Posts

Showing posts from February, 2025

PAMBA JIJI FC 0-3 YANGA SC (LIGI KUU YA NBC TZ BARA)

Image
 

TABORA UNITED YAICHAPA DODOMA JIJI 1-0 ALI HASSAN MWINYI

Image
BAO la kujifunga la Dissan Galiwango dakika ya 36 limeipa Tabora United ushindi wa 1-0 dhidi ya Dodoma Jjji mchana wa leo Uwanka wa Ali Hassan Mwinyi Tabora. Kwa ushindi huo, Tabora United inafikisha pointi 37, ingawa inabaki nafasi ya nne, ikizidiwa pointi nne na Singida Black Stars baada ya wote kucheza mechi 22, wakati Dodoma Jiji inabaki na pointi zake 26 za mechi 21 nafasi ya saba.

AZAM FC YANANWA CHAMAZI, SARE 1-1 NA NAMUNGO

Image
WENYEJI, Azam FC wametoa sare ya kufungana bao 1-1 na Namungo FC katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara usiku huu Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam. Namungo FC walianza kupata bao lililofungwa na Khamis Khalifa dakika ya 12, kabla ya Mgambia, Gibrill Sillah kuisawazishia Azam FC dakika ya 43. Azam FC wangeweza kuondoka na ushindi kama si nyota wake, Feisal Salum kukosa penalti iliyopanguliwa na kipa, adhabu ambayo ilitolewa baada ya winga Iddy Suleiman ‘Nado’ kuangushwa kwenye boksi. Kwa matokeo hayo, Azam FC inafikisha pointi 45 katika mchezo wa 22, ingawa inabaki nafasi ya tatu — na Namungo nayo inatimiza pointi 23 katika mchezo wa 22 pia na kupanda kwa nafasi moja hadi ya 12 kwenye ligi ya timu 16. Ikumbukwe mwisho wa msimu timu mbili zitashuka Daraja na mbili nyingine zitakazomaliza nafasi y 14 na 13 zitamenyana baina yao na mshindi wa jumla atasalia Ligi Kuu, wakati timu itakayofungwa itakwenda kumenyana na timu ya Championship kujaribu tena kubaki Ligi ...

JKT TANZANIA YATOA SARE NA KENGOLD, 1-1 MBWENI

Image
WENYEJI, JKT Tanzania wamelazimishwa sare ya kufungana bao 1-1 na Kengold katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara leo Uwanja wa Meja Jenerali  Charles Isamuhyo, Mbweni Jijini Dar es Salaam. JKT Tanzania walianza kupata bao, mfungaji Edward Songo kwa penalti dakika ya 45’+6, kabla ya mshambuliaji Suleiman Salim Rashid 'Bwenzi' kuisawazishia Kengold dakika ya 85. Kwa matokeo hayo, JKT Tanzania inafikisha pointi 27, ingawa inabaki nafasi ya sita — na Kengold inafikisha pointi 15, nayo inabaki mkiani kwenye ligi ya timu 16 baada ya wote kucheza mechi 22. Ikumbukwe mwisho wa msimu timu mbili zitashuka Daraja na mbili nyingine zitakazomaliza nafasi y 14 na 13 zitamenyana baina yao na mshindi wa jumla atasalia Ligi Kuu, wakati timu itakayofungwa itakwenda kumenyana na timu ya Championship kujaribu tena kubaki Ligi Kuu.

KAGERA SUGAR YAAMBULIA SULUHU KWA KMC KAITABA

Image
TIMU ya Kagera Sugar imeambulia sare ya mabao mbele ya wageni wao, KMC katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara usiku huu Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba. Kwa matokeo hayo, Kagera Sugar inafikisha pointi 16 na inabaki nafasi ya 15 kwenye ligi ya timu 16, wakati KMC inafikisha pointi 24 na kupanda kwa nafasi moja hadi ya 10 baada ya wote kucheza mechi 22. Ikumbukwe mwisho wa msimu timu mbili zitashuka Daraja na mbili nyingine zitakazomaliza nafasi y 14 na 13 zitamenyana baina yao na mshindi wa jumla atasalia Ligi Kuu, wakati timu itakayofungwa itakwenda kumenyana na timu ya Championship kujaribu tena kubaki Ligi Kuu.

FOUNTAIN GATE YAICHAPA TANZANIA PRISONS 1-0 BABATI

Image
BAO la mkwaju wa penalti la Amos Charles dakika ya 27 limeipa Fountain Gate ushindi wa 1-0 dhidi ya Tanzania Prisons katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara leo Uwanja wa Tanzanite Kwaraa mjini Babati mkoani Manyara. Kwa ushindi huo, Fountain Gate wanafikisha pointi 25 na kupanda hadi nafasi ya nane, wakati Tanzania Prisons wanabaki na pointi zao 18 nafasi ya 14 kwenye Ligi ya timu 16 baada ya wote kucheza mechi 22. Ikumbukwe mwisho wa msimu timu mbili zitashuka Daraja na mbili nyingine zitakazomaliza nafasi y 14 na 13 zitamenyana baina yao na mshindi wa jumla atasalia Ligi Kuu, wakati timu itakayofungwa itakwenda kumenyana na timu ya Championship kujaribu tena kubaki Ligi Kuu.

