Posts

Showing posts from December, 2024

YANGA SC 5-0 FONTAIN GATE (LIGI KUU YA NBC TZ BARA)

Image
 

COASTAL UNION YAAMBULIA SARE KWA KMC, 1-1 ARUSHA

Image
WENYEJI, Coastal Union wametoka sare ya kufungana bao 1-1 na KMC FC katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa Sheikh Amri Abeid Jijini Arusha. KMC walitangulia kwa bao la mapema tu dakika ya kwanza, kabla ya Maulid Juma kuisawazishia Coastal Union kwa penalti dakika ya 89. Kwa matokeo hayo, Coastal Union inafikisha pointi 18, ingawa inabaki nafasi ya 11 ikizidiwa pointi moja na KMC baada ya wote kucheza mechi 16 sasa.

PACOME AFUNGA MAWILI YANGA YAICHAPA FOUNTAIN GATE 5-0

Image
MABINGWA watetezi, Yanga wameibuka na ushindi wa mabao 5-0 dhidi ya Fountain Gate katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni, KMC Complex, Mwenge Jijini Dar es Salaam. Mabao ya Yanga leo yamefungwa na  viungo Muivory Coast, Pacome Zouzoua Peodoh mawili, dakika ya 16 na 45’+1, Mudathir Yahya Abbas dakika ya 41, beki Jackson Katanga Shiga aliyejifunga dakika ya 52 na mshambuliaji Clement Francis Mzize dakika ya 88. Kwa ushindi huo, Yanga inafikisha pointi 39 ikikamilisha mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu, ingawa inabaki nafasi ya pili nyuma ya Simba yenye pointi 40 baada ya wote kucheza mechi 15. Fountain Gate baada ya kupoteza mchezo wa leo inabaki na pointi zake 20 za mechi 16 sasa, japokuwa inaendelea kubaki nafasi ya sita.

M-BET, HALOPESA WAANZA KUMWAGA ZAWADI ZA WASHINDI WA KAMPENI YA AMSHA AMSHA

Image
KAMPUNI  ya michezo ya kubashiri ya M-Bet kwa kushirikiana na kampuni ya simu ya Halotel kupitia HaloPesa zimezawadia washindi wa kwanza wa kampeni ya Amsha Amsha zawadi mbalimbali. Meneja Masoko wa M-Bet, Levis Paul amewataja washindi hao kuwa ni Ramadhan Mussa wa Dodoma na Greta Godfrey wa Dar es Salaam ambao wameshinda simu janja za mkononi aina ya Samsung A-series zenye thamani ya Sh500,000  kila mmoja. Mbali ya zawadi za simu za mkononi, pia mkazi wa Songea, Vedasto Augustino ameshinda  televisheni aina ya Hisense yenye thamani ya Sh1.2 millioni. Mwakilishi wa kampuni ya simu ya Halotel, Keneth Bernald Wello (kulia) akimkabidhi zawadi ya televisheni aina ya Hisense yenye thamani ya Sh1.2 millioni Vedasto Agustino ambaye ameshinda kupitia kampeni ya Amsha Amsha. Washindi wote wamekwisha patiwa zawadi zao ambapo, wakazi wa Dodoma na Songea wametumiwa kupitia utaratibu waliouweka. Pia, Daniel Dende, Njelekela Vitass, Petro Edward, Manase Ernest, Paschaa...

DODOMA JIJI FC YAIKUNG’UTA MASHUJAA 3-1 JAMHURI

Image
WENYEJI, Dodoma Jiji wameibuka na ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Mashujaa FC katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara usiku wa leo Uwanja wa Jamhuri Jijini Dodoma. Mabao ya Dodoma Jiji FC yamefungwa na Mwana David Kibuta dakika ya 12, Lulihoshi Heritier dakika ya 16 na Zidane Sereri dakika ya 83, wakati la Mashujaa limefungwa na Crispin Ngushi dakika ya 90 na ushei. Kwa ushindi huo, Dodoma Jiji FC inafikisha pointi 19 na kusogea nafasi ya tisa, ikizidiwa tu wastani wa mabao na Mashujaa na JKT Tanzania baada ya wote kucheza mechi 16.

