Posts

Showing posts from May, 2019

NI LIVERPOOL AU TOTTENHAM KUBEBA TAJI LA LIGI YA MABINGWA MADRID LEO?

Image
Wachezaji wa Liverpool wakifanya mazoezi jana Uwanja wa Wanda Metropolitano mjini Madrid kuelekea fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya usiku wa leo uwanjani hapo dhidi ya wapinzani wao wa England, Tottenham Hotspur, pichani chini wakifanya mazoezi uwanjani hapo pia, Nani kubeba taji hilo leo, Liverpool au Spurs?   PICHA ZAIDI GONGA HAPA    

NI ESPERANCE TENA MABINGWA WA AFRIKA, WAIPIGA WYDAD 1-0 TUNISIA

Image
WENYEJI Esperance wamefanikiwa kutwaa taji la Ligi ya Mabingwa Afrika baada ya ushindi wa 1-0 dhidi ya Wydad Casablanca ya Morocco bao pekee la mshambuliaji Mualgeria Mohamed Youcef Belaili dakika ya 41 akimaliia pasi ya kiungo Mtunisia, mzaliwa wa England Ayman Ben Mohamed Uwanja wa OlImpiki mjini Rades, Tunisia. Kwa matokeo hayo, Esperance inayofundishwa na kocha Mtunisia, Moine Chaabani inabeba taji hilo kwa ushindi wa jumla wa 2-1 kufuatia sare ya 1-1 kwenye mchezo wa kwanza Uwanja wa Prince Moulay Abdallah mjini Rabat. Siku hiyo, wageni Esperance wakitangulia kwa bao la dakika ya 44 la Fousseny Coulibaly kabla ya Cheick Comara kuisawazishia Wydad dakika ya 79, wafungaji wote raia wa Ivory Coast. Wachezai wawili tu walionyeshwa kadi za njano usiku wa kuamkia leo, kiungo Muivory Coast, Coulibaly dakika ya 10 na Belaili dakika ya 42. Hilo linakuwa taji la pili mfululizo kwa Esperance na la nne jumla kihistoria, baada ya awali kulitwaa katika miaka 1994, 2011 na 2018. Kikosi ch

MAREFA WATANO KUCHEZESHA FAINALI ASFC AZAM FC NA LIPULI KESHO UWANJA WA ILULU

Image
Na Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF), limemtangaza Hance Mabena (pichani) kutoka Tanga kuwa mwamuzi wa mchezo wa fainali ya Kombe la shirikisho la hilo, maarufu kama Azam Sports Federation Cup (ASFC) utakaopigwa kesho Jumamosi Uwanja wa Ilulu mjini Lindi. Katika mchezo huo watatumika waamuzi sita kwa mara ya kwanza kwenye historia ya soka la Tanzania ambapo Mabena atasaidiwa na jumla ya waamuzi watano, wawili wa pembeni, wawili wa kwenye magoli na mmoja wa akiba. Mfumo wa kuwa na waamuzi sita ulianza kutumiwa na Shirikisho la Soka Afrika (CAF) kwenye AFCON ya vijana chini ya miaka 17 iliyofanyika nchini mwezi Aprili 2019. Kwa mujibu wa taarifa ya TFF iliyotolewa leo, Hance Mabena atasaidiwa na Mohamed Mkono kutoka Tanga kama mwamuzi msaidizi namba moja, Frednarnd Chacha kutoka Mwanza kama mwamuzi msaidizi namba 2, na Abubakar Mturo kutoka Mtwara atakuwa ni mwamuzi wa akiba. Waamuzi wasaidizi walioteuliwa kukaa kwenye magoli ni Martin Sanya kutoka Mor

JOSHUA NA RUIZ SHUGHULI NI JUMAMOSI MADISON SQUARE GARDEN

Image
Bingwa wa dunia wa uzito wa juu duniani, Anthony Joshua (kushoto) akitazamana kimikwara na mpinzani wake, Andy Ruiz Jr (kulia) jana wakati wa mkutano na Waandishi wa Habari kuelekea pambano lao la Jumamosi ukumbi Madison Square Garden mjini New York, Marekani.  Joshua mwenye urefu wa futi sita kwa sasa anashikilia mataji ya IBF, WBA na WBO akiwa na rekodi ya kushinda mapambano yake yote 22, 21 kwa knockout, wakati  Ruiz mwenye urefu wa futi nne amepoteza pambano  moja na kushinda 32, huku 21 akishinda kwa knockout pia.   PICHA ZAIDI GONGA HAPA  

