KMC YAILAZA DODOMA JIJI 2-1 MWENGE


WENYEJI, KMC wameibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Dodoma Jiji katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara leo Uwanja wa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni, KMC Complex, Mwenge, Dar es Salaam.
Mabao ya KMC yamefungwa na Abdallah Said dakika ya sita na Rashid Chambo dakika ya 28 — na la Dodoma Jiji limefungwa na Iddi Kipagwile dakika ya 39.
Kwa ushindi huo, KMC inafikisha pointi 30 katika mchezo wa 26 na kusogea nafasi ya tisa, wakati Dodoma Jiji inabaki na pointi zake 34 za mechi 27 nafasi y sita.


Comments

Popular posts from this blog

NYOTA WA KIKOSI CHA SIMBA KILICHOFIKA FAINALI KOMBE LA CAF 1993, DAMIAN KIMTI AFARIKI DUNIA

NI YANGA BINGWA KOMBE LA MUUNGANO 2025