YAKE UWANJA WA UHURU TANGU LIGI KUU BARA KUANZISHWA

Image
Timu ya Yanga imeweka rekodi ya aina yake pengine tangu kuanzishwa kwa Ligi Kuu Bara kuanzishwa hapa nchi kwa kuja na aina ya jezi tofauti tena ikicheza dhidi ya Azam FC, Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam. Katika mechi hiyo, Yanga ilikuja ikiwa na jezi zingine mpya, jezi ambayo imekuwa ni ya tisa sasa kwa timu hiyo kutoka mitaa ya Twiga, Jangwani kwa msimu huu. Katika mchezo huo ilioshinda kwa bao 1-0, Yanga ilikuja na jezi aina mpya zenye rangi ya njano na michirizi ya kijani na kuwaSAPRAIZI wanachama na mashabiki wake uwanjani. Hivi karibuni Kaimu Katibu Mkuu wa timu hiyo, Omar Kaya, aliwahi kunukuliwa akisema kuwa wanabadilisha jezi kwasababu wanaamua kama uongozi na hakuna atakayeweza kuwangia cha kufanya. Mabadiliko hayo ya jezi yamekuwa yakiwakera baadhi ya mashabiki kutokana na kubadilishwa mara kwa mara na kushindwa kujulikana ni jezi ipi rasmi inayotumika ikiwemo ya nyumbani na ugenini. Aidha, wapo pia ambao wamekuwa wakipongeza wakieleza kuvutiwa na jezi hizo a

MKUDE NA KIUNGO MWINGINE YANGA WATENGEWA MILIONI 500

Image
MASTAA wa Taifa Stars akiwemo Fei Toto wa Yanga na Jonas Mkude wa Simba mwaka huu wataota ndoto za ajabu. Wanakutana na maisha ambayo hawakuwahi kuyafikiria. Caf imetoa dola 260,000(Sh.Mil 598) kama advansi ya maandalizi ya Stars kwa ajili ya fainali za Afcon. Kwa lugha rahisi ni kwamba wachezaji wa Stars wanaeza kuweka kambi popote Duniani na kama fedha haitoshi wanaruhusiwa kuomba nyongeza. Lakini mechi zote tatu za awali za Stars kwenye Afcon zitachezwa usiku. Kwa mujibu wa taarifa ya Caf mgawo huo umetolewa kama advansi kwa timu zote zilizofuzu fainali za Afcon inayoanza Juni ambayo Stars haikuwahi kufuzu tangu kina Mkude na Feitoto wazaliwe. Mgawo huo utakatwa kwenye kiwango itakachoambulia timu husika mpaka mwisho wa mashindano kwani kila nafasi kwenye kundi ina kiwango chake. Kwa kufuzu tu hatua ya makundi kila timu shiriki ina uhakika wa Sh.Bil 1 lakini timu ikivuka hatua ya mtoano mkwanja unakuwa mnene. Bingwa wa Afcon msimu huu anabeba Sh.Bilioni 10.3 katika mashindano

AZAM FC 0-1 YANGA SC (LIGI KUU TANZANIA BARA)

Image

DIAMOND APEWA MTIHANI HUU MZITO NA BABA YAKE

Image
MOJA kati ya matukio yaliyotikisa ndani ya wiki iliyopita ni lile la kupatana kwa mwanamuziki Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ na baba yake Abdul Jumaa ambapo baada ya kupatana huko, msanii huyo amepewa mtihani mzito ambao akiufaulu, itaaminika kuwa kilichofanyika siyo kiini macho. Kupatana kwa wawili hao kumekuja baada ya figisu za muda mrefu ambazo zilihitimishwa Jumanne iliyopita ndani ya Studio za Wasafi TV ambapo waliamua kuzika tofauti zao na kufungua ukurasa upya. Hatua hiyo iliwafurahisha wengi ambao hawakuwa wakivutiwa na umbali uliokuwepo kati ya baba na mwanaye huyo hivyo pongezi nyingi zikamiminika kwa Diamond. Mbali na pongezi hizo, ndugu na mashabiki wa staa huyo walimpa mtihani mzito na kusema akiufaulu wataamini kilichotokea ni kweli na siyo kiki kama baadhi wanavyodhani.  Akizungumza na Ijumaa Wikienda, mmoja wa ndugu wa baba Diamond aliyejitambulisha kwa jina la Swedi Juma alisema, wamefurahishwa na hatua aliyofikia ndugu yao na mwanaye lakini wataamini kama kweli

