Popular posts from this blog
NYOTA WA KIKOSI CHA SIMBA KILICHOFIKA FAINALI KOMBE LA CAF 1993, DAMIAN KIMTI AFARIKI DUNIA
Na Stella Theopist, DAR ES SALAAM UONGOZI wa Klabu ya Simba umepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za kifo cha mchezaji wake wa zamani, Damian Mrisho Kimti aliyefariki dunia jana jioni Jijini Dar es Salaam. Kimti alikuwa mmoja wa wachezaji ambao walicheza mchezo wa fainali ya ubingwa wa Afrika Mashariki mwaka 1992 ambao tuliibuka na ushindi dhidi ya Yanga na pia alikuwa sehemu ya kikosi kilichocheza fainali ya Kombe la CAF mwaka 1993 dhidi ya Stella Abidjan. Klabu itamkumbuka Kimti kwa mchango wake mkubwa alioutoa kwetu kwa kipindi chote ambacho alikuwa akichezea timu yetu. Damian Kimti (kulia) akivalishwa Medali na aliyekuwa Waziri wa Michezo, Profesa Philemon Sarungi baada ya fainali ya Kombe la CAF mwaka 1993 Klabu ya Simba inaungana na familia pamoja na wadau wa mpira wa miguu katika msiba huu. Tunatoa pole kwa familia, ndugu, jamaa, marafiki na watu wote walioguswa na msiba huu. Mwenyezi Mungu ailaze roho ya marehemu mahala pema peponi.
NI YANGA BINGWA KOMBE LA MUUNGANO 2025
TIMU ya Yanga imefanikiwa kutwaa Kombe la Muungano, michuano maalum ya kuazimisha sherehe za miaka 61 ya Muungano ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar baada ya ushindi wa bao 1-0 dhidi ya JKU usiku huu Uwanja wa Gombani, Pemba. Shujaa wa Yanga leo ni kiungo kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Maxi Mpia Nzengeli aliyefunga bao hilo pekee dakika ya 45 na mabingwa hao wa Tanzania Bara wamezawadiwa Sh. Milioni. Pamoja na kufunga bao la ushindi, Nzengeli pia ameshinda Tuzo za Mfungaji Bora kwa mabao yake mawili jumla na Nyota wa Mchezo wa leo, wakati kiungo mwenzake wa Yanga, Mudathir Yahya Abbas ameshinda Tuzo ya Mchezaji Bora wa Mashindano. JKU, mabingwa wa Zanzibar kwa kumaliza nafasi ya pili wamezawadiwa Sh. Milioni 30. Jumla ya timu nane zimeshiriki michuano ya mwaka huu iliyoanzia hatua ya Robo Fainali, nyingine ni KMKM, Zimamoto na KVZ, zote za Zanzibar na Azam FC, Coastal Union na Singida Black Stars za Tanzania Bara. Mabingwa wa msimu uliopita, Simba hawakushiriki mic...

Mbona muonekano was gazeti siuoni au nakosea kufungua?
ReplyDeleteMbona muonekano was gazeti siuoni au nakosea kufungua?
ReplyDelete