BRAZIL HATARINI KUMKOSA NEYMAR MECHI NA BOLIVIA COPA AMERICA

Image
Neymar akifanya mazoezi peke yake Gym baada ya kuumia Jumanne kwenye kambi ya Brazil huko Granja Comary nje kidogo ya Jiji la Rio de Janeiro kujiandaa na michuano ya Copa America inayotarajiwa kuanza Juni 14 Brazil ikimenyana na Bolivia mjini Sao Paulo  PICHA ZAIDI GONGA HAPA  

KAGERE AWA MCHEZAJI BORA WA MWAKA SIMBA SC, OKWI ATOKA MIKONO MITUPU

Image
Na Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Rwanda, Meddie Kagere ameibuka kinara katika tuzo za Mo Simba kwa kushinda tuzo mbili – Mchezaji Bora na Mfungaji Bora wa Mwaka katika usiku ambap nyota Mganda, Emmanuel Okwi ametoka mikono mitupu. Kagere aliye katika msimu wake wa kwanza Simba SC tangu ajiunge nayo kutoka Gor Mahia ya Kenya katika tuzo ya Mchezaji Bora wa Mwaka amewashinda Nahodha na mshambuliaji mwenzake, John Raphael Bocco na kiungo Mzambia, Clatous Chama. Tuzo ya ufungaji bora amepewa moja kwa moja kwa kuwa mfungaji bora wa msimu wa klabu na mfungaji bora wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara akiiwezesha na timu yake kutwaa taji hilo.  Mshambuliaji wa kimataifa wa Rwanda, Meddie Kagere ndiye Mchezaji Bora wa Mwaka Simba SC  Beki anayeweza kucheza nafasi za kiungo pia, Erasto Edward Nyoni naye pia amepata tuzo mbili, Mchezaji Bora wa Wachezaji na Beki Bora wa Mwaka. Katika tuzo ya Beki Bora amewashinda Muivory Coast Serge Wawa Pascal na mchezaji mwenzake wa

ADI YUSSUF AWA MCHEZAJI WA KWANZA KUSAJILIWA BLACKPOOL YA LIGUE 1 ENGALND

Image
Na Mwandishi Wetu, LANCASHIRE  MSHAMBULIAJi chipukizi wa kimataifa wa Tanzania, Adi Yussuf amekuwa mchezaji wa kwanza kabisa dirisha hili kusajiliwa na timu ya Blackpool FC inayoshiriki Ligi Daraja la Pili England ijulikanayo kama Ligue 1. Yussuf mzaliwa wa kisiwani Zanzibar, amesaini mkataba wa miaka miwili kujiunga na timu hiyo inayoshiriki Ligi ya tatu kwa ukubwa England baada ya Ligi Kuu na Daraja la Kwanza, huku kukiwa na kipengele cha kuongezewa mwaka mmoja akifanya vizuri. Yussuf mwenye umri wa miaka 27 sasa, anajiunga na Blackpool yenye maskani yake Lancashire akitokea Solihull Moors kama mchezaji huru. Adi Yussuf amekuwa mchezaji wa kwanza dirisha hili kusajiliwa na Blackpool FC ya Ligue 1 England Baada ya kufunga mabao 21 katika mashindano yote Solihull Moors, yakiwemo mawili dhidi ya Seasiders kwenye mchezo wa marudiano wa Raundi ya Pili ya Kombe la FA na kuiwezesha timu hiyo kumaliza nafasi ya pili kwenye National League, Yussuf ameamua kwenda kujaribu changamoto mpya

CHELSEA YAIFUMUA ARSENAL 4-1 NA KUTWAA 'NDOO' YA EUROPA LEAGUE

Image
Wachezaji wa Chelsea wakimpongeza mwenzao, Olivier Giroud baada ya kufunga bao la kwanza dakika ya 49 katika ushindi wa 4-1 dhidi ya timu yake ya zamani, Arsenal usiku wa Jumatano kwenye fainali ya UEFA Europa League Uwanja wa Bakı Olimpiya mjini Baku, Azerbaijan. Mabao mengine ya Chelsea yamefungwa na Pedro dakika ya 60 na Edin Hazard mawili, dakika yaa 65 kwa penalti na 72, wakati la Arsenal limefungwa na Alex Iwobi dakika ya 69   PICHA ZAIDI GONGA HAPA