SIMBA SC YAENDELEZA WIMBI LA USHINDI LIGI KUU, YAICHAPA SINGIDA 1-0 LITI

Image
TIMU ya Simba SC imeibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya wenyeji, Singida Black Stars katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara leo Uwanja wa CCM LITI mjini Singida. Bao la Wekundu wa Msimbazi limefungwa na kiungo kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), Fabrice Luamba Ngoma dakika ya 42 akimalizia kona ya kiungo Muivory Coast, Jean Chjarles Ahoua kutoka upande wa kulia wa Uwanja. Kwa ushindi huo, Simba SC wanakamilisha mechi zao 15 za mzunguko wa Ligi Kuu wakiwa na  pointi 40 na kuendelea kuongoza mbele ya mabingwa watetezi, Yanga SC wenye pointi 36 za mechi 14, wakiwazidi wastani wa mabao tu Azam FC. Singida Black Stars baada ya kichapo cha leo wanabaki na pointi zao 33 za mechi 16 sasa nafasi ya nne, mbele ya jirani zao Tabora United wenye pointi 25 za mechi 15.

SERENGTI BOYS YACHAPWA 2-1, UGANDA NDIO MABINGWA CECAFA U17

Image
WENYEJI, Uganda wamefanikiwa kutwaa ubingwa wa Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati kwa vijana chini ya umri wa miaka 17 (CECAFA U17) baada ya kuichapa Tanzania mabao 2-1 leo Uwanja wa Hamz, Nakivubo Jijini Kampala. Tanzania waliuanza vyema mchezo huo na kupata bao la kuongoza mapema kipindi cha kwanza kupitia kwa Abel Josiah, kabla ya Uganda kuzinduka kipindi cha pili na kufunga mabao mawili kupitia kwa Arafat Nkoola na James Bogere. Uganda na Tanzania wote wamefuzu Fainali za Afrika, AFCON U17 ambazo zitafanyika mwakani nchini Morocco.  

TANZANIA PRISONS YAICHAPA PAMBA JIJI 1-0 UWANJA WA SOKOINE

Image
TIMU ya Tanzania Prisons imeibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Pamba Jiji ya Mwanza katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa Sokoine Jijini Mbeya. Pongezi kwa mfungaji wa bao hilo pekee, kiungo Tariq Abdallah Simba aliyefumua shuti la umbali wa mita 17 kumtungua kipa wa zamani wa Tanzania Prisons, Yona Geoffrey Amos dakika ya 31. Kwa ushindi huo, Tanzania Prisons wanafikisha pointi 14 na kujiinua hadi nafasi ya 13, ikiishushia Pamba Jiji nafasi ya 14 baada ya wote kucheza mechi 16. 

DODOMA JIJI 0-4 YANGA SC (LIGI KUU YA NBC TZ BARA)

Image
 

MZIZE AWEKA MBILI NYAVUNI YANGA YAICHAPA DODOMA JIJI 4-0 JAMHURI

Image
MABINGWA watetezi, Yanga wameendeleza wimbi la ushindi katika Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara baada ya kuwachapa wenyeji, Dodoma Jiji mabao 4-0 katika jioni ya leo Uwanja wa Jamhuri Jijini Dodoma. Mabao ya Yanga leo yamefungwa na mshambuliaji mzawa, Clement Francis Mzize mawili, dakika ya 19 na 38, kiungo Mburkinabe Stephane Aziz Ki dakika ya 29 na mshamabuliaji Mzimbabwe, Prince Dube Mpumelelo dakika ya 63. Kwa ushindi huo, Yanga SC inafikisha pointi 36, ingawa inabaki nafasi ya pili ikizidiwa pointi moja na watani wa jadi, Simba SC baada ya wote kucheza mechi 14, wakati Dodoma Jiji inabaki na pointi zake 16 za mechi 15 nafasi ya 11.

