Posts

Showing posts from April, 2025

TANZANIA YACHAPWA 3-2 NA MOROCCO FAINALINYA FUTSAL AFRIKA

Image
TANZANIA jana imefungwa mabao 3-2 na wenyeji, Morocco katika mchezo wa Fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika ya Futsal kwa Wanawake Afrika Uwanja wa Salle Moulay Abdellah Jijiji Rabat. Mabao ya Morocco yalifungwa na El Madani dakika ya 19, Korrych dakika ya  33 na Demraoui dakika ya 39, wakati ya Tanzania yalifungwa na Anastasia Antony Katunzi dakika ya tatu na na Jamila Rajab Mnunduka dakika ya 15. Kipa wa Tanzania, Naijat Idrisa Bakari alichaguliwa mchezaji bora baada ya mchezo huo wa Fainali. Pamoja na kufungwa katika mchezo wa Fainali, Tanzania nayo imeumgana na Morocco kufuzu Fainali za Kombe la Dunia za Futsal zitakazofanyika nchini  Philippines kuanzia Novemba 21 hadi Desemba 7, mwaka huu.

TANZANIA YAANZA VIBAYA AFCON U20, YACHAPWA 1-0 NA AMAJITA

Image
TANZANIA imeanza vibaya Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika  kwa vijana chini ya Umri wa miaka 20 baada ya kuchapwa bao 1–0 na Afrika Kusini katika mchezo wa Kundi A leo Uwanja wa  Suez Canal Jijini Ismailia nchini Misri inakofanyika michuano hiyo. Bao pekee la Amajita lililoizamisha Ngorongoro Heroes limefungwa na Shakeel April wa Cape Town City dakika ya 27 akimalizia kazi nzuri ya Mogamat Faiz Abrahams wa Stellenbosch, wote viungo. Ngorongoro Heroes itashuka tena dimbani Mei 3 kumenyana na  Sierra Leone, kabla ya kucheza na Zambia Mei 6 na kukamilisha mechi zake za Kundi A Mei 9 kwa kumenyana na wenyeji, Misri. 

ZIMAMOTO 1-1 (PENALTI 1-3) YANGA SC (KOMBE LA MUUNGANO)

Image
 

YANGA NAO WAINGIA FAINALI KWA MATUTA PEMBA

Image
MABINGWA wa Tanzania, Yanga SC wamefanikiwa kuingia Fainali ya Kombe la Muungano baada ya ushindi wa penalti 3-1 dhidi ya Zimamoto kufuatia sare ya kufungana 1-1 ndani ya dakika 90 Uwanja wa Gombani, Pemba. Shujaa wa Yanga leo ni kipa Abdultwalib Hamidu Mshery aliyeokoa penalti za wachezaji wawili wa Zimamoto, Said Mwinyi na  Suleiman Said, huku ya Yussuf Idrisa ilkigonga mwamba na ya Abdulhamid Ramadhan pekee ndiyo ilimpita na kutinga nyavuni. Waliofunga penalti za Yanga ni mabeki Israel Patrick Mwenda na Bakari Nondo Mwamnyeto na mshambuliaji Clement Francis Mzize huku ya Maxi Mpia Nzengeli pekee ikienda nje. Katika dakika 90 za mchezo, Yanga walitangulia kupata bao kupitia kwa kiungo Mkongo, Maxi Mpia Nzengeli dakika ya 29, kabla ya Said Mwinyi kuisawazishia Zimamoto kwa penalti dakika ya 71. Fainali ya michuano hiyo maalum ya kuazimisha sherehe za Muungano wa Tanganyika na Zanzibar uliozaa Tanzania tukufu Aprili 26 itachezwa Mei 1 hapo hapo Uwanja wa Gombani — na Yanga ...

KOCHA MMOROCCO WA AZAM FC ALIMWA FAINI KWA KUWAFANYIA FUJO MAREFA

Image
KOCHA wa Azam FC, Mmorocco Rachid Taoussi ametozwa Faini ya Sh. 500,000 kwa kosa la kuwafanyia fujo na kuwarushia chupa marefa katika dhidi na ya wenyeji, Singida Black Stars Aprili 6 Uwanja wa CCM LITI mjini Singida. Rachid Taoussi aliye katika msimu wake wa kwanza Azam FC amedaiwa kufanya hayo baada ya mchezo huo ambao timu yake ilichapwa 1-0, bao pekee la mshambuliaji Mkenya, Elvis Baranga Rupia dakika ya 75.

RAIS SAMIA AZIPONGEZA TIMU ZA TAIFA ZA FUTSAL NA WANAFUNZI

Image
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan amezipongeza timu ya taifa Futsal na ya vijana chini ya miaka 15 kwa kufanya vyema kwenye mashindano ya Kimataifa. “Ninaipongeza Timu ya Taifa ya Vijana chini ya umri wa miaka 15 kwa kuwa mabingwa wa Mashindano ya Mpira wa Miguu kwa Shule za Afrika (CAF African Schools Football Championship) kwa mara ya pili mfululizo. Ninajivunia ushindi wenu kwani ni fahari kwa Taifa letu na chachu ya kuendelea kukua kwa sekta ya michezo nchini,” amesema Rais Dk. Samia katika taarifa yake leo. Tanzania juzi ilifanikiwa kutwaa ubingwa wa Michuano ya Ubingwa wa Shule za Afrika (ASFC), inayoshirikisha vijana chini ya umri wa miaka 15 kwa mara ya pili mfululizo baada ya ushindi wa Penalti 3-2 dhidi ya Senegal kufuatiua sare ya bila mabao Uwanja wa Chuo Kikuu cha Ghana Jijini Accra. Hiyo inakuwa mara ya pili mfululizo kwa vijana hao wa Tanzania kutwaa taji hilo  baada ya mwaka jana pia kuwa mabingwa visiwani Zanzibar. Upande wa wa...

