Posts

Showing posts from April, 2023

TANESCO YAJISAFISHA TATIZO LA TAA UWANJA WA MKAPA

Image
SHIRIKA la Umeme Tanzania (TANESCO) limetolea ufafanuzi tatizo la taa wakati wa mchezo wa marudiano wa Robo Fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika baina ya Yanga na Rivers United ya Nigeria leo Uwanja wa Benjamín Mkapa Jijini Dar es Salaam. Taa zilififia dakika ya 27 kabla ya kuzimika kabisa wakati wa mchezo huo na kulazimisha timu kurejea vyumbani kwa takriban dakika 20 na zilipowaka vikosi vikarejea kumalizia mechi. Yanga SC imefanikiwa kwenda Nusu Fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika licha ya sare ya bila kufungana na Rivers United wakinufaika ushindi wa 2-0 ugenini kwenye mchezo wa kwanza Jumapili iliyopita Nigeria, mabao ya mshambuliaji Mkongo, Fiston Kalala Mayele. Yanga sasa itamenyana na Marumo Gallants ya Afrika Kusini ambayo imeitoa Pyramids ya Misri kwa jumla ya mabao 2-1, ikitoa sare ya 1-1 Cairo wiki iliyopita na kushinda 1-0 leo Phokeng, NW. Mechi ya kwanza Yanga na Marumo Gallants itafanyika Dar es Salaam Mei 10 na marudiano yatafuatia Afrika Kusini Mei 17.

ROBERTINHO AELEKEZA NGUVU ZAKE UBINGWA WA LIGI KUU YA TANZANIA BARA

Image
KOCHA Mbrazil wa Simba, Robert Oliveira ‘Robertinho’ amesema kwamba amehamishia nguvu zake kwenye Ligi Kuu ya Tanzania Bara baada ya kutolewa katika Ligi ya Mabingwa Afrika. Mbio za Simba SC katika Ligi ya Mabingwa Afrika kwa mara nyingine ziliishia hatua ya Robo Fainali baada ya kutolewa na mabingwa watetezi, Wydad Club Athletic Ijumaa kwa penalti 4-3  Uwanja wa Mohamed V Jijini Casablanca, Morocco. Dakika 90 zilimalizika kwa Wydad AC kushinda 1-0, bao pekee la mshambuliaji Msenegal, Bouly Junior Sambou dakika ya 24 kwa kichwa na kufanya sare ya jumla ya 1-1 kufuatia Simba kushinda 1-0 kwenye mchezo wa kwanza wiki iliyopita Dar es Salaam, bao la mshambuliaji Mkongo Jean Othos Baleke dakika ya 31. Kuelekea mechi nne za mwisho za Ligi Kuu, Simba inashika nafasi ya pili kwa pointi zake 63, ikizidiwa pointi tano na mabingwa watetezi, Yanga SC baada ya wote kucheza mechi 26. Wekundu hao wa Msimbazi wana mechi moja tu ugenini dhidi ya Namungo FC Jumatano Uwanja wa Majaliwa, Ruangwa m

MAN UNITED WAIZABA ASTON VILLA 1-0 OLD TRAFFORD

Image
BAO pekee la Bruno Fernandes dakika ya 39 limeipa Manchester United ushindi wa 1-0 dhidi ya Aston Villa leo Uwanja wa Old Trafford Jijini Manchester na kujiongezea matumaini ya kufuzu Ligi ya Mabingwa Ulaya msimu ujap. Ushindi unaifanya Manchester United ifikishe pointi 63 katika mchezo wa 32, ingawa wanabaki nafasi ya nne wakizidiwa pointi mbili na Newcastle United ambayo pia imecheza mechi moja zaidi, wakati Aston Villa inabaki na pointi 54 za mechi 34 nafasi ya sita.

WENYE TAJI LAO MAN CITY YAREJEA KILELENI LIGI KUU ENGLAND

Image
MABINGWA watetezi, Manchester City wamerejea kileleni mwa Ligi Kuu ya England baada ya ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya wenyeji, Fulham leo Uwanja wa Craven Cottage Jijini London. Mabao ya Manchester City yamefungwa na washambuliaji Mnorway, Erling Haaland kwa penalti dakika ya tatu na Muargentina Julian Álvarez dakika ya 36, wakati la Fulham limefungwa na Carlos Vinícius dakika ya 15. Kwa ushindi huo, Manchester City imefikisha pointi 76 katika mchezo wa 32 na kurejea juu ya msimamo wakiizidi pointi moja Arsenal ambayo pia imecheza mechi moja zaidi, huku Fulham ikibaki na pointi zake 45 za mechi 33 nafasi ya 10.