SIMBA SC 2-2 AZAM FC (LIGI KUU YA NBC TZ BARA)

Image
 

ZIDANE SERERI AZIMA SHANGWE ZA SIMBA DAKIKA ZA JIONI

Image
TIMU za Simba SC na Azam FC zimegawana pointi moja moja baada ya sare ya kufungana mabao 2-2 katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara usiku huu Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam. Azam FC walitangulia na bao la dakika ya pili tu la winga Mgambia, Gibrill Sillah akimalizia mpira uliotemwa na kipa Mguinea, Mousa Camara kufuatia krosi nzuri ya Iddi Suleiman ‘Nado’ kutoka kushoto mwa Uwanja. Simba wakasawazisha dakika ya 25 kwa bao la winga Mkongo, Elly Mpanzu Kibisawala aloyepokea pasi nzuri ya kiungo mshambuliaji Mtanzania, mwenye asili ya Kongo, Kibu Dennis Prosper. Kipindi cha pili ikawa zamu ya Simba kutangulia kwa bao la beki Abdurazam Mohamed Hamza dakika ya 76 akimalizia kwa kichwa mpira wa adhabu wa kiungo Muivory Coast, Jean Charles Ahoua kutoka kulia mwa Uwanja. Aliyeinusuru Azam kupoteza mchezo wa leo ni winga mzawa chipukizi wa miaka 19, Zidane Sereri kwa kusawazisha bao dakika ya 88 baada ya kupokea pasi ndefu ya kiungo Feisal Salum na kuwatoka mabeki ...

MASHUJAA FC 0-5 YANGA SC (LIGI KUU YA NBC TZ BARA)

Image
 

NAMUNGO FC YABANWA NA COASTAL UNION, ZATOKA SULUHU RUANGWA

Image
WENYEJI, Namungo wamelazimishwa sare ya bila kufungana na Costal Union katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara usiku huu Uwanja wa Majaliwa, Ruangwa mkoani Lindi. Kwa matokeo hayo, Namungo wanafikisha pointi 22 na kupanda kwa nafasi moja hadi ya 12, wakati Coastal Union inafikisha pointi 24, ingawa inabaki nafasi ya nane baada ya wote kucheza mechi 21.

SINGIDA BLACK STARS YAAMBULIA SARE KWA PAMBA, 2-2 LITI

Image
WENYEJI, Singida Black Stars wamelazimishwa sare ya kufungana mabao 2-2 na Pamba Jiji FC katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara mchana wa leo Uwanja wa CCM LITI mjini Singida. Mabao ya Singida Black Stars yamefungwa na washambuliaji, Muivory Coast, N'guessan Serge Archange Pokou dakika ya 10 na Mghana, Jonathan Sowah kwa penalti dakika ya 32, wakati ya Pamba yote yamefungwa na mshambuliaji Mkenya, Mathew Tegisi Momanyi dakika ya 28 na 47. Kwa matokeo hayo, Singida Black Stars inafikisha pointi 38 na inabaki nafasi ya nne, wakati Pamba inafikisha pointi 22 na kupanda kwa nafasi moja hadi ya 11 baada ya wote kucheza mechi 21.

KIPAGWILE AING’ARISHA DODOMA JIJI, YAICHAPA FOUNTAIN GATE 1-0

Image
BAO pekee la winga Iddi Kipagwile dakika ya 38 limeipa Dodoma Jiji FC ushindi wa 1-0 dhidi ya Fountain Gate katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara usiku huu Uwanja wa Jamhuri, Dodoma. Kwa ushindi huo, Dodoma Jiji FC inafikisha pointi 26 katika mchezo wa 20 na kupanda kwa nafasi mbili hadi ya saba, wakati Fountain Gate inabaki na pointi zake 22 za mechi 21 nafasi ya 11.

MECHI YA SIMBA NA AZAM SASA KUCHEZWA MKAPA SAA 1:00 USIKU

Image
MCHEZO wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara baina ya Simba SC na Azam FC umehamishwa kutoka Uwanja wa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni, KMC Complex, Mwenge hadi Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam kesho. Aidha, taarifa ya Bodi ya Ligi Kuu Tanzania Bara (TPLB) pia imesema badala ya Saa 10:00 jioni, sasa mechi hiyo ya mahasimu wa Jiji itaanza Saa 1:00 usiku, sababu ya kubadili Uwanja ikiwa ni udogo wa KMC Complex ukilinganisha na ukubwa wa mechi yenyewe. 

KENGOLD YAAMBULIA SARE KWA KMC, ZAFUNGANA 1-1 SOKOINE

Image
WENYEJI, Kengold wametoa sare ya kufungana bao 1-1 na KMC katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa Sokoine Jijini Mbeya. Beki wa kushoto, Osacl Paul Mwaigaga alianza kuifungia KMC dakika ya 41, kabla ya mshambuliaji Suleiman Salim Rashid 'Bwenzi' kuisawazishia Kengold kwa penalti dakika ya 69. Kwa matokeo hayo, Kengold wanafikisha pointi 14, ingawa wanandelea kushika mkia wakizidiwa pointi moja na Kagera Sugar iliyopo nafasi ya 15 baada ya wote kucheza mechi 21. Kwa upande wao KMC wanafikisha pointi 23 katika mechi ya 21 pia na kupanda kwa nafasi moja hadi ya 10, wakizidiwa tu wastani wa mabao na Dodoma Jiji iliyocheza mechi 19, Coastal Union na Mashujaa zote mechi 20.