AZAM FC YAUMALIZA MWENDO KOMBE LA MAPINDUZI

Image
TIMU ya JKU imefanikiwa kuingia Fainali ya Kombe la Muungano baada ya ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Azam FC usiku wa leo Uwanja wa Gombani, Pemba. Mabao ya JKU yamefungwa na Neva Adelin dakika ya 50 na Freddy Suleiman dakika ya 80, wakati bao pekee la Azam FC limefungwa na beki Mcolombia, Yeison Fuentes dakika ya 15. JKU sasa itasubiri mshindi wa Nusu Fainali ya kesho Kati ya Yanga na Zimamoto kukutana naye katika Fainali Mei 1.

TANZANIA MABINGWA TENA MICHUANO YA SHULE ZA AFRIKA WAVULANA

Image
TANZANIA imefanikiwa kutwaa ubingwa wa Michuano ya Ubingwa wa Shule za Afrika (ASFC), inayoshirikisha vijana chini ya umri wa miaka 15 kwa mara ya pili mfululizo baada ya ushindi wa Penalti 3-2 dhidi ya Senegal kufuatiua sare ya bila mabao jana Uwanja wa Chuo Kikuu cha Ghana Jijini Accra. Hiyo inakuwa mara ya pili mfululizo kwa vijana hao wa Tanzania kutwaa taji hilo  baada ya mwaka jana pia kuwa mabingwa visiwani Zanzibar. Upande wa wanawake, wenyeji Ghana waliweka heshima baada ya kutwaa ubingwa kwa ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Uganda. Michuano hiyo iliyofanyika kwenye viwanja Chuo Kikuu cha Ghana kuanzia Aprili 23 hadi 26 ilikutanisha vijana wenye vipaji bora kutoka kote barani Afrika, kusherehekea ubora, umoja na nguvu ya mabadiliko ya soka. Sherehe za kufunga mashindano hayo ya siku nne yanayofanyika kwa msimu wa tatu mfululizo zilihudhuriwa na Rais wa Shirikisho la Soka Afrika (CAF), Dk Patrice Motsepe na Mkuu wa Nchi ya Ghana, Rais John Dramani Mahama ambao kwa pamoj...

AL AHLY YAACHANA NA KOCHA KOLLER BAADA YA KUVULIWA UBINGWA WA AFRIKA

Image
KLABU ya Al Ahly imemfukuza kazi kocha mkuu Marcel Koller siku moja tu baada ya kuondolewa katika michuano ya  Ligi ya Mabingwa Afrika na Mamelodi Sundowns. Koller alishuhudia timu yake ikitupwa nje kwa sheria ya bao la ugenini baada ya bao la kujifunga la Yasser Ibrahim na kuifanya Mamelodi Sundowns kukata tiketi ya kucheza fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika. Ilimaanisha kuwa wababe hao wa Misri walishindwa kufika fainali kwa mara ya kwanza baada ya miaka sita, jambo ambalo lilisababisha bodi ya klabu hiyo kuitisha mkutano wa dharura. Katika mkutano huo iliamuliwa kuachana na mtaalamu huyo wa Uswisi, ambaye alikuwa ameshinda mataji 11 na klabu hiyo. Koller mwenyewe alikuwa ameelezea kusikitishwa kwake na timu yake kutotolewa kwa 'bahati mbaya' katika kwa Ligi ya Mabingwa ya CAF. "Sote tumesikitishwa sana, hatukupoteza mchezo," alisema baada ya mechi. Tulijifunga na kutupwa nje. Haifurahishi. Tulitaka kuandika historia, haikufanikiwa na bila shaka hatujafurahi...

KVZ 0-2 YANGA SC (KOMBE LA MUUNGANO)

Image
 

AZIZ KI AFUNGA YANGA YATINGA NUSU FAINALI KOMBE LA MUUNGANO

Image
MABINGWA wa Tanzania Bara, Yanga wamefanikiwa kuingia Nusu Fainali ya Kombe la Mapinduzi, michuano hiyo maalum ya kuazimisha miaka 61 ya Muungano baada ya ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya KVZ usiku huu Uwanja wa Gombani, Pemba. Ilikuwa siku nzuri kwa winga Dennis David Nkane aliyetoa pasi ya bao la kwanza lililofungwa na kiungo Mburkinabe, Stephane Aziz Ki dakika ya 28, kabla ya yeye mwenyewe kufunga la pili dakika ya 86. Yanga sasa itakutana na JKU iliyoitoa Singida Black Stars katika mchezo wa Nusu Fainali Jumanne, wakati Jumatatu itachezwa Nusu Fainali ya kwanza kati ya Azam FC na Zimamoto. Wakati Azam FC iliitoa KMKM kwa kuichapa bao 1-0, Zimamoto pia iliitupa nje Coastal Union  ya Tanga kwa kuichapa bao 1-0 pia hapo hapo Gombani. Fainali ya michuano hiyo maalum ya kuazimisha sherehe za Muungano wa Tanganyika na Zanzibar uliozaa Tanzania tukufu Aprili 26 itachezwa Mei 1 hapo hapo Uwanja wa Gombani. Mabingwa watetezi, Simba wameshindwa kushiriki michuano ya mwaka huu kwa sa...