NUSU FAINALI LIGI YA MABINGWA NI AL AHLY V ESPERANCE NA MAMELODI V WYDAD

Image
VIGOGO wa Afrika, Al Ahly wamefanikiwa kwenda Nusu Fainali ya Ligi ya Mabingwa baada ya sare ya bila kufungana na wenyeji, Raja Club Athletic jana Uwanja wa Mohamed V Jijini Casablaca nchini Morocco. Matokeo hayo yanawafanya waende Nusu Fainali baada ya ushindi wa 2-0 kwenye mchezo wa kwanza, nyumbani nchini Misri na watakutana na Esperance ya Tunisia ambayo imeitoa JS Kabylie ya Algeria. Nyota Mualgeria, Yousri Bouzouk aliinyima nafasi ya kufunga Al Ahly dakika ya 45 baada ya kupiga nje penalti kufuatia yeye mwenyewe kuangushwa na kiungo wa Kimataifa wa Mali, Aliou Dieng. Na ilikuwa nafasi ya pili Yousri Bouzouk anapoteza baada ya dakika ya 28 kupata mpira akiwa eneo zuri la kufunga, lakini shuti lake likaokolewa na kipa Mohamed Elshenawy. Esparence ilishinda 1-0 mechi ya kwanza Algeria wiki iliyopita kabla ya jana kulazimisha sare ya 1-1 Tunis. Mechi nyingine za marudiano za Robo Fainali, wenyeji Mamelodi Sundowns wameitoa Belouizdad baada ya kuichapa 2-1 jana Afrika Kusini n

TFF YASHUTUSHWA NA TUHUMA ZA RUSHWA LIGI YA CHAMPIONSHIP

Image
SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF) limesema kwamba linafuatilia kwa karibu tuhuma za rushwa katika mchezo wa Ligi ya Championship baina ya Fountain Gate na Kitayosce uliofanyika jana Uwanja wa CCM Gairo mkoani Morogoro na kumalizika kwa sare ya bila mabao.

MAYELE APEWA JEZI YA HESHIMA YA MABAO 50 YANGA

Image
WACHEZAJI wa Yanga SC leo wamemkabidhi mwenzao, mshambuliaji Mkongo Fiston Kalala Mayele jezi ya idadi ya mabao aliyofunga hadi sasa, 50 zoezi ambalo limefanyika kambini kwao Uwanja wa Avic Town, Kigamboni nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam. Na imekuwa siku moja kabla ya mchezo wa marudiano wa Robo Fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Rivers United ya Nigeria kesho Uwanja wa Benjamín Mkapa Jijini Dar es Salaam. Katika mchezo huo utakaoanza Saa 2:00 usiku Yanga inahitaji hata sare ili kwenda Nusu Fainali baada ya ushindi wa 2-0 kwenye mchezo wa kwanza wiki iliyopita Nigeria. VÍDEO ALICHOZUNGUMZA FISTONll KALALA MAYELE BAADA YA KUKABIDHIWA JEZI YA MABAO 50

JKT, KITAYOSCE NA PAMBA ZOTE ZATOA SARE CHAMPIONSHIP

Image
TIMU za JKT Tanzania, Kitayosce na Pamba FC zote zimetoa sare katika mechi zao za leo za Ligi ya Championship na kufanya msimamo uendelee kusomeka kama ulivyokuwa. JKT Tanzania imefungana mabao 3-3 na Mashujaa Uwanja wa Meja Jenerali Isamuhyo huko Mbweni, Dar es Salaam, Pamba imefungana bao 1-1 na African Sports Uwanja wa Mkwakwani Jijini Tanga na Kitayosce haijafungana na Fountain Gate Uwanja wa CCM Gairo mkoani Morogoro. Msimamo wa Championship sasa JKT Tanzania ambayo tayari imekwishapanda Ligi Kuu ina pointi 63 za mechi 27, Kitayosce 54 na Pamba FC 53 baada ya wote kucheza mechi 26. Mechi nyingine ya Championship leo Mbeya Kwanza imeichapa Pan Africans 2-1 Uwanja wa Maji Maji mjini Songea. Mbeya Kwanza imefikisha pointi 37 na kusogea nafasi ya saba na Pan Africans sasa ina pointi 24 na kusogea nafasi ya 14 baada ya wote kucheza mechi 26.

