Posts

Showing posts from January, 2020

MTANGO AMTWANGA MTHAILAND TKO RAUNDI YA SABA MKWAKWANI

Image
Refa Anthony Rutta akimuinua mkono bondia Salim Jengo Mtango baada ya kumshinda Suriya Tatakhun wa Thailand kwa Technical Knockout (TKO) raundi ya saba usiku wa leo Uwanja wa Mkwakwani Jijini na kutwaa taji la UBO uzito wa Light 

ARSENAL YAMSAJILI KWA MKOPO WA MIEZI SITA BEKI MRENO, CEDRIC SOARES

Image
Arsenal imekamilisha usajili wa beki Mreno, Cedric Soares kwa mkopo wa miezi sita kutoka Southampton, zote za England   PICHA ZAIDI GONGA HAPA

MIGUU YA MABEKI WA SIMBA SC INAVYOWAHUKUMU MAKIPA WAO

Image
Na Mustafa Mtupa, DAR ES SALAAM ILIKUWA ni mchana ambao uliambatana na hali ya jua kali lililo mchoma yeyote aliyetembea barabarani kwa miguu. Nikiwa miongoni mwa watembea kwa miguu hao na kukubali ngozi yangu kushambuliwa na jua kisawa sawa hata vitobo vidogo vilivyo patikana kwenye ngozi yangu vikaruhusu maji yaliyo changanyika na chumvi kutoka kwenye ngozi yangu na kunipa kibaria cha kujifuta kila mara. Safari yangu ilikuwa ni kuelekea kwenye moja ya jengo maarufu linalo milikiwa na klabu kongwe hapa nchini na barani Afrika kiujumla kati kati kabisa ya jiji la dar es salaam maeneo ya Karikakoo ambapo ndipo linapopatikana jengo hilo la Klabu ya simba. Kwa hakika nilifika japo hali ya miguu yangu ilikuwa haitamaniki kwa kukoga vumbi la kutosha. lakini wala haikuni shughulisha nilisogea karibu kabisa na sehemu niliyoona kuwa kuna watu wameketi na kupiga soga mbali mbali ambazo moja kwa moja niligundua zilikuwa ni soga zinazohusu hali ya kiwango ya timu yao ya Simba. Baada ya kufi

MESSI APIGA MBILI BARCELONA YAICHAPA LEGANES 5-0 KOMBE LA MFALME

Image
Mshambuliaji Leonel Messi akipongezwa na Arturo Vidal baada ya kuifungia Barcelona mabao mawili dakika za 59 na 89 katika ushindi wa 5-0 dhidi ya Leganes kwenye mchezo wa Hatua ya 16 Bora Kombe la Mfalme Hispania usiku wa Alhamisi Uwanja wa Camp Nou. Mabao mengine ya Barca inayotinga Robo Fainali sasa, yamefungwa na Antoine Griezmann dakika ya nne, Clement Lenglet dakika ya 27 na Arthur Melo dakika ya 77   PICHA ZAIDI GONGA HAPA

BRUNO FERNANDES ASAINI MKATABA WA MIAKA MITANO NA NUSU KUJIUNGA NA MAN UNITED

Image
Kiungo Mreno, Bruno Fernandes (kulia) akisaini mkataba wa miaka mitano na nusu kujiunga na Manchester United kutoka Sporting Lisbon ya kwao, Ureno  kwa dau la Pauni Milioni 46.6, ambalo linaweza kupanda hadi Pauni Milioni 68. Kushoto ni kocha wa Manchester United, Ole Gunnar Solskjaer ambaye ana matumaini mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25 ataisaidia timu yake   PICHA ZAIDI GONGA HAPA