VIDEO: KOCHA AZAM - YANGA WAMEZIBA MBELE, UKOMAVU SIYO UMRI

Image

DOOH!! NI PIGO KUBWA YANGA, HIVI NDIYO GADIEL MICHAEL ALIVYOUMIA UHURU

Image

VIDEO: ZAHERA ATAJA SIFA YA AZAM, AELEZA NAMNA ALIVYOWAPANGA WACHEZAJI WAKE

Image
Mtanange kati ya Klabu ya Yanga na Azam FC umemalizika kwa Yanga kuwachapa bao 1 - 0, mkwaju uliowekwa kimiana na Winga Mrisho Ngassa. Baada ya kuwachapa waoka mikato hao, Kocha Mkuu wa Yanga, Mwinyi Zahera, amesema alishajipanga kuifunga Azam hivyo na kuwapa silaha za kutosha wachezaji wake...

VIDEO: KOCHA AZAM - WAKUJILAUMU NI SISI WENYEWE, TUMEKOSA NAFASI

Image

VIDEO: RIP AZAM, HII NDIYO YANGA, HATUBEBWI

Image

MTUHUMIWA WA MAUWAJI YA 2PAC ATUPWA JELA MIAKA 10

Image
Darnell Brim mtuhumiwa wa mauwaji ya 2 Pac  amehukumiwa miaka 10 jela baada ya kukutwa na kosa la kutaka kuuza Dawa za kulevya ‘Cocain’. Darnell Brim alikamatwa na madawa ya kulevya mwaka 2013, sasa amekiri kosa kuhukumiwa kifungo hicho. Darnell Brim ni miongoni mwa watu wanne waliokuwa katika gari nyeupe aina ya Cadillac ambayo iliichapa risasi gari ya Suge Knight na kumuaa Tupac Shakur 1996 lakini polisi walishindwa kuthibitisha.

AUSSEMS: TUMERUDI DAR, KAZI BADO

Image
KOCHA Mkuu wa Simba, Patrick Aussems, amefunguka kuwa wanarudi jijini Dar kujipanga zaidi baada ya kukusanya pointi tisa kwenye mechi zao nne za Kanda ya Ziwa. Kikosi hicho kilirejea Dar jana Jumapili Kikitokea mkoani Mara ambapo kilikuwa na mechi ya Ligi Kuu Bara dhidi ya Biashara United na Kushinda 2-0. Mechi nyingine Simba Walizocheza Kanda ya Ziwa na kushinda ni dhidi ya Alliance na KMC, huku wakifungwa na Kagera Sugar. Aussems ameliambia Championi Jumatatu, kuwa wanarudi Dar kujipanga zaidi kwa ajili ya mechi zao zijazo za ligi ambazo wanataka kushinda ili kukaa juu ya msimamo wa ligi. “Ni furaha kushinda mechi yetu ya mwisho Musoma na kupata pointi ambazo tulikuwa tunazitaka. Nimeridhika na utendaji wa kazi wa kikosi change katika mechi za Kanda ya Ziwa. “Kwa sasa tumerudi Dar kuja kujipanga kwa ajili ya mechi zetu zijazo, lengo ni kushinda ili kukaa juu kwenye msimamo wa ligi,” alisema kocha huyo raia wa Ubelgiji. Mechi inayofuata ya Simba ni kesho Jumanne dhidi ya JKT Ta

