YANGA SC YAREJEA KILELENI BAADA YA KUICHAPA KAGERA SUGAR 4-0
MABINGWA watetezi, Yanga SC wamerejea kileleni mwa Ligi Kuu ya NBC ya Tanzania Bara baada ya ushindi wa mabao 4-0 dhidi ya Kagera Sugar jioni ya leo Uwanja wa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni, KMC Complex, Mwenge Jijini Dar es Salaam.
Mabao ya Yanga leo yamefungwa na nyota wazawa, mshambuliaji Clement Francis Mzize dakika ya 32, kiungo Mudathir Yahya Abbas dakika ya 60, kiungo Muivory Coast, Pacome Zouzoua Peodoh kwa penalti dakika ya 78 na mshambuliaji Mzambia, Kennedy Musonda dakika ya 86.
Yanga ingeweza kuondoka na ushindi wa mabao 5-0 leo kama kiungo Mburkinabe, Stephane Aziz Ki.
Kwa ushindi huo, Yanga inafikisha pointi 42 katika mchezo wa 16 na kupanda juu ya msimamo, ikiizidi pointi mbili Simba ambayo pia ina mechi moja mkononi na kesho inacheza na Tabora United mjini Tabora.
Kwa upande wao Kagera Sugar baada ya kipigo cha leo 11 za mechi 16 nafasi ya 15 kwenye ligi ya timu 16 — mbele ya Ken Gold yenye pointi sita za mechi 16 pia.
Comments
Post a Comment