AZAM FC YALAZIMISHWA SARE YA 1-1 NA MTIBWA SUGAR TAIFA TIMU ZOTE ZIKIMALIZA PUNGUFU

Image
Kiungo wa Mtibwa Sugar, Salum Kihimbwa akiupitia mpira mguuni mwa beki Mganda wa Azam FC, Nicholas Wadada katika mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara Alhamisi Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Timu hizo zilitoka sare ya 1-1, Mtibwa Sugar wakitangulia kwa bao la Ismail Mhesa dakika ya 67, kabla ya Muivory Coast, Richard Ella D'jodi kuisawazishia Azam FC kwa penalti dakika ya 77.  Timu zote zilimaliza pungufu baada ya wachezaji wake kuonyeshwa kadi za pili za njano na kutolewa kwa kadi nyekundu, wakianza Mtibwa Sugar waliompoteza beki wao, Dickson Job dakika ya 72 kabla ya mshmabuliaji wa Azam, Shaaban Chilunda kutolewa dakika ya mwisho kabisa, 90 na ushei.  

REAL MADRID YAICHAPA ZARAGOZA 4-0 KOMBE LA MFALME HISPANIA

Image
Nyota wa Real Madrid, Mbrazil Vinicius Junior akiwatoka mabeki wa Real Zaragoza katika mchezo wa hatua ya 16 Bora Kombe la Mfalme Hispania usiku wa jana Uwanja wa De la Romareda. Mabao ya Real Madrid yalifungwa na Raphael Varane dakika ya sita, Lucas Vazquez dakika ya 32, Vinicius Junior dakika ya 72 na Karim Benzema dakika ya 79 na kwa ushindi huo kikosi cha Mfaransa, Zinedine Zidane kinatinga Robo Fainali   PICHA ZAIDI GONGA HAPA

LIVERPOOL YAICHAPA WEST HAM UNITED 2-0 NA KUZIDI KUUKARIBIA UBINGWA

Image
Roberto Firmino, Jordan Henderson, Mohamed Salah, na Georginio Wijnaldum wakishangilia baada ya Liverpool kupata bao la kwanza jana katika ushindi wa 2-0 dhidi ya West Ham United kwenye mchezo wa Ligi Kuu ya England jana Uwanja wa London. Mabao ya Liverpool yalifungwa na Mohamed Salah dakika ya 35 kwa penalti na Alex Oxlade-Chamberlain dakika ya 52 na kwa ushindi huo, Wekundu hao wa Anfield sasa wanaongoza Ligi Kuu kwa pointi 19 zaidi ya Manchester City wanaofuatia baada ya wote kucheza mechi 24   PICHA ZAIDI GONGA HAPA  

MAN UNITED PUNGUFU YAICHAPA MAN CITY 1-0, LAKINI YATOLEWA

Image
Refa Kevin Friend akimuonyesha Nemanja Matic wa Manchester United kadi nyekundu dakika ya 76 baada ya kumuonyesha kadi ya njano ya pili kwa kumchezea rafu Ilkay Gundogan wa Manchester City kwenye mchezo wa marudiano wa Nusu Fainali Kombe la Ligi England jana Uwanja wa Etihad. Manchester United ilishinda 1-0, bao pekee la Matic dakika ya 35, lakini ni Manchester City inayokwenda fainali kwa ushindi wa jumla wa 3-2 baada ya kushinda 3-1 kwenye mchezo wa kwanza Uwanja wa Old Trafford Januari 7 na itamenyana na Aston Villa Machi 1, Uwanja wa Wembley, London   PICHA ZAIDI GONGA HAPA

SIMBA SC 3-2 NAMUNGO FC (LIGI KUU YA TANZANIA BARA)