REKODI YA BEKI JOHN TERRY YAVUNJWA BAADA YA KUPITA MISIMU SITA

Image
TUZO ya mchezaji bora wa mwaka 2018-19 aliyoibeba jana beki wa Liverpool, Virgil Van Dijk imevunja rekodi iliyowekwa kwa muda wa misimu sita baada ya kubebwa kwa mara ya kwanza na beki wa Chesea John Terry msimu wa mwaka 2004-05. Dijk alitwaa tuzo hiyo iliyokuwa mikononi mwa mchezaji mwenzake Mohamed Salah ambaye alitwaa msimu uliopita wa mwaka 2017-18. Beki huyo mwenye miaka 27 aliwapoteza washindani wenzake ambao alikuwa akishindana nao ikiwa ni pamoja na Raheem Sterling, Bernardo Silva, Sergio Aguero, Sadio Mane na Eden Hazard. Pia mshabuliaji wa kikosi cha timu ya wanawake ya  Arsenal Vivianne Miedema mwenye miaka 22 alitwaa tuzo ya mchezaji bora baada ya kuisaidia timu yake kutwaa ubingwa akiwashinda  wenzake kama Steph Houghton, Nikita Parris, Keira Walsh, Erin Cuthbert na Ji So-yun. Miedema amesaidia timu yake hiyo ya Arsenal kutwaa kombe hilo baada kupita misimu mitatu mara ya mwisho kutwaa ubingwa huo ilikuwa mwaka 2012.

STRAIKA MPYA YANGA ATUA

Image
YANGA imemshusha nchini kimyakimya straika wa FC Lupopo, Rodrick Mutuma na watamalizana nae kwa siri sana arejee DR Congo. Mchezaji huyo raia wa Zimbabwe, ni miongoni mwa wachezaji walioko kwenye rada ya Mwinyi Zahera ambaye amepanga kukamilisha usajili wa Yanga mwezi ujao. Tayari kocha huyo mwenye uraia wa Ufaransa ameshapewa advansi aliyotaka ya Sh.Mil 80 kumalizana na baadhi ya wachezaji wakae mkao wa kula. Habari za uhakika ambazo Spoti Xtra imezipata ni kwamba Mutuma aliyeifungia timu yake bao pekee katika mechi ya ligi dhidi ya TP Mazembe msimu huu, ametua Dar es Salaam wiki iliyopita kwa maagizo ya Zahera na kwamba atamaliza dili yake wikiendi hii kwa siri. Mmoja wa viongozi wa Yanga aliidokeza Spoti Xtra kuwa wameamua kufanya hivyo kutokana na hali halisi iliyoko klabuni na wanataka kumalizana na wachezaji wote muhimu kwa wakati. Habari zinasema kwamba mchezaji huyo amefichwa na moja ya hoteli Jijini Dar es Salaam na haipaswi kuvuja mpaka msimu umalizike. Alisema kwamba

JKT TANZANIA YAPANIA KUISIMAMISHA SIMBA KESHO

Image
KOCHA Mkuu wa JKT Tanzania, Abdallah Mohamed 'Bares' amesema kuwa kesho atapambana kupata matokeo mbele ya Simba kutokana na maandalizi aliyoyafanya kwa muda aliokuwa na kikosi. Bares ambaye mchezo wake wa kwanza alishinda mbele ya Mbeya City, kesho atashusha muziki mzito kuimaliza Simba ambayo ipo kwenye kampeni ya kushinda mechi zake ili kutetea ubingwa. "Tumejipanga kupata matokeo mbele ya Simba, tupo tayari na tuna imani ya kupata matokeo mbele ya kikosi cha Simba kesho. "Nakitambua vema kikosi cha Simba pamoja na mbinu zake hivyo hawanipi shinda, nimewapa mbinu mpya na kali vijana wangu, hivyo sapoti ya mashabiki muhimu," amesema Bares. Mchezo huo utachezwa kesho Uwanja wa Uhuru, majira ya saa 10:00 Jioni.

