YANGA PRINCESS YAITOA SIMBA QUEENS KWA MATUTA NGAO YA JAMII
TIMU ya Yanga Princess imefanikiwa kuingia Fainali ya michuano ya Ngao ya Jamii kuelekea msimu mpya wa Ligi Kuu ya Wanawake Tanzania Bara baada ya ushindi wa penalti 4-3 kufuatia sare ya kufungana bao 1-1 na watani, Simba Queens Uwanja wa jioni ya leo Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni, KMC Complex, Mwenge Jijini Dar es Salaam.
Yanga Princess walitangulia kwa bao la dakika ya kwanza tu la mshambuliaji wake chipukizi mzawa, Agness Palangyo, kabla ya mshambuliaji wa Kimataifa wa Kenya, Jentrix Shikangwa Milimu kuisawazishia Simba Queens dakika ya 88.
Yanga Princess walitangulia kwa bao la dakika ya kwanza tu la mshambuliaji wake chipukizi mzawa, Agness Palangyo, kabla ya mshambuliaji wa Kimataifa wa Kenya, Jentrix Shikangwa Milimu kuisawazishia Simba Queens dakika ya 88.
Comments
Post a Comment