YANGA PRINCESS YAITOA SIMBA QUEENS KWA MATUTA NGAO YA JAMII

TIMU ya Yanga Princess imefanikiwa kuingia Fainali ya michuano ya Ngao ya Jamii kuelekea msimu mpya wa Ligi Kuu ya Wanawake Tanzania Bara baada ya ushindi wa penalti 4-3 kufuatia sare ya kufungana bao 1-1 na watani, Simba Queens Uwanja wa jioni ya leo Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni, KMC Complex, Mwenge Jijini Dar es Salaam.
Yanga Princess walitangulia kwa bao la dakika ya kwanza tu la mshambuliaji wake chipukizi mzawa, Agness Palangyo, kabla ya mshambuliaji wa Kimataifa wa Kenya, Jentrix Shikangwa Milimu kuisawazishia Simba Queens dakika ya 88.
Sasa Yanga Princess watakutana na JKT Queens Jumamanosi katika Fainali hapo hapo Uwanja wa KMC, huku Simba Queens wakicheza na CEASIAA Queens kuwania nafasi ya tatu.
Kwa upande wao JKT Queens walitangulia Fainali baada ya kuichapa CEASIAA Queens 7-0, Stumai Abdallah Athumani aking’ara Zaidi kwa kufunga hat trick.
UP SOUND: MABAO YA JKT



Comments

Popular posts from this blog

NYOTA WA KIKOSI CHA SIMBA KILICHOFIKA FAINALI KOMBE LA CAF 1993, DAMIAN KIMTI AFARIKI DUNIA