SIMBA YAIJIBU KIANA YANGA, YAJIPA UBINGWA WAO KWA HESABU KALI

Image
UONGOZI wa Simba umesema kuwa kwa sasa kilichobaki kwa kila timu ni lazima ishinde mechi zake ili kubeba ubingwa na hilo likiwezekana watakaa juu kwa tofauti ya pointi 10 huku wapinzani wao Yanga wakiendelea kupeta. Ofisa wa Habari wa Simba, Haji Manara amesema kuwa ubingwa wa ligi upo mikononi mwao hivyo wana uhakika wa kuutwaa tena msimu huu. "Sisi ni mabingwa wa Taifa hili na ubingwa wa msimu huu upo milkononi mwetu, yaani kila mtu akishinda zake tutakaa juu kwa points kumi. "Tukutane kesho pale Uwanja wa Uhuru kuzisaka tatu pointi tatu muhimu, s logan yetu k ila mtu ashinde zake hesabu tutazikuta mwambani," amesema Manara. Kama Simba atashinda mechi zake 11 zilizobaki itajikusanyia jumla ya pointi 33 na kufanya wawe na jumla ya pointi 102, Yanga kama watashinda mechi zote 5 zilizobaki itajikusanyia pointi 15 na kufanya ifikishe jumla ya pointi 92.

YANGA MOTO CHINI, WAJIKITA KILELENI KIBABE, VITA YA UBINGWA YANOGA

Image
KIKOSI cha Yanga leo kimeendeleza moto wake kwenye Ligi Kuu Bara baada ya kuinyoosha kwa bao 1-0 timu ya Mabingwa wa Afrika Mashariki na Kati Azam FC mchezo uliochezwa Uwanja wa Uhuru. Azam FC iliyo chini ya Idd Cheche ilianzisha muziki kamili kwa ajili ya kuivaa Yanga ujanja ulioshtukiwa mapema na Kocha wa Yanga, Mwinyi Zahera aliyeamua kuanza na mbinu ya kushambulia kwa kushtukiza kipindi cha kwanza. Bao pekee la ushindi lilifungwa na Mrisho Ngassa dakika ya 13 baada ya kutumia pasi ya Ibrahim Ajibu uliomshinda mlinda mlango wa Azam FC, Razack Abarola. Mpaka dakika 90 zinakamilika hakuna mshambuliaji wa Azam aliyeweza kufumania nyavu zilizokuwa chini ya Klaus Kindoki ambaye alikuwa akilindwa vilivyo na beki Abdalah Shaibu 'Ninja'. Ushindi wa leo unaongeza vita ya ubingwa kwa Yanga baada ya kufikisha jumla ya pointi 77 baada ya kucheza michezo 33 kwenye ligi. Azam FC wanabaki nafasi ya tatu wakiwa na pointi zao 66 huku wakiwa na michezo mitano mkononi ili kumaliza mzun

YANGA SC YAINYAMAZISHA AZAM FC UHURU, YAICHAPA 1-0 BAO PEKEE LA MRISHO NGASSA

Image
Na Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM YANGA SC imeibuka na ushindi wa 1-0 dhidi ya Azam FC katika mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara uliofanyika Uwanja wa Uhuru, zamani Taifa mjini Dar es Salaam. Shujaa wa Yanga SC leo ni mchezaji wake kipenzi cha mashabiki, Mrisho Khalfan Ngassa aliyefunga bao hilo pekee dakika ya 13 akimalizia krosi nzuri ya kiungo mwenzake mshambuliaji, Ibrahim Ajibu Migomba. Kwa ushindi huo, Yanga SC inafikisha pointi 77 baada ya kucheza mechi 33 ikiendelea kuongoza Ligi Kuu mbele ya mabingwa watetezi, Simba SC wenye pointi 69 za mechi 27, wakati Azam FC inabaki nafasi ya tatu na pointi zake 66 za mechi 33. Yanga SC leo iliingia na maarifa ya kucheza kwa makini zaidi, ikijilinda zaidi na kushambulia kwa kushitukiza, huku Azam FC wakionekana bora tangu mwanzo wa mchezo. Na baada ya kupata bao lake hilo moja pekee la ushindi, Yanga SC ikazidisha mchezo wa kujihami na pamoja na Azam FC kuuteka mchezo na kushambulia zaidi, lakini hawakufanikiwa kupata bao. Yanga il