RAIS WA FIFA, INFANTINO AIPONGEZA SIMBA SC KWA KUTWAA TENA UBINGWA WA LIGI KUU

Image
Na Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM RAIS wa Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA) Gianni Infantino ametuma salamu za pongezi kwa Klabu ya Simba kwa kutwaa Ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara. Infantino ametuma salamu hizo za pongezi kupitia kwa Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) Wallace Karia. Katika Salamu hizo Infantino amesema amefurahishwa kusikia Simba SC wamevikwa taji la Ubingwa wa Ligi Kuu 2018/2019 ikiwa ni mara ya pili mfululizo jambo ambalo ni la kupongezwa. Amesema hayo ni majibu ya jitihada na juhudi na ameomba salamu hizo zifikishwe kwa uongozi, wachezaji, kocha na benchi lake zima la ufundi, Madaktari pamoja na mashabiki na kuwataka kuendeleza uthubutu na hamasa. Rais wa FIFA, Gianni Infantino (kushoto) akiwa na Waziri Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa   Infantino kwa niaba ya Jamii ya Mpira Kimataifa ameishukuru Simba na TFF kwa kusaidia kusambaza ujumbe chanya wa Mpira wa Miguu ambao unajumuisha watu wote. Akimalizia salamu zake kwa Rais wa TFF,In

MTIBWA SUGAR 0-0 SIMBA SC (LIGI KUU TZ BARA)

Image

YANGA SC 0-2 AZAM FC (LIGI KUU TZ BARA)

Image

TAIFA STARS KUINGIA KAMBINI JUMAMOSI HOTELI YA WHITE SANDS MAANDALIZI YA AFCON

Image
Na Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM TIMU ya soka ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars itaingia kambini Juni 1 katika hoteli ya White Sands mjini Dar es Salaam kujiandaa Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) baadaye mwezi huu nchini Misri. Akizungumza na Waandishi wa Habari leo mjini Dar es Salaam, Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Wallace Karia amesema kwamba hoteli ya White Sands imejitolea kuisaidia Taifa Stars kambi ya awali ya wiki moja kwa maandalizi ya AFCON. Karia amesema kwamba Taifa Stars itaingia kambini White Sands Juni 1 hadi 7 kwa maandalizi ya awali ya AFCON kabla ya kikosi kwenda Alexandria. Amesema kikosi kitaondoka na wachezaji 32 baada ya kuchujwa saba kutoka 39 walioitwa na kati ya hao ni 23 tu watashiriki AFCON. Karia amesema wachezaji wengine wataendelea kubaki kambini kwa maandalizi ya michuano ya Ubingwa wa Mataifa ya Afrika (CHAN), inayohusisha wachezaji wanaocheza ligi za nchini mwao pekee. Kikosi cha kocha Mnigeria, Emmanuel Amunike kitaanza

NI ARSENAL AU CHELSEA KUBEBA 'NDOO' YA UEFA EUROPA LEAGUE LEO BAKU?

Image
TIMU za Arsenal na Chelsea tayari wako jijini Baku kwa ajili ya fainali ya Europa usiku wa leo, London ni jiji la pili tu kuwahi kufikisha timu mbili katika fainali ya mashindano ya vilabu Ulaya. Madrid ndio lilikuwa jiji la kwanza na wamefanya hivyo mara mbili, 2014 na 2016 ambapo Real na Atletico walifika fainali pamoja, lakini mwaka huu ni zamu ya London. Kocha wa Arsenal Unai Emery, ambaye amewahi kushinda Kombe hilo mara tatu mfululizo akiwa na Sevilla ana changamoto kubwa kwenye kupanga kikosi chake katika nafasi ya mlinda mlango. Pert Cech, ambaye amekuwa akidaka kwenye mechi za Europa, anahusishwa kujiunga na Chelsea kwenye nafasi ya Mkurugenzi wa Ufundi. Baadhi ya wachambuzi wanashauri Emery kutokana na hali ilivyo amuanzishe mlinda mlango chaguo la kwanza Bernd Leno nafasi ya kuanza kwenye mchezo huo jijini Baku. Emery atamkosa kiungo mshambuliaji Henrikh Mkhitaryan, ambaye hakusafiri na timu inayokwenda kucheza katika dimba la Olympic Stadium kwenye mji mkuu wa Azerbai

KAGERA SUGAR KUMENYANA NA PAMBA, MWADUI FC NA GEITA GOLD KATIKA ‘PLAY-OFFS’