MTIBWA SUGAR YAREJEA LIGI KUU BAADA YA MSIMU MMOJA TU TANGU ISHUKE

Image
TIMU ya Mtibwa Sugar imejihakikishia kurejea Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara baada ya msimu mmoja tu licha ya sare ya kufungana bao 1-1 na Big Man FC  jana Uwanja wa Ilulu mjini Lindi. Matokeo hayo yanaifanya Mtibwa Sugar ifikishe pointi 67 katika mechi ya 28, ambazo ni Mbeya City pekee inaweza kufikisha ikiwa itashinda mechi zake zote mbili za mwisho – hivyo imejihakikishia kuwa moja ya timu mbili zinazopanda Ligi Kuu. Big Man inabaki na pointi zake 46 nafasi ya saba ikiwa bado kwenye mawindo ya kupanda Ligi Kuu kupitia Play-Off.  

AZAM FC YATINGA FAINALI KOMBE LA MUUNGANO

Image
TIMU ya Azam FC imefanikiwa kutinga Nusu Fainali ya Kombe la Muungano baada ya ushindi wa bao 1-0 dhidi ya KMKM jioni ya leo Uwanja wa Gombani, Pemba. Pongezi kwa mfungaji wa bao hilo pekee, beki na Nahodha Lusajo Elukaga Mwaikenda dakika ya 63 na sasa Azam FC watakutana na JKU katika Nusu Fainali. Mchezo uliotangulia wa Robo Fainali jioni ya leo Zimamoto iliifunga Coastao Union 1-0 hapo hapo Uwanja wa Gombani na sasa itakutana na mshindi wa Robo Fainali ya mwisho kati ya Yanga na KVZ zitakazomenyana kesho kuanzia Saa 1:15 usiku hapo hapo Gombani. Mechi za Nusu Fainali ya michuano hiyo maalum ya kuazimisha sherehe za Muungano wa Tanganyika na Zanzibar uliozaa Tanzania tukufu Aprili 26, mwaka 1964 zitafuatia Aprili 28 na 29, wakati Fainali itachezwa Mei 1 hapo hapo Uwanja wa Gombani. Mabingwa watetezi, Simba wameshindwa kushiriki michuano ya mwaka huu kwa sababu wanakabiliwa na mechi ya marudiano ya Nusu Fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Stellenbosch ya Afrika Kusini...

MAMELODI YAING’OA AL AHLY DAKIKA YA MWISHO KABISA

Image
TIMU ya Mamelodi Sundowns FC imeingia Fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika baada ya kuwatoa mabingwa watetezi, Al Ahly kufuatia sare ya 1-1 leo Uwanja wa Cairo International Jijini Cairo nchini Misri. Mamelodi Sundowns wanakwenda Fainali kwa faida ya mabao ya ugenini kufuatia sare ya bila mabao katika mchezo wa kwanza Aprili 19 Uwanja wa Loftus Versfeld Jijini Pretoria, Afrika Kusini. Katika mchezo wa marudiniano leo, mshambuliaji Taher Mohamed alianza kuwafungia Ahly dakika ya 24, kabla ya Yasser Ibrahim kujifunga dakika ya 90 kuitemesha tonge kinywani timu yake na kuipeleka Fainali Mamelodi. Matokeo haya yanamaanisha Ahly inavuliwa taji hilo baada ya kukaa nalo kwa misimu miwili mfululizo, wakati Mamelodi wanakwenda Fainali kwa mara ya kwanza tangu mwaka 2016 walipotwaa taji hilo kwa ushindi wa 3-0 nyumbani na kipigo cha 1-0 ugenini. Mamelodi Sundowns sasa wanasubiri mshindi kati ya Pyramids ya Misri na Orlando Pirates ya Afrika Kusini kukutana naye katika Fainali - timu ambazo z...

ZIMAMOTO YAIREJESHA TANGA COASTAL UNION MAPEMA TU

Image
TIMU ya Zimamoto imefanikiwa kutinga Nusu Fainali ya Kombe la Muungano baada ya ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Coastao Union ya Tanga jioni ya leo Uwanja wa Gombani, Pemba. Pongezi kwa mfungaji wa bao hilo pekee, Rashid Salum dakika ya 28 na sasa wanaungana na ndugu zao, JKU waliokuwa wa kwanza kutinga Nusu Fainali jana jioni kwa ushindi wa penalti 6-5 kufuatia sare ya 2-2 ndani ya dakika ya 90 hapo hapo Uwanja wa Gombani, Pemba. Baadaye kuanzia Saa 1:15 usiku wa leo KMKM watacheza Azam FC ya Dar es Salaam katika Robo Fainali ya tatu ya michuano hiyo usiku hapo hapo Uwanja wa Gombani. Vigogo, Yanga watakamilisha hatua hiyo ya Robo Fainali ya michuano hiyo maalum ya kuazimisha sherehe za Muungano wa Tanganyika na Zanzibar uliozaa Tanzania tukufu Aprili 26, mwaka 1964 — kwa kumenyana na wenyeji wengine, KVZ kuanzia Saa 1:15 usiku. Mechi za Nusu Fainali zitafuatia Aprili 28 na 29, wakati Fainali itachezwa Mei 1 hapo hapo Uwanja wa Gombani. Mabingwa watetezi, Simba wameshindwa kushiri...