NAMUNGO FC YAICHAPA FOUNTAIN GATE 2-1 PALE PALE BABATI

Image
TIMU ya Namungo FC imeibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya wenyeji, Fountain Gate katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara Uwanja wa Tanzanite Kwaraa mjini Babati mkoani Manyara. Mabao ya Namungo FC yamefungwa na viungo Pius Charles Buswita dakika ya 10 na Geoffrey Julius Luzendaze dakika ya 78, wakati bao pekee la Fountain Gate limefungwa na winga Salum Kihimbwa dakika ya 30. Kwa ushindi huo, Namungo FC inafikisha pointi 17 katika mchezo wa 16 na kusogea nafasi ya 11, wakati Fountain Gate wanabaki na pointi zao 20 za mechi 15 sasa nafasi ya sita.  

SIMBA SC 1-0 JKT TANZANIA (LIGI KUU YA NBC TZ BARA)

Image
 

SIMBA SC YAJITANUA KILELENI LIGI KUU, YAICHAPA JKT TANZANIA 1-0 MWENGE

Image
TIMU ya Simba SC imeendeleza wimbi la ushindi katika Ligi Kuu ya Tanzania Bara baada ya ushindi wa bao 1-0 dhidi ya JKT Tanzania leo Uwanja wa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni, KMC Complex, Mwenge Jijini Dar es Salaam. Lilikuwa ni bao la dakika ya 90 na ushei la mkwaju wa penalti wa Kiungo Muivory Coast, Jean Charles Ahoua aliyemchambua kipa Yacoub Suleiman wa JKT Tanzania baada ya beki Mohamed Bakari kumchezea rafu Shomari Kapombe kwenye boksi. JKT Tanzania ikamaliza mechi pungufu ya mchezaji mmoja baada ya Refa Kayombo Kefa wa Mbeya kumtoa kwa kadi nyekundu Mohamed Bakari kufuatia kumuonyesha kadi ya pili ya njano alipomchezea rafu Shomari Kapombe. Kwa ushindi huo, Simba inafikisha pointi 37 katika mchezo wa 14 na kuendelea kuongoza Ligi Kuu, mbele ya mabingwa watetezi, Yanga wenye pointi 33 za mechi 13, wakati JKT Tanzania inabaki na pointi zake 19 za mechi 15 sasa nafasi ya nane kwenye ligi ya timu 16.

SINGIDA BLACK STARS YAICHIMBIA KABURI KENGOLD, YAICHAPA 2-1 LITI

Image
WENYEJI, Singida Black Stars wametoka nyuman na kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Kengold FC katika mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara leo Uwanja wa CCM LITI mjini Singida. Kengold ilitangulia kwa bao la Hubert la winga Herbet Charles Lukindo dakika ya 25, kabla ya kiungo Muivory Coast, Josaphat Arthur Bada kuisawazishia Singida Black Stars dakika ya 46 na mshambuliaji Mkenya, Elvis Baranga Rupia kufunga la ushindi dakika ya 55. Kwa ushindi huo, Singida Black Stars wanafikisha pointi 33 katika mchezo wa 15, ingawa wanabaki nafasi ya nne, wakati Kengold wanaendelea kushika mkia kwenye ligi ya timu 16 wakibaki na pointi zao sita za mechi 16 sasa.

ZUBERI FOBA MASUDI AONGEZA MKATABA AZAM FC HADI 2027

Image
KLABU ya Azam imemuongeza mkataba wa miaka miwili kipa wake wa pili, Zuberi Foba Masudi ambao utamfanya aendelee kuitumikia timu ya Bilionea Alhaj Sheikh Salim Bakhresa na familia yake hadi mwaka 2027. “Kipa wetu @foba_zubeir, ataendelea kusalia kwenye viunga vya Azam Complex hadi mwaka 2027 baada ya kuongeza mkataba mpya wa miaka miwili,”umesema taarifa ya Azam FC leo. Licha ya kuwa kipa wa pili nyuma ya Mustafa Mohamed wa Sudan, lakini Foba amekuwa na mwendelezo mzuri msimu huu akiwa amedaka mechi tano za mashindano yote bila kuruhusu bao hata moja.