JKT TANZANIA YAICHAPA KAGERA SUGAR 2-0 MBWENI

Image
WENYEJI, JKT Tanzania wameibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Kagera Sugar katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara jioninya leo Uwanja wa Meja Jenerali Michel Isamuhyo, Mbweni Jijini Dar es Salaam. Mabao ya JKT Tanzania yamefungwa na mshambuliaji Edward Songo dakika ya 40 kwa penalti na beki Wilson Nangu dakika ya 61. Kwa ushindi huo, JKT Tanzania inafikisha pointi 26 na kupanda kwa nafasi mbili hadi ya sita, wakati Kagera Sugar inabaki na pointi zake 15 nafasi ya 15 kwenye ligi ya timu 16 baada ya wote kucheza mechi 21.

TANZANIA PRISONS YATOA SARE NA TABORA UNITED, 1-1SOKOINE

Image
WENYEJI, Tanzania Prisons wamelazimishwa sare ya kufungana bao 1-1 na Tabora United katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara mchana wa leo Uwanja wa Sokoine Jijini Mbeya. Beki Mnigeria, Emmanuel Ugochucku Chigozie alianza kujifunga dakika ya 67 kuiipatia Tanzania Prisons bao la kuongoza, kabla ya Emmanuel Samuel kuisawazishia Tabora United dakika ya 82. Kwa matokeo hayo, Tanzania Prisons inafikisha pointi 18, ingawa inabaki nafasi ya 14, wakati Tabora United inafikisha pointi 34, nayo inabaki nafasi ya tano baada ya wote kucheza mechi 21. 

SIMBA SC NA AL MASRY ROBO FAINALI, IKIVUKA INA ZAMALEK

Image
KLABU ya Simba itamenyana na Al Masry ya Misri katika Robo Fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika mechi ya kwanza ikichezwa Aprili 3 Jijini Cairo na marudiano Aprili Aprili 10 Jijini Dar es Salaam. Ikifanikiwa kuvuka hapo na kwenda Nusu Fainali itakutana na mshindi kati ya Stellenbosch ya Afrika Kusini na mabingwa, watetezi, Zamalek ya Misri. Katika Ligi ya Mabingwa Afrika, mabingwa watetezi, Al Ahly watamenyana na Al Hilal ya Sudan, wakati MC Alger ya Algeria itamenyana na Orlando Pirates ya Afrika Kusini.

TWIGA STARS YAICHAPA EQUTORIAL GUINEA 3-1 KUFUZU WAFCON

Image
TIMU ya soka ya taifa ya wanawake, Twiga Stars imeibuka na ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Equtorial Guinea  katika mchezo wa kwanza Raundi ya Kwanza kufuzu Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika kwa Wanawake, (WAFCON) 2026 jioni ya leo Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam. Mabao ya Twiga Stars yamefungwa na kiungo, Stumai Abdallah Athumani wa JKT Queens dakika ya 49 na washambuliaji Enekia Kasonga ‘Lunyamila’ wa Mazatlán ya Mexico dakika ya 55 na Diana Lucas Msewa wa Trabzonspor ya Uturuki dakika ya 90’+4. Bao pekee la Equtorial Guinea limefungwa na beki, Gertrudis Engueme Obiang Midje wa anayechezea klabu ya Real Sociedad II ya Hispania. Timu hizo zitarudiana Februari 26 Uwanja wa Malabo, Malabo kuanzia Saa 10:00 na mshindi wa jumla atakutana na Uganda na Ethiopia kuwania kufuzu raundi ya mwisho ya mchujo.

NAMUNGO FC 0-3 SIMBA SC (LIGI KUU YA NBC TZ BARA)

Image
 

AHOUA AFUNGA PENALTI MBILI, ATEBA AKOSA MOJA SIMBA YAICHAPA NAMUNGO PUNGUFU 3-0 RUANGWA

Image
TIMU ya Simba SC imeibuka na ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Namungo FC katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara usiku huu Uwanja wa Majaliwa, Ruangwa mkoani Lindi. Mabao ya Simba SC yamefungwa na kiungo Muivory Coast, Jean Charles Ahoua mawili yote kwa penalti dakika ya 45 na 71, wakati lingine amefunga mshambuliaji Mganda, Steven Dese Mukwala dakika ya 90’+1. Simba ingeweza kuondoka na ushindi mnono zaidi kama si mshambuliaji Mcameroon Christian Leonel Ateba Mbida kukosa penalti nyingine dakika ya 52. Namungo FC ilimaliza pungufu mchezo huo baada ya beki wake Derick Mukomnozi kutolewa kwa kadi nyekundu dakika ya 33. Kwa ushindi huo, Simba SC inafikisha pointi 50 katika mchezo w 19, ingawa inabaki nafasi ya pili ikizidiwa pointi mbili na mabingwa watetezi, Yanga ambao pia wamecheza mechi moja zaidi. Kwa upande wao Namungo FC baada ya kupoteza mchezo huo wanabaki na pointi zao 21 za mechi 20 nafasi y 13 kwenye Ligi ya timu 16.

