ZAYD NA DUBE KUKOSEKANA WIKI TATU AZAM FC


BAADA ya kufanyiwa vipimo vya kina, ni rasmi sasa nyota wawili wa Azam FC, kiungo mzawa Yahya Zayd na mshambuliaji Mzimbabwe, Prince Dube watakuwa nje ya dimba kwa muda wa wiki tatu kila mmoja.
Wachezaji hao walilazimika kufanyiwa mabadiliko ya haraka kipindi cha kwanza, Azam FC ikiichapa Singida Fountain Gate mabao 2-1, kwenye mchezo uliopita wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara.
Dube anasumbuliwa na majeraha ya nyonga, huku Zayd akiwa amechanika kiraba (meniscus) kinachokuwa katikati ya goti, kinacholiimarisha lisikwaruzane.
Kiraba hicho pia huwezesha goti kufanya kazi vizuri kwa maana ya kukunja na kukunjua.
Wachezaji hao wanaendelea na programu ya kutibu majeraha yao chini ya uangalizi wa Mtaalamu wa tiba za viungo (physiotherapist) wa timu yetu, Joao Rodrigues.


Comments

Popular posts from this blog

NYOTA WA KIKOSI CHA SIMBA KILICHOFIKA FAINALI KOMBE LA CAF 1993, DAMIAN KIMTI AFARIKI DUNIA