MESSI AFUNGA BAO LA KWANZA UFARANSA


MSHAMBULIAJI Lionel Messi jana amefunga bao lake la kwanza Ligue 1, Ufaransa akiiwezesha Paris Saint-Germain kuichapa 3-1 Nantes Uwanja wa Parc des Princes Jijini Paris.
Messi alifunga bao la tatu dakika ya 87 akimalizia pasi ya Kylian Mbappe aliyefunga pia bao la kwanza dakika ya pili tu, wakati bao la pili Dennis Appiah alijifunga dakika ya 81.
Bao pekee la Nantes lilifungwa na Randal Kolo Muani dakika ya 76 katika mchezo huo ambao PSG ilimaliza pungufu baada ya Keylor Navas kutolewa kwa kadi nyekundu dakika ya 65.


Comments

Popular posts from this blog

NYOTA WA KIKOSI CHA SIMBA KILICHOFIKA FAINALI KOMBE LA CAF 1993, DAMIAN KIMTI AFARIKI DUNIA

NYOTA WA SIMBA SC ILIYOFIKA NUSU FAINALI KLABU BINGWA AFRIKA, ABBAS DILUBGA AFARIKI DUNIA