MASHUJAA FC YAICHAPA PAMBA JIJI 2-0 LAKE TANGANYIKA

Image
WENYEJI, Mashujaa wameibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Pamba Jiji katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa Lake Tanganyika mjini  Kigoma. Mabao ya Mashujaa FC leo yamefungwa na kiungo Hassan Haji Ali dakika ya 35 na winga David Richard Ulomi dakika ya 83 — na kwa ushindi huo, Mashujaa inafikisha pointi 23 katika mchezo wa 20 na kuruka kutoka nafasi ya 13 hadi ya sita. Kwa upande wao Pamba Jiji FC baada ya kupoteza mchezo huo wanabaki na pointi zao 21 za mechi 20 pia na kushukia kwa nafasi moja hadi ya 12 kwenye Ligi ya timu 16, ambayo mwisho wa msimu mbili zitashuka. Timu nyingine mbili zitakazomaliza nafasi y 13 na 14 zitamenyana baina yao kwa mechi mbili za nyumbani na ugenini na mshindi wa jumla atasalia Ligi Kuu, wakati timu itakayofungwa itakwenda kumenyana na timu ya Championship kujaribu tena kubaki Ligi Kuu.

DODOMA JIJI YAICHAPA TANZANIA PRISONS 3-2 JAMHURI

Image
WENYEJI, Dodoma Jiji FC wameibuka na ushindi wa mabao 3-2 dhidi ya Tanzania Prisons katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara usiku huu Uwanja wa Jamhuri, Dodoma. Mabao ya Dodoma Jiji yamefungwa na Paul Peter dakika ya 57, Iddi Kipagwile dakika ya 64 na Augustine Samson dakika ya 90’+4, wakati ya Tanzania Prisons yamefungwa na Beno Khalfan Ngassa dakika ya 19 na Lambert Sibiyanka dakika ya 78. Kwa ushindi huo, Dodoma Jiji FC wanafikisha pointi 23 katika mchezo wa 19 na kusogea nafasi ya saba kutoka ya 13, wakati Tanzania Prisons inabaki na pointi zake 17 za mechi 20 nafasi ya 14.

KENGOLD YAICHAPA KAGERA SUGAR 1-0 SOKOINE, LAKINI BADO INASHIKA MKIA

Image
WENYEJI, Kengold wameibuka na ushindi wa 1-0 dhidi ya Kagera Sugar katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara jioni ya Uwanja wa Sokoine Jijini Mbeya. Bao pekee lililoipa pointi tatu muhimu Kengold inayopambana kwa bidi kuepuka kushuka daraja – limefungwa na kiungo Mishamo Daud Charles dakika ya 81 akimalizia kazi nzuri ya mshambuliaji,  Suleiman Salim Rashid 'Bwenzi'. Kwa ushindi huo, Kengold wanafikisha pointi 13, ingawa wanaendelea kushika mkia katika ligi ya timu ya 16, wakizidiwa pointi mbili na Kagera Sugar iliyopo nafasi ya 15 baada ya wote kucheza mechi 20 sasa.

FOUNTAIN GATE NA TABORA UNITED HAKUNA MBABE, SARE 0-0 BABATI

Image
WENYEJI, Fountain Gate wametoka sare ya bila mabao na jirani zao, Tabora United katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa Tanzanite Kwaraa mjini Babati mkoani Manyara. Kwa matokeo hayo, Fountain Gate inafikisha pointi 22 na kusogea nafasi ya saba, wakati Tabora United inafikisha pointi 33 na inabaki nafasi ya nne baada ya wote kucheza mechi 20.  

AZAM FC YAICHAPA MASHUJAA MABAO 2-0 CHAMAZI

Image
WENYEJI, Azam FC wameibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Mashujaa FC katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara usiku huu Uwanja wa Azam Complex, Chamazi Jijini Dar es Salaam. Mabao ya Azam FC yamefungwa na kiungo Zidane Sereri dakika ya 72 na    beki kutoka Mali, Yoro Mamadou Diaby dakika ya 82. Kwa ushindi huo, Azam FC inafikisha pointi 42 katika mchezo wa 19, ingawa inabaki nafasi ya tatu nyuma ya Simba SC yenye pointi 47 za mechi 18 na mabingwa watetezi, Yanga wenye pointi 49 za mechi 19. Kwa upande wao Mashujaa baada ya kupoteza mchezo wa leo wanabaki nafasi ya 10 na pointi zao 20 za mechi 19 pia.