Image
Na Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM BODI ya Ligi Tanzania Bara (TPLB) imetoa ufafanuzi kuhusu nafasi zinapopaswa kukaa timu za Stand United na Kagera Sugar kwenye msimamo wa ligi kuu 2018/19 baada ya mechi za mwisho kuhitimishwa jana. Akizungumza na wanahabari leo, Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Ligi Boniface Wambura amesema timu inayostahili kukaa nafasi ya 19 na kushuka daraja moja kwa moja ni Stand United huku Kagera Sugar ikistahili kukaa nafasi ya 18. Wambura amesema licha ya timu hizo kulingana pointi, kwa timu zote kuwa na pointi 44, Kagera Sugar ina faida ya kuwa na tofauti kubwa ya magoli ya kufunga na kufungwa ambayo ni -10 wakati Stand United ina tofauti ndogo ya magoli ya kufunga na kufungwa ambayo ni -12. Kwa ufafanuzi huo, Kagera Sugar na Mwadui FC sasa watalazimika kupitia kwenye hatua ya mtoano (Play-Off) dhidi ya timu zilizotoka daraja la kwanza ili kujinusuru na janga la kushuka daraja wakati Stand United ikiungana na African Lyon kushuka daraja moja kwa moja. Mechi za

JOSHUA AFANYA MAZOEZI YA WAZI NEW YORK KABLA YA KUMVAA RUIZ

Image
BINGWA wa ngumi uzito wa juu duniani, Anthony Joshua (kulia) amefanya mazoezi ya wazi leo mjini New York kuelekea pambano lake na Andy Ruiz Juni 1 mjini humo siku ambayo pia mabondia wa kike Delfine Persoon na Katie Taylor watapigana. Joshua mwenye urefu wa futi sita kwa sasa anashikilia mataji matatu kati ya manne; IBF, WBA na WBO akiwa na rekodi ya kushinda mapambano yake yote 22, kati ya 21 kwa knockout. Ruiz mwenye urefu wa futi nne amepoteza pambano moja na kushinda 32, huku 21 akishinda kwa knockout pia. Delfine Persoon wa Ubelgiji ndiye bingwa wa taji la WBC uzito wa Light na Katie Taylor wa Ireland anashikilia mataji ya WBA, IBF na WBO uzito huo wa Light   PICHA ZAIDI GONGA HAPA .

CHELSEA HATARINI KUMKOSA KANTE LEO MECHI NA ARSENAL BAKU

Image
Kiungo Mfaransa, N'Golo Kante akifanya mazoezi ya peke yake jana Uwanja wa Baku baada ya kuumia Jumamosi mazoezini kuelekea fainali ya Europa League usiku wa leo dhidi ya Arsenal  PICHA ZAIDI GONGA HAPA

SIMBA SC WAKABIDHIWA KOMBE BAADA YA DROO NA MTIBWA SUGAR MOROGORO

Image
Na Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM MABINGWA wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara, Simba SC wamekabidhiwa Kombe lao baada ya sare ya 0-0 na wenyeji, Mtibwa Sugar katika mchezo wa mwisho wa ligi hiyo jioni ya leo Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro. Simba SC inayofundishwa na kocha Mbelgiji, Patrick Aussems imemaliza Ligi Kuu na pointi 93, zikiwa ni saba zaidi ya watani wao wa jadi, Yanga SC waliomaliza na pointi 86 katika nafasi ya pili, wakati Azam FC imeshika nafasi ya tatu kwa pointi zake 75. Hilo linkuwa taji la pili mfululizo la ubingwa wa Ligi Kuu kwa Simba SC na la 20 jumla kihistoria baada ya awali kulibeba katika miaka ya 1965, 1966, 1973, 1976, 1977, 1978, 1979, 1980, 1984, 1990, 1994, 1995, 2001, 2003, 2004, 2007, 2010, 2012 na 2018. Watani wao, Yanga SC ndio mabingwa mara nyingi zaidi wa Ligi Kuu, mara 27 wakiwa wamebeba taji hilo miaka ya 1968, 1969, 1970, 1971, 1972, 1974, 1981, 1983, 1985, 1987, 1989, 1991, 1992, 1993, 1996, 1997, 1998, 2002, 2005, 2006, 2008, 2009, 2011, 2013, 20