JKU YAITUPA NJE SINGIDA BLACK STARS KOMBE LA MUUNGANO

Image
TIMU ya JKU imefanikiwa kutinga Nusu Fainali ya Kombe la Muungano baada ya ushindi wa penalti 6-5 dhidi ya Singida Black Stars jioni ya leo Uwanja wa Gombani, Pemba. Katika dakika 90 za kawaida za mchezo mabao ya JKU yamefungwa na Tariq Mohamed dakika ya 28 kwa penalti na Freddy Suleiman dakika ya 45’+3, wakati ya Singida Black Stars yamefungwa na Victorien Adebayor dakika ya sita na Iddi Khalid dakika ya 25. Michuano hiyo maalum ya kuazimisha sherehe za Muungano wa Tanganyika na Zanzibar uliozaa Tanzania tukufu Aprili 26, mwaka 1964 itaendelea kesho kwa Zimamoto  kuumana na Coastal Union ya Tanga Aprili 25 kuanzia Saa 10:00 jioni, kabla yan KMKM watacheza Azam FC ya Dar es Salaam kuanzia Saa 1:15 usiku hapo hapo Uwanja wa Gombani. Vigogo, Yanga watakamilisha hatua hiyo ya Robo Fainali kwa kumenyana na wenyeji wengine, KVZ Jumamosi kuanzia Saa 1:15 usiku — wakati mechi za Nusu Fainali zitafuatia Aprili Jumatatu na Jumanne na Fainali itachezwa Mei 1 hapo hapo Uwanja wa Gombani...

SERIKALI YAGHARAMIA USAFIRI NA MALAZI SIMBA SC MARUDIANO NA STELLENBOSCH

Image
SERIKALI ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya Mheshimiwa Dk. Samia Samia Suluhu Hasan imegharamia usafiri na malazi kwa klabu ya Afrika kwenye mchezo wake wa marudiano wa Nusu Fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya wenyeji, Stellenbosch Jumapili. Katika barua yake ya shukrani kwa Rais Samia, Rais wa Simba SC, Mohamed 'Mo' Dewji ambaye pia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi amesema; "Tumepokea kwa moyo wa shukrani mchango wa malazi na usafiri kuelekea mchezo wetu wa marudiano wa Nusu Fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Stellenbosch utakaofanyika Afrika Kusini,". Mo Dewji ambaye ni Mbunge wa zamani wa jimbo la Singida mjini ametoa shukrani pia kwa Wizara ya Fedha na Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa kazi nzuri ya kuratibu safari hiyo.  Kikosi cha Simba SC kimeondoka leo kwa ndege maalum ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) waliyopewa na Serikali kikiwa na  wachezaji 23 kwa ajili ya mchezo huo wa Jumapili kuanzia Saa...

SIMBA SC KUONDOKA NA WACHEZAJI 23 KESHO KUIFUATA STELLENBOSCH

Image
KIKOSI cha Simba SC cha wachezaji 23 kinatarajiwa kuondoka kesho asubuhi kwenda Jijini Durban, Afrika Kusini kwa ajili ya mchezo wa marudiano wa Nusu Fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya wenyeji, Stellenbosch Jumapili. Simba SC inahitaji sare ya aina yoyote kukata tiketi ya Fainali baada ya ushindi wa 1-0 kwenye mchezo wa kwanza wa Jumapili ya juzi Uwanja wa New Amaan Complex, Zanzibar. Pongezi kwa mfungaji wa bao hilo pekee, kiungo wa Kimataifa wa Ivory Coast, Jean Charles Ahoua dakika ya 45'+2 kwa shuti la kitaalam la mpira wa adhabu lililomshinda kipa wa Afrika Kusini, Oscarine Masuluke. Mechi ya marudiano itaanza Saa 10:00 jioni pia Uwanja wa Moses Mabhida Jijini Durban na mshindi wa jumla atakutana na mshindi wa jumla Kati ya RSB Berkane ya Morocco na CS Constantine ya Algeria katika Fainali. Ikumbukwe ilishinda 4-0 kwenye mchezo wa kwanza mabao ya Youssef Mehri dakika ya kwanza, Msenegal, Paul Valère Bassène dakika ya 21 na Oussama Lamlaoui, mawili dakika ya ...