PAMBA JIJI YAIKANDA COASTAL UNION 2-0 KIRUMBA NA KUJITOA ‘DANGER ZONE’

Image
WENYEJI, Pamba Jiji FC wameibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Coastal Union ya Tanga katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara leo Uwanja wa CCM Kirumba Jijini Mwanza. Mabao ya Pamba Jiji leo yamefungwa na kiungo John Ben Nakibinge dakika ya 18 na mshambuliaji Mguinea, Abdoulaye Yonta Camara dakika ya 21. Kwa ushindi huo, Pamba Jiji wanafikisha pointi 21 na kupanda kutoka nafasi ya 13 hadi ya nane ikizizidi tu wastani wa mabao Namungo FC na Fountain Gate baada ya wote kucheza mechi 19. Kwa upande wao Coastal Union baada ya kupoteza mchezo huo wanabaki na pointi zao 22 za mechi 19 pia wakibaki katika nafasi ya tisa, wakiizidi wastani wa mabao tu KMC ambayo nayo ina mechi 19 za kucheza.

KMC 1-6 YANGA SC (LIGI KUU Y NBC TZ BARA)

Image
 

AZIZ KI APIGA HAT TRICK YANGA YAICHAPA KMC 6-1 MWENGE

Image
MABINGWA watetezi, Yanga wamerejea kileleni mwa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara baada ya ushindi wa mabao 6-1 dhidi ya wenyeji, KMC  jioni ya leo Uwanj wa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni, KMC Complex, Mwenge, Dar es Salaam. Ilikuwa ni siku nzuri kwa kiungo Mburkinabe, Stephane Aziz Ki aliyefunga mabao matatu, mawili kwa penalti dakika ya 18 na 56 na lingine dakika ya 49. Mabao mengine ya Yanga yamefungwa na mshambuliaji Mzimbabwe, Prince Dube Mpumelelo dakika ya 10, kiungo Mkongo, Maxi Mpia Nzengeli dakika ya 90’+1 na beki mzawa, Israel Patrick Mwenda dakika ya 90’+4. Bao pekee la KMC leo limefungwa na kiungo Redemtus Jeremiah Mussa akimtungua kwa shuti la mbali kipa namba moja wa Mali, Djigui Diarra dakika ya 51. Kwa ushindi huo, Yanga inafikisha pointi 49 katika mchezo wa 19 na kurejea kileleni, ikiizidi pointi mbili Simba ambayo pia ina mechi moja mkononi. Kwa upande wao KMC baada ya kichapo cha leo inabaki na pointi zake 22 za mechi 19 nafasi ya saba kwenye ligi ya t...

TABORA UNITED YAAMBULIA SARE KWA KENGOLD, 1-1 MWINYI

Image
WENYEJI, Tabora United wamelazimisha sare ya kufungana bao 1-1 na Kengold katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara leo Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi mjini Tabora. Kengold walianza kupata bao lilkfungwa kwa mkwaju wa penalti na  mshambuliaji wake tegemeo, Suleiman Salim Rashid 'Bwenzi' dakika ya 25, kabla ya mshambuliaji Mkongo, Heritier Ma Olongi Makambo kuisawazishia Tabora United dakika ya 87. Kwa matokeo hayo, Tabora United inafikisha pointi 32 na inabaki nafasi ya tano, nyuma ya Singida Black Stars yenye pointi 37 baada ya wote kucheza mechi 19. Kwa upande wao Kengold baada ya sare ya leo wanaendelea kushika mkia katika ligi ya timu 16 wakifikisha pointi 10 katika mchezo wa 19 pia.

SINGIDA BLACK STARS YAICHAPA JKT TANZANIA 1-0 MBWENI

Image
BAO pekee la mshambuliaji Mghana, Jonathan Sowah dakika ya 51 limeipa Singida Black Stars ushindi wa 1-0 dhidi ya wenyeji, JKT Tanzania katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa Meja Jenerali Charles Isamuhyo, Mbweni, Dar es Salaam. Kwa ushindi huo, Singida Black Stars inafikisha pointi 37 katika mchezo wa 19,  ingawa inabaki nafasi ya nne ikizidiwa pointi mbili na Azam FC ambayo pia ina mechi moja mkononi. Kwa upande wao JKT Tanzania baada ya kichapo cha leo wanabaki na pointi zao 20 za mechi 19 pia nafasi ya 10. 

TABORA UNITED YAICHAPA KAGERA SUGAR 2-1 PALE PALE KAITABA

Image
TIMU ya Tabora United imeibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya wenyeji, Kagera Sugar katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara leo Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba. Mabao ya Tabora United yamefungwa na mshambuliaji Offen Francis Chikola dakika ya 52 na beki Mkongo, Andy Bikoko dakika ya 77, wakati la Kagera Sugar limefungwa na kiungo Cleophace Anthony Mkandala dakika ya 90’+5. Kwa ushindi huo, Tabora United imefikisha pointi 31, ingawa inabaki nafasi ya tano ikizidiwa pointi tatu na Singida Black Stars baada ya wote kucheza mechi 18. Kwa upande wake Kagera Sugar hali inazidi kuwa mbaya baada ya kupoteza mchezo huo wakibaki na pointi zao 12 za mechi 18 Sasa nafasi ya 15 kwenye ligi ya timu 16.