Image

KAGERE APIGA BAO LA USHINDI BADO DAKIKA MBILI SIMBA SC YAWACHAPA NAMUNGO FC 3-2 TAIFA

Image
Na Asha Said, DAR ES SALAAM MABINGWA watetezi, Simba SC wameendelea kung’ara baada ya ushindi wa mabao 3-2 dhidi ya Namungo FC kwenye mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara usiku wa leo Uwanja wa Taifa Jijini Darves Salaam. Kwa ushindi huo, Simba SC inayofundishwa na kocha Mbelgiji, Sven Ludwig Vandonbroeck inafikisha pointi 44 katika mchezo wa 17 na kuendelea kuongoza Ligi Kuu kwa pointi tisa zaidi ya Azam FC inayofuatia katika nafasi ya pili, ingawa imecheza mechi 16, wakati Namungo inabaki na pointi zake 28 za mechi 16. Katika mchezo huo uliochezeshwa na refa Florentina Zabron wa Dodoma, aliyesaidiwa na Mohamed Mkono wa Tanga na Kassim Safisha wa Pwani, hadi mapumziko Simba SC walikuwa wanaongoza kwa mabao 2-1. Shujaa; Meddie Kagere akishangilia baada ya kuifungia Simba SC bao la ushindi dakika ya 88 ikiilaza Namungo FC 3-2 Kiungo wa kimataifa wa Kenya, Francis Kahata Nyambura aliifungia Simba SC bao la kwanza dakika ya 21 akiirukia kwa kichwa cha mkizi krosi maridadi ya beki wa

BONDIA WA THAILAND AWASILI LEO DAR KUZIPIGA NA SALIM MTANGO IJUMAA UWANJA WA MKWAKWANI

Image
Bondia Suriya Tatakhun akiwa na kocha wake baada ya kuwasili leo Jijini Dar es Salaam kutoka kwao, Thailand tayari kwa pambano kubwa la ngumi la kimataifa dhidi ya mwenyeji, Salim Jengo Mtango usiku wa Ijumaa Uwanja wa Mkwakwani Jijini Tanga kuwania taji lilio wazi la UBO uzito wa Light 

MATHEO AIPIGIA BAO PEKEE POLISI YAICHAPA TANZANIA PRISONS 1-0 LEO USHIRIKA

Image
Bao pekee la mshambuliaji Matheo Anthony Simon dakika ya 82 limetosha kuipa ushindi wa 1-0 Polisi Tanzania dhidi ya Tanzania Prisons katika mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa Ushirika mjini Moshi mkoani Kilimanjaro.

MTENDAJI MKUU WA AZAM FC AFANYA ZIARA KLABU KADHAA NCHINI MISRI, AKUTANA HADI NA HIMID MAO

Image
OFISA Mtendaji Mkuu wa Azam FC, Abdulkarim Amin 'Popat', akiwa makao makuu ya miamba ya soka barani Afrika, Al Ahly. Popat amefanya ziara hiyo leo, kwa lengo kuu la kujifunza mambo mbalimbali ya soka, pamoja na kujionea uwekezaji uliofanywa na klabu hiyo ya karne barani Afrika. Aidha kwenye ziara hiyo alikuwa sambamba na mwenyeji wake, Amgad Alghoniny, ambaye ni Mhariri wa kitengo cha habari cha timu hiyo. Mbali ya kutembelea kwa miamba hiyo, Popat pia alipata fursa ya kukutana na Nahodha wa zamani wa Azam FC, Himid Mao 'Ninja', anayekipiga nchini humo katika timu ya ENPPI.  Hapa akiwa na kiungo wa zamani wa Azam FC, Mtanzania Himid Mao ambaye kwa sasa anachezea ENPPI  Hapa akiwa na Himid Mao na mshambuliaji wa kimataifa wa Burundi, Fiston Abdul Razak anayecheza naye ENPPI 

KASEJA NA PAWASA WAJITOKEZA MAFUNZO YA DIPLOMA C YA KOZI YA UKOCHA YA CAF

Image
Nyota wa zamani wa klabu ya Simba, kipa Juma Kaseja (kushoto) na beki Boniface Pawasa (kulia) ni miongoni mwa makocha 30 waliojitokeza kushiriki Kozi ya siku 28 ya Diploma C ya Shirikisho la Soka Afrika (CAF) inayoendelea makao makuu ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Karume, Ilala,  Dar es Salaam  

UZINDUZI WA TAWI LA SIMBA SC BUNGENI MJINI DODOMA ULIVYOFANA MAPEMA LEO

Image
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Job Yustino Ndugai akikata utepe wakati wa uzinduzi wa tawi la klabu hiyo Bungeni mjini Dodoma mapema leo uliokwenda sambamba na uzinduzi wa Kadi za Mashabiki Kanda ya Kati, ambazo zinatolewa kwenye matawi yote ya benki ya Equity nchini Job Ndugai ambaye pia ni mbunge wa jimbo la Kongwa kwa tiketi ya chama tawala, CCM alishiriki mazoezi yote mawili    Job Ndugai ni shabiki mzuri wa klabu ya Simba  

