SERENGETI GIRLS YAWACHAPA MISRI 4-1 LEO TUNISIA



TIMU ya taifa ya wasichana chini ya umri wa miaka 17, Serengeti Girls leo imeibuka na ushindi wa mabao 4-1 dhidi ya Mısri katika michuano ya Nchi za Kaskazini mwa Afrika (UNAF) Uwanja wa Manispaa wa Kram mjini Kram nchini Tunisia.
Mabao ya Serengeti Girls ambao ni waalikwa kwenye michuano hiyo yamefungwa na Mwatima Mwarabu mawili, Yasinta Joseph Mitoga na Jamila Rajab Mnunduka moja kila mmoja.
Katika michuano hiyo inayofikia tamati Septemba 9, Serengeti Girls watarudi uwanjani keshokutwa kumenyana na Morocco, kabla ya kukamilisha kazi kwa kucgeza na wenyeji, Tunisia Jumamosi mechi zote zikipigwa Uwanja wa Ariana kuanzia Saa 10:30 jioni kadhalika.


Comments

Popular posts from this blog

NYOTA WA KIKOSI CHA SIMBA KILICHOFIKA FAINALI KOMBE LA CAF 1993, DAMIAN KIMTI AFARIKI DUNIA