CHASAMBI AFUNGA LA TATU SIMBA YAICHAPA PRISONS 3-0 MWENGE

Image
WENYEJI, Simba SC wameibuka na ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Tanzania Prisons katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni, KMC Complex, Mwenge, Dar es Salaam. Mabao ya Simba SC yote leo yamefungwa na viungo, Muivory Coast, Jean Charles Ahoua dakika ya 29, Mkongo, Ellie Mpanzu Kibisawala dakika ya 44 na mzawa, Ladack Juma Chasambi dakika ya 45’+2. Kwa ushindi huo, Simba SC inafikisha pointi 47 na kurejea kileleni mwa Ligi Kuu ikiwazidi pointi moja mabingwa watetezi, Yanga baada ya wote kucheza mechi 18. Kwa upande wao Tanzania Prisons baada ya kupoteza mchezo wa leo wanabaki na pointi zao 17 za mechi 18 Sasa nafasi ile ile ya 14 kwenye ligi ya timu 16.

MASHUJAA NA COASTAL UNION HAKUNA MBABE, 0-0 KIGOMA

Image
WENYEJI, Mashujaa FC wamelazimishwa ya bila mabao na Coastal Union katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa Lake Tanganyika mjini Kigoma. Kwa matokeo hayo, 20 na kusogea nafasi ya tisa ikizizidi tu wastani wa mabao JKT Tanzania na Dodoma Jiji baada ya wote kucheza mechi 18. Kwa upande wao Coastal Union wanafikisha pointi 22 na kusogea nafasi ya sita ikiizidi tu wastani wa mabao KMC baada ya nao pia kucheza mechi 18.

JKT TANZANIA 0-0 YANGA SC (LIGI KUU YA NBC TZ BARA)

Image

KMC YAILAMBA SINGIDA BLACK STARS MABAO 2-0 MWENGE

Image
WENYEJI, KMC wamebuka na ushindi wa 2-0 dhidi ya Singida Black Stars katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni, KMC Complex, Mwenge, Dar es Salaam. Mabao ya KMC yaliyoizamisha Singida Black Stars leo  yote yamefungwa na Paul Oscar dakika ya 35 na 40. KMC inafikisha pointi 20 katika mchezo wa 18 pia na kusogea nafasi ya tisa, wakati Singida Black Stars inabaki na pointi zake 34 nafasi ya nne baada ya kucheza mechi 18 pia.

KENGOLD YAICHAPA FOUNTAIN GATE MABAO 2-0 UWANJA WA SOKOINE

Image
WENYEJI, Kengold wameibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Fountain Gate katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara leo Uwanja wa Sokoine Jijini Mbeya.   Mabao ya Kengold yamefungwa na mshambuliaji Suleiman Salim Rashid 'Bwenzi' dakika ya 33 kwa penalti baada ya yeye mwenyewe kuangushwa na Fadhil Kisungi na la pili amefunga mshambuliaji Mzambia, Obrey Choro Chirwa dakika ya 83 akimalizia pasi ya Rodgers Gabriel. Kwa ushindi huo, Kengold inafikisha pointi tisa katika mchezo wa 18, ingawa inaendelea kushika mkia katika ligi ya timu 16, wakati Fountain Gate inabaki na pointi zake 21 za mechi 18 pia nafasi ya saba. 

NAMUNGO FC YAAMBULIA SARE KWA DODOMA JIJI, 2-2 RUANGWA

Image
WENYEJI, Namungo FC wamelazimishwa sare ya kufungana mabao 2-2 na Dodoma Jiji katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara usiku huu Uwanja wa Majaliwa, Ruangwa mkoani Lindi. Mabao ya Namungo FC yamefungwa na Pius Buswita dakika y 44 na Erasto Nyoni dakika ya 56 kwa penalti, wakati ya Dodoma Jiji yamefungwa na Paul Peter dakika ya   21 na Apollo Otieno dakika ya 31. Kwa matokeo hayo, Namungo FC wanafikisha pointi 18 katika mchezo wa 18 na kushuka kwa nafasi moja hadi ya 13, wakati Dodoma Jiji wanafikisha pointi 20 katika mchezo wa 18 na kupanda kwa nafasi mbili hadi ya nane.

KIJANA WETU KAANZIA BENCHI MECHI YA LIGI YA MOROCCO USIKU WA LEO

Image
KOCHA Muafrika Kusini, Rulani Mokwena amemuanzishia benchi mshambuliaji mpya wa Wydad Athletic Club, Suleiman Mwalimu Abdallah ‘Gomez’ Katika mchezo wa Ligi Kuu ya Morocco, Botola Pro dhidi ya Hassania Union Sport d'Agadir unaotarajiwa kuanza Saa 4:00 usiku wa leo Uwanja wa Larbi Zaouli Jijini Casablanca. GONGA KUTAZAMA ZAIDI CHUMBA CHA WACHEZAJI WYDAD AC

KASEKE AFUNGA DAKIKA ZA JIONI PAMBA YAILAZA AZAM FC 1-0

Image
WENYEJI, Pamba Jiji wameibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Azam FC katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa CCM Kirumba Jijini Mwanza. Bao lililowazamisha Azam FC leo limefungwa na kiungo mkongwe, Deus David Kaseke dakika ya 86, akigusa mpira wa kwanza baada tu ya kuingia kutokea benchi kuchukua nafasi ya kiungo Mrundi, Shassir Nahimana. Ushindi huo wa pili mfululizo wakitoka kushinda ugenini dhidi ya Dodoma Jiji 1-0 pia — unaifanya Pamba Jiji FC ifikishe pointi 18 katika mchezo wa 18 na kupanda kwa nafasi mbili hadi ya 12, wakati Azam FC inabaki na pointi zake 39 za mechi 18 pia nafasi ya tatu.