MCHEZAJI KUPELEKWA KWA MKOPO NI UAMUZI WA BENCHI LA UFUNDI

Image
Na Dominick Salamba, DAR ES SALAAM DIRISHA dogo la usajili msimu huu limetuletea taswira ya kushangaza sana kwa wachezaji wetu na waajiri wao. Kuna kitu kinaitwa usajili wa mkopo,hii inamaanisha kuwa,klabu X inaweza kumtumia mchezaji ambae anamilikiwa na klabu nyingine na wao kumtumia kwa makubaliano maalum kutoka timu x,mchezaji husika na timu inayohitaji huduma ya mchezaji husika. Kwa nini usajili wa mkopo? kabla ya kulijua hilo kila mmoja anapaswa kujua kuwa kila timu inasajili wachezaji kwa ajili ya kuwatumia katika mashindano tofauti ndani ya msimu,kisha tufahamu kuwa uamuzi wa kumpeleka mchezaji kwa mkopo mahali fulani ni uamuzi wa benchi la ufundi,baada ya kutathmini nafasi ya mchezaji huyo kwenye timu, hapo ndipo utagundua kuwa mchezaji anaweza kupelekwa kwa mkopo ili kulinda kipaji chake,na ni kwa faida ya timu husika endapo mchezaji ataimarika kwa siku zijazo.. 👉🏽👉🏽Katika nchi za wenzetu zilizopiga hatua kisoka mara nyingi wachezaji wanaopelekwa kwa mkopo ni wale vij

SAMATTA ‘AWAKOSAKOSA’ LEICESTER CITY, ASTON VILLA YASHINDA 2-1 NA KUTINGA FAINALI KOMBE LA LIGI ENGLAND

Image
Na Mwandishi Wetu, BIRMINGHAM  MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Tanzania, Mbwana Ally Samatta jana amecheza kwa dakika 67 tu, timu yake mpya, Aston Villa ikishinda 2-1 dhidi ya Leicester City Uwanja wa Villa Park, Jijini Birmingham na kuingia fainali ya Kombe la Ligi England. Samatta alikuwa anacheza mechi yake ya kwanza kabisa baada ya kukamilisha uhamisho wa Pauni Milioni 8.5 kutoka KRC Genk ya Ubelgiji, klabu yake ya kwanza Ulaya aliyojiunga nayo mwaka 2016 akitokea TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC). Pamoja na ugeni wake, Samatta, mchezaji wa zamani wa Mbagala Market, ambayo sasa inajulikana kama African Lyon na Simba, zote za Dar es Salaam, alicheza kwa kiwango kizuri na kukaribia kufunga kabla ya kocha Dean Smith kumpumzisha dakika ya 67, akimuingiza mshambuliaji kinda wa England, Keinan Davis. Mbwana Samatta akisikitika baada ya kukosa bao la wazi jana Uwanja wa Villa Park, Birmingham   PICHA ZAIDI GONGA HAPA Katika mchezo huo, mabao ya Villa yalifungwa na Ma