WYDAD CASABLANCA 1-0 SIMBA SC (PENALTI 4-3, LIGI YA MABINGWA)

Image
 

SIMBA WALIVYOIANZA SAFARI YA KUREJEA NYUMBANI LEO

Image
KIUNGO wa Simba SC raia wa Mali, Sadio Kanote akiwa Jijini Casablanca, Morocco leo wakati wa safari ya kurejea nyumbani, Dar es Salaam baada ya kutolewa na Wydad Club Athletic katika Ligi ya Mabingwa Afrika kwa penalti 4-3 usiku wa kuamkia leo Uwanja wa Mohamed V kufuatia sare ya jumla ya 1-1, kila timu ikishinda 1-0 kwake. GONGA HAPA KUTAZAMA PICHA ZAIDI

NABI ASEMA DHAMIRA YA YANGA NI KUWAFUNGA TENA RIVERS

Image
KOCHA Mkuu wa Yanga SC, Nasredeen Nabi amesema dhamira yao ni kushinda mchezo wa kesho wa marudiano Robo Fainali Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Rivers United ya Nigeria Uwanja wa Benjamín Mkapa Jijini Dar es Salaam. Akizungumza kwenye mkutano na Waandishi wa Habari leo Jijini Dar es Salaam kuelekea mchezo huo wa kesho Nabi amesema ushindi wa 2-0 kwenye mchezo wa kwanza hautakuwa na maana kama kesho hawatashinda. Mechi ya kwanza Yanga ilishinda 2-0, mabao ya mshambuliaji Mkongo Fiston Kalala Mayele Uwanja wa Venue Godswill Akpabio International mjini Uyo, Nigeria Jumapili iliyopita. Ikumbukwe mshindi wa jumla atakutana na mshindi wa jumla katí ya Pyramids ya Misri na Marumo Gallants ya Afrika Kusini ambazo mechi ya kwanza zilitoka sare ya 1-1 Misri Jumapili iliyopita.

SIMBA SC YAFA KIUME MOROCCO, YATOLEWA KWA MATUTA

Image
SAFARI ya Simba SC katika Ligi ya Mabingwa Afrika kwa mara nyingine leo imeishia hatua ya Robo Fainali baada ya kutolewa na mabingwa watetezi, Wydad Club Athletic kwa penalti 4-3 usiku huu Uwanja wa Mohamed V Jijini Casablanca, Morocco. Dakika 90 zilimalizika kwa Wydad AC kushinda 1-0, bao pekee la mshambuliaji Msenegal, Bouly Junior Sambou dakika ya 24 kwa kichwa na kufanya sare ya jumla ya 1-1 kufuatia Simba kushinda 1-0 kwenye mchezo wa kwanza wiki iliyopita Dar es Salaam, bao la mshambuliaji Mkongo Jean Othos Baleke dakika ya 31. Na katika mikwaju ya penalti, shujaa wa Wydad alikuwa ni kipa Youssef El Motie ayeokoa penalti mbili za beki Shomari Kapombe na kiungo Clatous Chama. Waliofunga penalti za Wydad ni kiungo Yahya Jabrane, mabeki Ayoub El Amloud, Amine Aboulfath na kiungo Abdellah Haimoud wakati waliofunga za Simba ni viungo Erasto Nyoni, Mrundi Said Ntibanzokiza na mshambuliaji Mzambia, Moses Phiri. Sasa Wydad itakutana na mshindi wa jumla katí ya CR Belouizdad ya Al