COASTAL UNION YAICHAPA JKT TANZANIA 2-1 ARUSHA

Image
WENYEJI, Coastal Union wameibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya JKT Tanzania katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara leo Uwanja wa Sheikh Amri Abeid Jijini Arusha. Mabao ya Coastal Union yamefungwa na Bakari Msimu dakika ya 26 na Maabad Maulid dakika ya 68, wakati la JKT Tanzania alijifunga beki Lameck Lawi dakika ya 64. Kwa ushindi huo, Coastal Union inafikisha pointi 21 na kusogea nafasi ya sita, wakati JKT Tanzania wanabaki na pointi zao 19 na kushuka kwa nafasi moja hadi ya tisa baada ya wote kucheza mechi 17.

YANGA NA COASTAL 32 BORA KOMBE LA CRDB, AZAM NA SIMBA WAPATA VIBONDE

Image
MABINGWA watetezi, Yanga watamenyana na Coastal Union ya Tanga katika hatua ya 32 Bora Kombe la Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), michuano inayodhaminiwa na  Benki ya CRDB. Vigogo wengine wa soka nchini, Simba SC watamenyana na TMA Stars ya Arusha, Azam FC na Mbeya City, wakati Singida Black Stars watamenyana na Leo Tena FC ya Bukoba. MECHI ZOTE HATUA YA 32 BORA KOMBE LA CRDB JKT Tanzania Vs Biashara United  Tabora United Vs Transit Camp  Mashujaa FC Vs Geita Gold  Simba SC Vs TMA Star's  AzamFC Vs Mbeya City  Singida Black Stars Vs Leo Tena FC  Yanga SC Vs Coastal Union  Fountain Gate Vs Stand United  Cosmolitan Vs KMC  Mbeya Kwanza Vs Mambali Ushirikiano  Tanzania prisons Vs Bigman FC  Kagera Sugar Vs Namungo FC  Polisi Tanzania Vs Songea United  Kiluvya FC Vs Pamba Jiji  Mtibwa sugar Vs Tows Stars Girrafu Academy Vs Green Worries

PAMBA JIJI YAICHAPA DODOMA JIJI 1-0 PALE PALE JAMHURI

Image
BAO pekee la mshambuliaji Mkenya, Mathew Tegisi Momanyi dakika ya 23 limetosha kuipa Pamba Jiji FC ushindi wa ugenini wa 1-0 dhidi ya wenyeji, Dodoma Jiji katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara leo Uwanja wa Jamhuri Jijini Dodoma. Kwa ushindi huo, Pamba Jiji inafikisha pointi 15 katika mchezo wa 17, japokuwa inabaki nafasi ya 14 na Dodoma Jiji inabaki na pointi zake 19 za mechi 17 nafasi ya tisa.

YANGA SC 6-1 KENGOLD (LIGI KUU YA NBC TZ BARA)

Image
 

TABORA UNITED YAZINDUKA NA KUICHAPA NAMUNGO FC 2-1

Image
TIMU ya Tabora United imezinduka na kupata ushindi wa 2-1 dhidi ya Namungo FC katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara leo Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi mjini Tabora. Mabao ya Tabora United leo yamefungwa na winga Offen Francis Chikola dakika ya 32 na mshambuliaji Mkongo, Heritier Ma Olongi Makambo dakika ya 52, baada ya kiungo Jacob Raymond Massawe kuanza kuifungia Namungo FC dakika ya nne. Kwa ushindi huo, Tabora United wanafikisha pointi 28, ingawa wanabaki nafasi ya tano, wakati Namungo FC inabaki na pointi zake 17 nafasi ya 12 kwenye ligi ya timu 16 baada ya wote kucheza mechi 17.

MZIZE NA DUBE KILA MMOJA APIGA MBILI YANGA YASHINDA 6-1

Image
MABINGWA watetezi, Yanga SC wameibuka na ushindi wa mabao 6-1 dhidi ya Kengold katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni, KMC Complex, Mwenge Jijini Dar es Salaam. Mabao ya Yanga leo yamefungwa na washambuliaji, Mzimbabwe Prince Dube Mpumelelo mawili, dakika ya pili na 46, Clement Francis Mzize dakika ya sita na 43, viungo, Muivory Coast Pacome Peodoh Zouzoua dakika ya 39 na Mkenya,  Duke Ooga Abuya dakika ya 84. Bao pekee la Kengold katika mchezo wa leo limefungwa dakika ya 90’+3 na kiungo mpya, Suleiman Bwenzi aliyesajiliwa dirisha dogo kutoka Mbeya Kwanza ya Championship. Kwa ushindi huo, Yanga inafikisha pointi 45 katika mchezo wa 17 na kupanda kileleni mwa Ligi Kuu ikiwazidi pointi mbili watani, Simba SC ambao pia wana mechi moja mkononi na kesho wanaweza kuurejea uongozi wakiifunga Fountain Gate huko Babati. Kengold hali inazidi kuwa mbaya baada ya matokeo ya leo katika mchezo wa 17 wa msimu ikibaki na po...