AZAM FC YAMALIZA LIGI KUU KWA USHINDI, YAICHAPA YANGA 2-0 UWANJA WA TAIFA TAIFA

Image
Na Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM TIMU ya Azam FC imemaliza vyema Ligi Kuu ya Tanzania Bara baada ya ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya vigogo, Yanga SC jioni ya leo Uwanja wa Taifa mjini Dar es Salaam. Pamoja na ushindi huo, Azam FC imemaliza katika nafasi ya tatu kwenye msimamo wa Ligi Kuu kwa pointi zake 75 nyuma ya vigogo wengine, Simba SC walioibuka mabingwa kwa pointi zao 93 na Yanga waliomaliza na pointi 86.  Katika mchezo wa leo, mabao ya Azam FC yamefungwa na beki wake Mghana, Daniel Amoah dakika ya 45 na ushei na kiungo Mzanzibari, Mudathir Yahya dakika ya 50. Ushindi huo ni sawa na kisasi kwa Azam FC baada ya kufungwa 1-0 na Yanga SC katika mchezo wa mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu Uwanja wa Uhuru.  Wakati Simba SC ikitwaa ubingwa wa Ligi Kuu kwa mara ya pili mfululizo, Stand United imeungana na African Lyon kuteremka daraja baada ya kufungwa 2-0 na JKT Tanzania.  Nazo Kagera Sugar ya Bukoba na Mwadui FC ya Shinyanga zitamenyana na timu za Daraja la Kwanza, Pamba SC na geita

STAND UNITED ‘CHAMA LA WANA’ YASHUKA DARAJA, KAGERA NA MWADUI ZAANGUKIA ‘KAPUNI’

Image
Na Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM TIMU ya Stand United ya Shinyanga, maarufu kama Chama la Wana’ leo imeipa mkono wa kwaheri Ligi Kuu ya Tanzania Bara baada ya kuchapwa mabao 2-0 na JKT Tanzania 2-0 Uwanja wa Meja Isamuhyo, Mbweni mjini Dar es Salaam. Mabao yaliyoizamisha Stand United leo yamefungwa na washambuliaji wa JKT Tanzania, Samuel  Kamuntu dakika ya 51 na Najim Magulu dakika ya 73. JKT Tanzania iliyorejea msimu huu Ligi Kuu, imenusurika kushuka baada ya kumaliza na pointi 47 katika nafasi ya 10, wakati Stand United imemaliza nafasi ya 19 kwa pointi zake 44, ikiungana na African Lyon kuteremka daraja. Nazo Kagera Sugar ya Bukoba na Mwadui FC ya Shinyanga zitamenyana na timu za Daraja la Kwanza, Pamba SC na geita Gold kuwania kubaki Ligi Kuu katika mechi za mchujo. Hiyo ni baada ya Kagera Sugar inayofundishwa na Nahodha wa zamani wa timu ya taifa ya Tanzania, Mecky Mexime kulazimishwa sare ya 1-1 na Mbao FC Uwanja wa CCM Kirumba mjini Mwanza na Stand United kushinda 3-1 dhid

CHEKI AMBAVYO RONALDO NI MTU MBAYA DUNIA NZIMA HAKUNA KAMA YEYE!

Image
Cristiano Ronaldo akionyesha uwezo wake mkubwa kisoka kwa kubinuka tik tak katika mchezo wa kirafiki wa Hisani wa Juventus jana Uwanja wa Allianz mjini Torino   PICHA ZAIDI GONGA HAPA

WENGER ALIVYOMKOKOTA KAMA BEHEWA ZIDANE MECHI YA HISANI JANA

Image
Kocha wa zamani wa Arsenal, Arsene Wenger akimtoka nyota wa zamani wa Ufaransa na Real Madrid, Zinedine Zidane katika mechi ya hisani jana mjini  Bordeaux, Ufaransa   PICHA ZAIDI GONGA HAPA  

VILLA WAIPIGA DERBY 2-1 NA KUREJEA LIGI KUU ENGLAND

Image
Wachezaji wa Aston Villa wakishangilia baada ya kuifunga 2-1 Derby County usiku wa jana Uwanja wa Wembley katika mechi ya fainali ya mchuji wa kupanda wa Ligi Kuu England. Mabao ya Villa inayorejea Ligi Kuu tangu ishuke mwaka 2016 yamefungwa na Anwar El Ghazi na John McGinn huku la Derby County likifungwa na Jack Marriott   PICHA ZAIDI GONGA HAPA  

MAHOJIANO MAALUM BIN ZUBEIRY NA BAKARI MALIMA 'JEMBE ULAYA'