DK. MSOLLA AITISHA MKUTANO WA DHARURA WA WANACHAMA YANGA FEBRUARI 16 JKNICC

Image
Na Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM KLABU ya Yanga inatarajiwa kufanya mkutano wa dharula Februari 16, mwaka huu katika ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Kambarage Nyerere (JKNICC), Dar es Salaam kuanzia Saa 4:00 asubuhi. Taarifa ya Mwenyekiti wa Yanga SC, Dk. Mshindo Mbette Msolla kwa vyombo vya Habari leo imesema kwamba ameitisha mkutano huo kwa kuzingatia Ibara ya 22 ya Katiba ya mwaka 2010. Msolla amesema mkutano huo utakuwa na ajenda sita ambazo ni; Ufunguzi wa Mkutano, Kuthibitisha Akidi ya Mkutano, Kupitia Ajenda za Mkutano, Kuwasilisha na Kuainisha Mapendekezo ya Katiba/Mapendekezo Mapya, Kupigia Kura Mapendekezo ya Marekebisho ya Katiba na Kufunga Mkutano. Msolla, aliyewahi kuwa kocha Mkuu wa Taifa Stars, aliingia madarakani Yanga  Mei 5, mwaka jana katika uchaguzi uliofanyika leo Bwalo la Maofisa wa Jeshi la Polisi, Osyterbay mjini Dar es Salaam akishinda kwa kishindo dhidi ya Dk. Jonas Benedict Tiboroha. Msolla alipata jumla ya 1,276 dhidi ya 60 tu za

SIMBA SC YAKANA TUHUMA ZA KUTAKA KUMHONGA KIPA WA YANGA, RAMADHANI KAWBILI

Image
Na Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM KLABU ya Simba SC imesema imeyapokea kwa masikitiko makubwa maelezo ya kipa wa Yanga SC, Ramadhani Awamu Kabwili kuishutumu klabu hiyo kutaka kumhonga aihujumu klabu yake. Taarifa ya Mtendaji Mkuu wa Simba, Senzo Masingiza leo imesema kwamba kauli za aina hiyo kutoka kwa wachezaji ni za kuchukiza na siyo za heshima ambazo zinaashiria upangaji wa matokeo ya mechi kama ilivyotuhumiwa na mchezaji huyo na klabu yake inazipinga na kukemea vikali. “Kauli hizi zina madhara makubwa kwenye uadilifu wa klabu ya Simba na viongozi wake. Uadlifu na heshima Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania kwa ujumla unawekwa mashakani kama kauli za namna hii hizi hazitachukuliwa hatua stahiki,”amesema Senzo katika taarifa yake. Hata hivyo, Ofisa huyo Raia wa Afrika Kusini amesema kwamba wamefurahishwa mno na hatua iliyochukuliwa na TFF baada ya kauli za mlinda mlango huyo chipukizi wa kimataifa wa Tanzania. Jana TFF iliiagiza Kamati yake ya Maadili kufuatilia ukweli kuhus

THOMAS ULIMWENGU ASAINI MKATABA WA MIAKA MIWILI KUREJEA KLABU YA TP MAZEMBE

Image
Na Mwandshi Wetu, LUBUMBASHI MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Tanzania, Thomas Emmanuel Ulimwengu amesaini mkataba wa miaka miwili kujiunga tena na klabu yake, TP Mazembe. Ulimwengu mwenye umri wa miaka 27, amerejea Kamalondo ambako aliondoka mwaka 2016 kwenda Ulaya, ambako hata hivyo hakufanikiwa.  Kati ya mwaka 2017 na 2018 alichezea na klabu za AFC Eskilstuna ya Sweden na FK Sloboda Tuzla ya Bosnia kabla ya kurejea Afrika na kuchezea klabu za Al Hilal ya Sudan na JS Saoura ya Algeria. Na sasa amejiunga tena na Mazembe kama mchezaji huru na anatarajiwa kuwasil Lubumbashi Jumatano kuanza tena maisha mapya katika mji aliouzoea. Ulimwengu anafanya idadi ya Watanzania katika klabu hiyo kufika watatu, baada ya kiungo Ramadhani Singano ‘Messi’ na mshambulaji Eliud Ambokile. Ulimwengu aliyezaliwa Juni 14, mwaka 1993 aliibukia katika taasisi ya soka Tanzania (TSA) mwaka 2008, kabla ya mwaka 2009 kwenda kuanza kukomazwa Ligi Kuu katika klabu ya Moro United. Alicheza Moro United kwa mkopo

MO DEWJI ALIPOMKABIDHI JEZI YA SIMBA SC RAIS WA FIFA, GIANNI INFANTINO

Image
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Simba, Mohamed 'Mo' Dewji (kulia) akimkabidhi jezi ya klabu hiyo, Rais wa Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA), Gianni Infantino makao makuu ya bodi hiyo ya kandanda Jijini Zurich, Uswisi