KOCHA MPYA YANGA AMEFUNDISHA UFARANSA, KUWAIT, SAUDI ARABIA, MOROCCO NA KLABU KUBWA ALGERIA

Image
KOCHA mpya wa Yanga, Miloud Hamdi (53), Mualgeria mwenye uraia wa Ufaransa ana uzoefu wa kufundisha soka tangu mwaka 2004 alipoanza na timu ya vijana nchini Ufaransa, ES Vitrolles, kabla ya kuhamia GS Consolat mwaka 2009 hadi 2012 . Baada ya hapo akaenda Ettifaq U21 ya Saudi Arabia hadi mwaka 2015 USM Alger akaajiriwa kama Kocha Msaidizi wa USM Alger ya Algeria, kabla ya kupewa Ukocha Mkuu mwaka 2016. Baadaye mwaka 2016 akaenda Nahdat Berkane ya Morocco, kabla ya kurejea USM Alger mwaka 2017 hadi 2018 akaenda Al-Salmiya SC ya  Kuwaiti, kabla ya kurejea Algeria mwaka 2021 kufundisha CS Constantine hadi 2022 alipohamia JS Kabylie hadi mwaka jana. Anajiunga na Wananchi kuchukua nafasi ya Siad Ramovic mwenye uraia wa Ujerumani aliyeondoka ghafla jana.

YANGA SC YAACHANA NA RAMOVIC, YALETA KOCHA WA USM ALGER

Image
KLABU ya Yanga imeachana na kocha Siad Ramovic mwenye uraia wa Ujerumani na kumtambulisha, Miloud Hamdi, Mualgeria mwenye uraia wa Ufaransa pia kuwa Kocha wake Mkuu ambaye anaungana na timu mara moja.

MAHOJIANO BIN ZUBEIRY NA ABEID KASABALALA ALIYETAMBA MECCO NA RELI

Image
 

TABORA UNITED 0-3 SIMBA SC (LIGI KUU YA NBCA TZ BARA)

Image
 

ATEBA APIGA MBILI SIMBA SC YAITANDIKA TABORA UNITED 3-0

Image
TIMU ya Simba SC imerejea kileleni mwa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara baada ya ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya wenyeji, Tabora United katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara leo Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi mjini Tabora. Chachu ya ushindi wa leo ni winga Mkongo, Elie Mpanzu Kibisawala aliyesaidia upatikanaji wa mabao yote, mawili yakifungwa na mshambuliaji Mcameroon, Leonel Christian Ateba Mbida na lingine beki, Shomari Salum Kapombe. Bao la kwanza Ateba alipokea pasi ya Mpanzu na kufunga dakika ya 12 na la pili akafunga kwa penalti dakika ya 34 kufuatia Mkongo huyo kuangushwa na beki Mkongo-Brazzaville, Faria Jobel Ondongo.  Bao la tatu Ateba alipokea pasi ya Mpanzu tena akiwa kwenye nafasi ya kufunga, lakini akamsetia Kapombe aliyekuwa anatokea nyuma  na kufumua shuti lililotinga nyavuni. Kwa ushindi huo, Simba SC inafikisha pointi 43 na kurejea kileleni ikiwazidi pointi moja mabingwa watetezi, Yanga baada ya wote kucheza mechi 16. Tabora United kwa upande wao wan...

YANGA SC 4-0 KAGERA SUGAR (LIGI KUU YA NBZ TZ BARA)

Image
 

YANGA SC YAREJEA KILELENI BAADA YA KUICHAPA KAGERA SUGAR 4-0

Image
MABINGWA watetezi, Yanga SC wamerejea kileleni mwa Ligi Kuu ya NBC ya Tanzania Bara baada ya ushindi wa mabao 4-0 dhidi ya Kagera Sugar jioni ya leo Uwanja wa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni, KMC Complex, Mwenge Jijini Dar es Salaam. Mabao ya Yanga leo yamefungwa na nyota wazawa, mshambuliaji Clement Francis Mzize dakika ya 32, kiungo Mudathir Yahya Abbas dakika ya 60, kiungo Muivory Coast, Pacome Zouzoua Peodoh kwa penalti dakika ya 78 na mshambuliaji Mzambia, Kennedy Musonda dakika ya 86. Yanga ingeweza kuondoka na ushindi wa mabao 5-0 leo kama kiungo Mburkinabe, Stephane Aziz Ki. Kwa ushindi huo, Yanga inafikisha pointi 42 katika mchezo wa 16 na kupanda juu ya msimamo, ikiizidi pointi mbili Simba ambayo pia ina mechi moja mkononi na kesho inacheza na Tabora United mjini Tabora. Kwa upande wao Kagera Sugar baada ya kipigo cha leo 11 za mechi 16 nafasi ya 15 kwenye ligi ya timu 16 — mbele ya Ken Gold yenye pointi sita za mechi 16 pia.