Image

ZAMALEK WATWAA TAJI LA KWANZA AFRIKA TANGU WAVULIWE UBINGWA NA SIMBA 2003

Image
TIMU ya Zamalek ya Misiri imefanikiwa kutwaa Kombe la Shirikisho Afrika baada ya ushindi wa penalti 5-3 kufuatia sare ya jumla ya 1-1 dhidi ya Renaissance Sportive Berkane, maarufu kama RSB Berkane usiku wa jana Uwanja wa Borg El Arab mjini Alexandria, Bao pekee la penalti la beki Mmisri, Mahmoud Alaa Eldin dakika ya 55 liliipa Zamalek ushindi wa 1-0 ndani ya dakika 120 za mchezo wa jana Misri. Na kufuatia RSB Berkane kushinda 1-0 pia, bao pekee la mshambuliaji Mtogo, Fo-Doh Kodjo Laba dakika ya 90 na ushei akimalizia pasi ya Hamdi Laachir liliipa RSB Berkane Uwanja wa Manispaaa ya Berkane Mei 20 mchezo ukahamia kwenye mikwaju ya penalti. Zamalek ilipata penalti zake zote kupitia kwa nyota wake, Mmorocco mzaliwa wa Ufaransa, Khalid Boutaib, Mahmoud Alaa, Abdallah Gomaa, Youssef Obama na Ahmed Sayed ‘Zizo’.  Lakini  Hamdi Laachir akakosa penlati ya kwanza ya Berkane, wakati Ismail Mokadem, Mtoto Fo-Doh Kodjo Laba na Mburkina Faso, Issoufou Dayo walifunga. Jana ilikuwa mara ya nne

TP MAZEMBE WAAMUA KUACHANA NA AJIBU NA SASA ANAREJEA KLABU YAKE KIPENZI, SIMBA

Image
Na Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM KLABU ya Tout Puissant Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) imeamua kusitisha mpango wa kumsajili kiungo mshambuliaji wa kimataifa wa Tanzania, Ibrahim Ajibu baada ya kushindwa kukubaliana kwenye maslahi binafsi. Kwa mujibu wa mawasiliano yaliyovuja baina ya Andre Mtine wa TP Mazembe na Makamu Mwenyekiti wa Yanga SC, Frederick Mwakalebela mpango huo umekufa. Katiba barua yake kwa Mwakalebela ambayo pia aliwatumia nakala Mkurugenzi wa Azam TV, Patrick Kahemele, Mtine amesema wameamua kusitisha mpango huo baada ya kutofikia makubaliano na Ajibu juu ya maslahi binafsi. Lakini habari zaidi zinasema kwamba Ajibu ameamua kurejea klabu yake ya zamani, Simba SC kufuatia kumaliza mkataba Yanga SC mwezi huu. Wiki iliyopita, Katibu wa TP Mazembe, Dony Kabongo alimuandikia barua Katibu wa Yanga kumtaarifu juu ya klabu yake kusaini mkataba wa awali na Ajibu na kuomba barua ya mchezaji huyo kuruhusiwa kuondoka Jangwani mkataba wake utakapomalizika

AUSSEMS ASAINI MKATABA MPYA KUENDELEA KUFUNDISHA SIMBA SC HADI JULAI 2020

Image
Na Mahmoud Zubeiry, DAR ES SALAAM KOCHA Mbelgiji, Patrick Winand J. Aussems amesaini mkataba mpya wa mwaka mmoja kuendelea kufundisha klabu ya Simba SC ya Dar es Salaam. Aussems amesaini mkataba huo mpya leo mbele ya Mwenyekiti wa Bodi ya Simba, mfanyabiashara bilionea Mohammed ‘Mo’ Dewji na Mwenyekiti wa klabu hiyo, Swedi Nkwabi. Na Simba SC imeamua kumpa mkataba mpya Aussems baada ya msimu wake mzuri wa kwanza akiiwezesha klabu kutetea ubingwa kufikia hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika ambako ilikwenda kutolewa katika Robo Fainali na TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC). Kocha Mbelgiji, Patrick Aussems (kushoto) akisaini mkataba nyumbani kwa Mohammed 'Mo' Dewji leo mjini Dar es Salaam. Kulia ni Mwenyekiti wa klabu, Swedi Nkwabi. Patrick Aussems (kushoto) wakati wa kusaini mkataba leo nyumbani kwa Mohammed 'Mo' Dewji (kulia). Katikati ni Mwenyekiti wa klabu, Swedi Nkwabi. Hadi Julai 2020; Sasa Patrick Aussems (kushoto) ataendelea kufu