WIKIENDI YA SHANGWE MERIDIANBET

Image
Wakati   wengi   tukusubiri   kujua   hatma   ya   baadhi   ya   timu kusalia   kwenye   Ligi   zao   na   nyingine   kutwaa   ubingwa , Meridianbet  wametoa  odds  kubwa   mwa   mechi  za  Wikiendi  hii. Kuna  michezo   ya   kasino   ya   mtandaoni  pia  inatoa   ushindi kirahisi ,  chaguo   ni   lako   kubashiri   soka  au  kasino   ya   mtandaoni . Mechi  za  Jumamosi   Meridianbet odds  kubwa   kila   mechi ,  Laliga   kitachafuka miamba   ya   soka  la Hispania FC Barcelona  na  Real Madrid  watashuka   dimbani   kwa   pamoja   kusaka   pointi  3  muhimu ,  ni  Barcelona vs Betis, Real Madrid vs Almeria  nanti   kuondoka   na   ushindi ?   Napoli  vinara   wa  Serie A  watahitaji   kuendelea   kuongoza kwenye   msimamo ,  pale  ambapo   atakutana   na   Sportiva Salernitana  Meridianbet  wanampa   nafasi   ya   ushindi Napoli   kwa  odds  kubwa   ya  1.20  huku   Sportiva   amepewa odds  kubwa   ya  12.74  unaenda  nan ani?  Ukiachana   na ubashiri   wa   soka   kuna   kasino  

SERIKALI KUANGALIA UPYA MGAWANYO WA MAPATO YA MECHI ZA KLABU

Image
NAIBU Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Hamis Mwinjuma ‘Mwana FA’ amesema kwamba Serikali inaangalia upya utaratibu ambao utawezesha klabu kunufaika zaidi na mapato ya milangoni katika mechi. Mwinjuma amesema hayo leo Bungeni Jijini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge wa Iramba Mashariki, Francis Mtinga kuhusu Mgawanyo wa mapato uliotolewa kwenye mechi iliyowakutanisha Simba na Yanga Aprili 16,2023. Mtinga amehoji ni lini Serikali itapitia upya utaratibu wa mgawanyo wa mapato baada ya Simba kupewa Shilingi Milioni 180 pekee kati ya Miliomi 450 zilizopatikana kwenye mchezo dhidi ya Yanga. “Tunaangalia utaratibu ambao utawezesha vilabu vyetu kunufaika zaidi, lakini kuna gharama kubwa za uendeshaji wa michezo inayotajwa na taasisi zetu zinaingia gharama kubwa ambayo inatoka mifukoni kwao kuweza kuifanya michezo hii ifanikiwe,”. “Kwa hiyo pamoja na lengo letu la kuhakikisha timu zetu zinafaidika lakini kuna gharama kubwa za uendeshaji na taasisi zetu zitashindwa kujiendesha ka

MAZOEZI YA MWISHO SIMBA SC KABLA YA OPERESHENI CASABLANCA KESHO

Image
WACHEZAJI wa Simba wakiwa mazoezini leo Uwanja wa Mohamed V Jijini Casablanca nchini Morocco kujiandaa na mchezo wa marudiano Robo Fainali Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Mabingwa watetezi, Wydad AC kesho. Mechi ya kwanza Simba ilishinda 1-0, bao la mshambuliaji Mkongo Jean Othos Baleke Jumamosi ya wiki iliyopita Uwanja wa Benjamín Mkapa Jijini Dar es Salaam. Mshindi wa jumla atakutana na mshindi wa jumla katí ya CR  Belouizdad ya Algeria na Mamelodi Sundowns ya Afrika Kusini zinazorudiana  Uwanja wa Loftus Versfeld mjini Pretoria. Mechi ya kwanza Mamelodi ilishinda 4-1 Uwanja wa Nelson Mandela mjini Baraki, Algiers, Algeria. GONGA HAPA KUTAZAMA PICHA ZAIDI

WAZIRI WA MICHEZO AWAZAWADIA MAMILIONI WANARIADHA GEAY NA SIMBU

Image
WAZIRI wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana (kulia) akimkabidhi zawadi ya Shilingi Milioni 3 Mwanariadha wa Kimataifa Gabriel Geay ambaye ameshika nafasi ya pili katika Mashindano ya Kimataifa ya Riadha (Buston Marathon) yaliyofanyika hivi  karibuni nchini Marekani. Kulia ni Naibu Waziri wa Wizara hiyo Mhe. Hamis Mwinjuma. Fedha hizo zimetolewa na Wizara ya  Utamaduni, Sanaa na Michezo. WAZIRI wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana akimkabidhi zawadi ya Shilingi Milioni 2 iliyotolewa na wizara hiyo, kwa  Mwanariadha wa Kimataifa Aliphonce Simbu (katikati)  ambaye ameshika nafasi ya tatu katika mbio za Yangzhou Jianzhen International Half Marathon. Kulia ni Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Mhe. Hamis Mwinjuma. Tukio hilo limefanyika leo Aprili 27, 2023 jijini Dodoma. PICHA ZAIDI GONGA HAPA