KOMBE LA MUUNGANO SASA MECHI ZOTE NI DIMBA LA GOMBANI KISIWANI PEMBA

Image
MICHUANO maalum ya kuazimisha sherehe za Muungano wa Tanganyika na Zanzibar uliozaa Tanzania tukufu Aprili 26, mwaka 1964 sasa itafanyika Uwanja wa Gombani, kisiwani Pemba kuanzia Aprili 24 hadi Mei 1, mwaka huu (2024). Serikali ya Mapinduzi Zanzibar imelazimika kuiondoa Uwanja wa New Amaan Complex, Zanzibar ambako ilipangwa kufanyika kati ya  Aprili 23 na Aprili 30 baada ya kupokea taarifa ya Shirikisho la Soka Afrika (CAF) ikielekeza Uwanja huo kutotumiwa mfululizo ili kulinda ubora wake. Na hiyo kwa sababu Uwanja huo utatumika kwa Fainali za Michuano ya Ubingwa wa Mataifa ya Afrika (CHAN), inayohusisha wachezaji wanaocheza ligi za nchini mwao pekee zinazoandaliwa kwa pamoja na Tanzania, Kenya na Uganda zitakazofanyika Agosti mwaka huu. Nchi hizo tatu za Afrika Mashariki pia ni wenyeji wa Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika 2027 zitakazofanyika Kati ya mwezi Juni na Julai mwaka huo. Katika ratiba mpya ya Kombe la Muungano, michuano inayoanzia hatua ya Robo Fainali, weny...

FOUNTAIN GATE 0-4 YANGA SC (LIGI KUU YA NBC TZ BARA)

Image
 

COASTAL UNION YAICHAPA KEN GOLD 2-1 MKWAKWANI NA KUISHUSHA DARAJA

Image
WENYEJI, Coastal Union wameibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Ken Gold katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara leo Uwanja wa Mkwakwani Jijini Tanga. Mabao ya Coastal Union yamefungwa na kiungo Bakari Msimu dakika ya 27 na mshambuliaji kutoka Mali, Amara Bagayoko dakika ya 37, wakati bao pekee la Ken Gold limefungwa na mshambuliaji Sadallah Lipangile dakika ya 39. Kwa ushindi huo, Coastal Union inafikisha pointi 31 na kusogea nafasi ya nane, wakati Ken Gold wanabaki na pointi zao 16 wakiendelea kushika mkia baada ya timu zote kucheza mechi 27.  Aidha, matokeo hayo yanamaanisha rasmi Ken Gold iliyopanda Ligi Kuu msimu kama mabingwa wa Championship wamekwishashuka daraja, kwani hata kama watashinda mechi zao tatu za mwisho watamaliza na pointi 25 ambazo zimekwishavukwa na Tanzania Prisons yenye pointi 27. Ligi Kuu inashirikisha timu 16 na mwisho wa msimu mbili zitashuka Daraja na mbili nyingine zitakazomaliza nafasi ya 14 na 13 zitamenyana baina yao na mshindi wa jum...

MZIZE APIGA MBILI YANGA YAITANDIKA FOUNTAIN GATE 4-0 BABATI

Image
MABINGWA watetezi, Yanga SC wameibuka na ushindi wa mabao 4-0 dhidi ya Fountain Gate katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara Uwanja wa Tanzanite Kwaraa, Babati mkoani Manyara. Mabao ya Yanga yamefungwa na mshambuliaji wake nyota, Clement Francis Mzize mawili dakika ya 39 na 70 na viungo, Mburkinabe Stephane Aziz Ki dakika ya 43 na Mzambia, Clatous Chota Chama dakika ya 89. Kwa ushindi huo, Yanga inafikisha pointi 70 katika mchezo wa 26 na kuendelea kuongoza Ligi Kuu kwa pointi 13 zaidi ya watani, Simba ambao hata hivyo wana mechi nne mkononi. Kwa upande wao Fountain Gate baada ya kupoteza mchezo wa leo wanabaki na pointi zao 29 za mechi 27 sasa nafasi ya 11.

SIMBA SC YAICHAPA STELLENBOSCH 1-0 ZANZIBAR BAO LA AHOUA

Image
TIMU ya Simba SC imeibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Stellenbosch FC ya Afrika Kusini katika mchezo wa kwanza was Nusu Fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika jioni ya leo Uwanja wa New Amaan Complex, Zanzibar. Pongezi kwa mfungaji wa bao hilo pekee, kiungo wa Kimataifa wa Ivory Coast, Jean Charles Ahoua dakika ya 45'+2 kwa shuti la kitaalam la mpira wa adhabu lililomshinda kipa wa Afrika Kusini, Oscarine Masuluke. Timu hizo zitarudiana Aprili 27 kuanzia Saa 10:00 jioni pia Uwanja wa Moses Mabhida Jijini Durban, Afrika Kusini na mshindi wa jumla atakutana na mshindi wa jumla Kati ya RSB Berkane ya Morocco na CS Constantine ya Algeria katika Fainali.

AZAM FC YATOKA NYUMA NA KUICHAPA KAGERA SUGAR 4-2 KAITABA

Image
TIMU ya Azam FC imetoka nyuma na kushinda mabao 4-2 dhidi ya wenyeji, Kagera Sugar katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara usiku huu Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba. Mabao ya Azam FC yamefungwa na beki Lusajo Elukaga Mwaikenda dakika ya 42, winga Iddi Suleiman Ally  'Nado' dakika ya 58, kiungo Nassor Yahya Kapama aliyejifunga dakika ya 83 na mshambuliaji Mcolombia, Jhonier Alfonso Blanco Yus dakika ya 87. Kwa upande wa wenyeji, Kagera Sugar walipata mabao yao kupitia kwa wachezaji wa nafasi ya kiungo Hija Shamte Lidah dakika ya na 26 na Kassim Ibrahim Feka dakika ya 61. Kwa ushindi huo, Azam FC inafikisha pointi 54 na kurejea nafasi ya tatu ikiizidi pointi moja Singida Black Stars baada ya wote kucheza mechi 27, wakati Kagera Sugar inabaki na pointi zake 22 za mechi 27 pia nafasi ya 15.

SINGIDA BLACK STARS YAICHAPA TABORA UNITED 3-0 LITI

Image
WENYEJI, Singida Black Stars wameibuka na ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Tabora United katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara leo Uwanja wa CCM LITI mjini Singida. Mabao ya Singida Black Stars yamefungwa na kiungo mshambuliaji wa Kimataifa wa Niger, Victorien Adebayor Zakari Adje dakika ya 21 na mshambuliaji Mghana, Jonathan Sowah, mawili dakika ya 52 kwa penalti na 86. Kwa ushindi huo, Singida Black Stars inafikisha pointi 53 katika mchezo wa 27 na kusogea nafasi ya pili, ikiizidi pointi mbili Azam FC ambayo hata hivyo ina mechi moja mkononi na muda huu wapo Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba wanacheza na wenyeji, Kagera Sugar. Kwa upande wao Tabora United pamoja na kupoteza mchezo wa leo wanabaki nafasi ya tano na pointi zao 37 wakiizidi pointi tatu Dodoma Jiji FC baada ya timu zote kucheza mechi 27.

AHMED ALLY ATOKA SALAMA, ALLY KAMWE APIGWA NA ONYO KALI

Image
AFISA habari wa Yanga, Ally Shaaban Kamwe ametozwa Faini ya Sh. Milioni 5 na kupewa onyo la kutorudia kosa la Kimaadili ndani ya miaka miwili kuanzia Aprili 16, mwaka huu (2025). Naye Afisa Habari wa Simba SC, Ahmed Ally hajakutwa na hatia juu ya makaosa ya Kimaadili yaliyowasilishwa mbele ya Kamati ya Maadilia ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kutokana na kukosekana ushahidi wa kutosha. Viongozi kadhaa wamechukuliwa hatua todauti kwa makosa ya Kimaadili yaliyowasilishwa mbele ya Kamati hiyo, pigo kubwa likienda kwa aliyekuwa Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Soka Temeke (TEFA),   Salehe Mohamed Salehe na waliokuwa Makamu Mwenyekiti Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Shufaa Jumanne Nyamlani ambao wamefungiwa maisha kujihusisha na Soka. 

KMC YAILAZA DODOMA JIJI 2-1 MWENGE

Image
WENYEJI, KMC wameibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Dodoma Jiji katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara leo Uwanja wa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni, KMC Complex, Mwenge, Dar es Salaam. Mabao ya KMC yamefungwa na Abdallah Said dakika ya sita na Rashid Chambo dakika ya 28 — na la Dodoma Jiji limefungwa na Iddi Kipagwile dakika ya 39. Kwa ushindi huo, KMC inafikisha pointi 30 katika mchezo wa 26 na kusogea nafasi ya tisa, wakati Dodoma Jiji inabaki na pointi zake 34 za mechi 27 nafasi y sita.

TANZANIA PRISONS YAICHAPA JKT TANZANIA 3-2 SOKOINE

Image
WENYEJI, Tanzania Prisons wameibuka na ushindi wa mabao 3-2 dhidi ya JKT Tanzania katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa Sokoine Jijini Mbeya. Mabao ya Tanzania Prisons yamefungwa na Oscar Mwajanga mawili, dakika ya 51 na 90 na Jeremiah Juma dakika ya 78, wakati ya JKT Tanzania yamefungwa na Mohamed Bakari dakika ya 12 na Jumanne Elfadhili aliyejifunga dakika ya 42. Kwa ushindi huo, Tanzania Prisons inafikisha pointi 27 katika mchezo wa 27, ingawa wanabaki nafasi ya 14, wakati JKT Tanzania inabaki na pointi zake 32 za mechi 26 nafasi ya saba. Ligi Kuu inashirikisha timu 16 na mwisho wa msimu mbili zitashuka Daraja na mbili nyingine zitakazomaliza nafasi ya 14 na 13 zitamenyana baina yao na mshindi wa jumla atasalia Ligi Kuu. Timu itakayofungwa itakwenda kumenyana na timu ya Championship kujaribu tena kubaki Ligi Kuu. 

BILIONEA RWEGASIRA ASHINDA TENDA YA JEZI NA KUAHIDI KUIJENGEA SIMBA SC UWANJA

Image
KAMPUNI ya Jayrutty Investment Limited imeahidi kuijenga klabu ya Simba Uwanja wa kisasa wenye uwezo wa kuingiza mashabiki 10,000.  Ahadi hiyo imetolewa na Mwanzilishi na Mwenyekiti wa Jayrutty Investment Company Limited, CPA Joseph Rwegasira baada ya Kampuni yake kutambulishwa ndiyo mshindi wa Tenda ya Usambazaji jezi za klabu hiyo kwa mkataba wa miaka mitano wenye thamani ya Sh. Bilioni 38.1 (Sh. 8,120,400,000). “Jambo la kwanza ambalo tunakwenda kutekeleza ni kujenga Uwanja wa mpira, Uwanja ambao utachukua mashabiki 10,000 hadi 12,000 na tumekubaliana kwamba Simba wana Uwanja Bunju na tutakwenda kujenga Uwanja Bunju, lakini kama watakuja na mapendekezo mengine basi tutayafuata,” amesema CPA Joseph Rwegasira.  Pamoja na hayo, CPA Joseph Rwegasira watainunulia Simba basi jipya aina ya Irizar, ambalo litaonekana hivi karibuni huku pia akisema watajenga chombo kikubwa cha habari kitakachokwenda sambamba na vymbo vya klabu nyingine kubwa. “Tunajua kwamba Simba makao makuu...

YANGA NA KVZ, AZAM NA KMKM ROBO FAINALI KOMBE LA MAPINDUZI

Image
VIGOGO, Yanga watamenyana na wenyeji, KVZ katika mchezo wa Robo Fainali ya Kombe la Muungano Aprili 25 kuanzia Saa 2:15 usiku Uwanja wa New Amaan Complex, Zanzibar. Robo Fainali nyingine ya michuano hiyo itazikutanisha wenyeji, JKU na Singida Back Stars Aprili 23, wenyeji, Zimamoto na Coastal Union Saa 10:15 na wenyeji wengine, KMKM dhidi ya Azam FC kuanzia Saa 2:15 usiku Aprili 24 Uwanja wa New Amaan Complex pia. Nusu Fainali zitafuatia Aprili 27 na 28, wakati Fainali itachezwa Aprili 30 hapo hapo Uwanja wa New Amaan Complex. Mabingwa watetezi, Simba wameshindwa kushiriki michuano ya mwaka huu kwa sababu wanakabiliwa na mechi za Nusu Fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Stellenbosch ya Afrika Kusini Aprili 20 nyumbani na Aprili 27 marudiano ugenini. Simba SC ilitwaa michuano hiyo iliyoanza mwaka jana kuzimisha sherehe za Muungano wa Tanganyika na Zanzibar kwa ushindi wa 1-0 dhidi ya Azam FC katika Fainali Uwanja wa New Amaan Complex. Bao pekee la Simba lilifungwa ...

YANGA NA JKT TANGA, SIMBA NA SINGIDA MANYARA MEI 16

Image
MABINGWA watetezi, Yanga SC watasafiri hadi Tanga kwa ajili ya mchezo wa Nusu Fainali ya Kombe la Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) dhidi ya JKT Tanzania kati ya Mei 16 na Mei 18 Uwanja wa Mkwakwani. Nusu Fainali nyingine ya michuano hiyo iliyo katika mwaka wa pili wa udhamini wa Benki ya CRDB itazikutanisha Simba na Singida Black Stars Uwanja wa Tanzanite Kwaraa, Babati mkoani Manyara. Yanga walitinga Nusu Fainali kwa ushindi wa mabao 8-1 dhidi ya Stand United jana Uwanja wa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni, KMC Complex, Mwenge, Dar es Salaam. Kwa upande wao JKT Tanzania iliitoa Pamba Jiji FC ya Mwanza juzi kwa kuichapa mabao 3-1 Uwanja wa Meja Jenerali Charles Isamuhyo, Mbweni Jijini Dar es Salaam. Simba SC  ilifungua milango ya Nusu Fainali kwa kuitupa nje Mbeya City kwa kuichapa mabao 3-1  Jumapili Uwanja wa KMC na Singida Black Stars iliitoa Kagera Sugar kwa kuifunga mabao 2-0 Uwanja wa CCM LITI mjini Singida juzi. 

YANGA SC 8-1 STAND UNITED (KOMBE LA TFF)

Image
 

AZIZ KI WA MOTO, CHAMA AMEWAKA YANGA YAITANDIKA STAND UNITED 8-1 MWENGE

Image
MABINGWA watetezi, Yanga SC wamefanikiwa kuingia Nusu Fainali ya Kombe la Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), michuano inayodhaminiwa na Benki ya CRDB baada ya ushindi wa mabao 8-1 dhidi ya Stand United jioni ya leo Uwanja wa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni, KMC Complex, Mwenge, Dar es Salaam. Nyota wa mchezo wa leo ni kiungo mshambuliaji wa Kimataifa wa Burkina Faso aliyehusika kwenye mabao saba kwa kusaidia upatikanaji mabao matatu na yeye mwenyewe kufunga manne. Alifunga mabao yake dakika za 10,48, 58 na 61 huku pia akiwasetia beki Nickson Kibabage kufunga dakika ya 20 na kiungo Mzambia, Clatous Chama mawili, dakika ya 32 na 40. Bao la nane la Yanga liliparikana kwa ushirika wa wachezaji waliotokea benchi, mshambuliaji Mzambia - Kennedy Musonda akifunga kwa kumalizia krosi ya kiungo Farid Mussa, huku bao pekee la Stand United likifungwa na Msenda Senda dakika ya 48. Yanga sasa itakutana na JKT Tanzania ambayo jana iliitoa Pamba Jiji FC ya Mwanza kwa kuichapa mabao 3-1 Uwanja ...

NI SINGIDA BLACK STARS NA SIMBA NUSU FAINALI KOMBE LA CRDB

Image
TIMU ya Singida Black Stars imefanikiwa kuingia Nusu Fainali ya Kombe la Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), michuano inayodhaminiwa na Benki ya CRDB baada ya ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Kagera Sugar jioni ya leo Uwanja wa CCM LITI mjini Singida. Mabao ya Singida Black Stars yamefungwa na kiungo mshambuliaji wa Kimataifa wa Niger,  Adebayor Zakari Victorien Adje dakika ya 11 na mshambuliaji Mghana, Jonathan Sowah dakika ya 66. Kwa ushindi huo Singida Black Stars itakutana na Simba SC katika Nusu Fainali ambayo iliitoa Mbeya City jana kwa kuichapa mabao 3-1 Uwanja wa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni, KMC Complex, Mwenge, Dar es Salaam.

SIMBA SC NA STELLENBOSCH KUPIGWA UWANJA WA AMAAN JUMAPILI

Image
MCHEZO wa kwanza wa Nusu Fainali Kombe la Shirikisho Afrika baina ya wenyeji, Simba SC na Stellenbosch ya Afrika Kusini utapigwa Uwanja wa New Amaan Complex Jumapili ya Aprili 27 kuanzia Saa 10:00 jioni. Simba SC wamelazimika kuupeleka mchezo huo Zanzibar kufuatia Serikali kufunga Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam kwa ukarabati. Stellenbosch imefika hatua hii baada ya kuwatoa waliokuwa mabingwa watetezi, Zamalek kwa kuwachapa 1-0 Aprili 9, bao la kiungo Sihle Nduli Uwanja wa Cairo International Jijini Cairo  kufuatia kutoka suluhu kwenye mchezo wa kwanza Aprili 2 pia Uwanja wa DHL Cape Town Jijini Cape Town. Simba SC ilifika Nusu Fainali ya michuano hiyo kwa kuitoa Al Masry ya Misri pia kwa penalti 4-1 kufuatia sare ya jumla ya 2-2 baada ya kila timu kushinda 2-0 nyumbani. Al Masry ilianza kushinda 2-0 pia kwenye mchezo wa kwanza Aprili 2 mabao ya washambuliaji Mualgeria, Abderrahim Deghmoum dakika ya 16 na Mnigeria, John Okoye Ebuka dakika ya 89 Uwanja wa New Su...

YANGA KUJENGA UWANJA WAKE MWAKANI KWA MSAADA WA SERIKALI

Image
RAIS wa klabu ya Yanga, Hersi Ally Said amesema kwamba mwaka ujao watajenga Uwanja wao kwa msaada wa Serikali. Akizungumza kwenye Mkutano wa Viongozi wa Klabu Duniani ulioandaliwa na Taasisi ya World Football Summit (WFS) Jijini Rabat nchini Morocco, Hersi amesema kwamba klabu za Afrika zinakabiliwa na changamoto kubwa ya miundombimu ikiwemo ukosefu wa viwanja vyao wenyewe. Afrika tuna changamoto nyingi, mojawapo tumeitaja ni miundombinu . Tumeona Ulaya klabu nyingi zinamiliki miundombinu, ikiwemo vifaa vya mazoezi, vituo vya mafunzo, pamoja na viwanja vya kuchezea mechi, ambayo ni tofauti na klabu nyingi za Afrika,” amesema Hersi ambaye pia Mwenyekiti wa Chama cha Klabu Afrika (ACA). Ameongeza kwamba huwezi kuinua kipaji cha mchezaji kuwa cha kiwango bora bila ya kuwa na miundombinu na kuzipongeza baadhi ya klabu barani zenye miundombinu bora zikiwemo Al Ahly ya Misri. “Kwa mfano klabu yangu, Yanga ni moja ya klabu kubwa ya umri wa miaka 90, lakini kusema ukweli hatuna Uwanja ...

SIMBA SC 3-1 MBEYA CITY (KOMBE LA TFF)

Image
 

SIMBA YATINGA NUSU FAINALI KOMBE LA CRDB, YAICHAPA MBEYA CITY 3-1

Image
TIMU ya Simba SC imefanikiwa kwenda Nusu Fainali ya Kombe la Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), michuano inayodhaminiwa na Benki ya CRDB baada ya ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Mbeya City leo Uwanja wa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni, KMC Complex, Mwenge, Dar es Salaam.   Mabao ya Simba SC yamefungwa na kiungo Mkongo, Fabrice Luamba Ngoma dakika ya 24, mshambuliaji Mcameroon, Christian Leonel Ateba Mbida dakika ya 30 na winga Mzambia, Joshua Mutale Budo dakika ya 43 baada ya kiungo Mudathir Said Khamis kuanza kuifungia Mbeya City dakika ya 22. Kwa ushindi huo, Simba itakutana na mshindi kati ya Singida Black Stars na Kagera Sugar zinazotarajiwa kumenyana kesho Uwanja wa CCM LITI mjini Singida. Nusu Fainali nyingine ya Kombe la CRDB itapigwa kesho baina ya JKT Tanzania na Pamba Jiji Uwanja wa Meja Jenerali Charles Isamuhyo, Mbweni, Dar es Salaam - wakati keshokutwa hatua hiyo itakamilishwa kwa mabingwa watetezi, Yanga kumenyana na Stand United Uwanja wa KMC ...