YANGA SC 4-0 TANZANIA PRISONS (LIGI KUU YA NBC TZ BARA )

Image
 

YANGA SC YAICHAPA TANZANIA PRISONS 4-0 MWENGE

Image
MABINGWA watetezi, Yanga SC wameibuka na ushindi wa mabao 4-0 dhidi ya Tanzania Prisons katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni, KMC Complex, Mwenge Jijini Dar es Salaam. Mabao ya Yanga leo yamefungwa na wazawa, mshambuliaji Clement Francis Mzize dakika ya 13, beki Ibrahim Hamad Abdullah ‘Bacca’ mawili dakika ya 42 na 83 na mshambuliaji Mzimbabwe, Prince Dube Mpumelelo dakika ya 45. Kwa matokeo hayo, Yanga inafikisha pointi 33 katika mchezo wa 13 na kusogea nafasi ya pili, ikiizidi tu wastani wa mabao Azam FC ambayo pia imecheza mechi mbili zaidi. Wote wapo nyuma ya Simba SC yenye pointi 34 za mechi 13 pia, wakati Tanzania Prisons inabaki na pointi zake 11 za mechi 15 sasa nafasi ya 14 kwenye ligi ya timu 16, ambayo mwisho wa msimu mbili zitateremka daraja.

KAGERA SUGAR 2-5 SIMBA SC (LIGI KUU YA NBC TZ BARA)

Image
 

MUKWALA APIGA MBILI SIMBA YAICHAPA KAGERA SUGAR 5-2 BUKOBA

Image
TIMU ya Simba SC imeibuka na ushindi wa mabao 5-2 dhidi ya wenyeji, Kagera Sugar katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba mkoani Kagera. Mabao ya Simba SC yamefungwa na beki Shomari Salum Kapombe dakika ya 13, viungo Muivory Coast Jean Charles Ahoua dakika ya 44, Mkongo Fabrice Luamba Ngoma dakika ya 53 na mshambuliaji Mganda, Steve Dese Mukwala mawili, dakika ya 66 na 85. Kagera Sugar ilipata mabao yake ya kufutia machozi mwishoni mwa mchezo, wakifunga beki Datius Peter dakika ya 79 na kiungo Cleophas Anthony Mkandala dakika ya 90’+3. Kwa ushindi huo, Simba SC inayofundishwa na Kocha Rais wa Afrika Kusini, Fadlu Davids inafikisha pointi 34 katika mchezo wa 13 na kurejea kileleni mwa Ligi Kuu mbele ya Azam FC yenye pointi 33 za mechi 15 na mabingwa watetezi, Yanga wenye pointi 30 za mechi 12. Kwa upande wao Kagera Sugar baada ya kupoteza mchezo wa leo wanabaki na pointi zao 11 za mechi 15 nafasi ya 15 kwenye ligi ya timu 16, ambayo mwisho wa ...

NAMUNGO FC YAAMBULIA SULUHU KWA JKT TANZANIA RUANGWA

Image
WENYEJI, Namungo FC wamelazimishwa sare ya bila mabao na JKT Tanzania katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara usiku huu Uwanja wa Majaliwa, Ruangwa mkoani Lindi. Kwa matokeo hayo, JKT Tanzania inafikisha pointi 19 katika mchezo wa 14, ingawa inabaki nafasi ya nane, wakati Namungo FC inakamilisha mechi 15 za mzunguko wa kwanza Ligi ya timu 16 ukiwa nafasi ya 13 kwa pointi zake 14.

KOCHA MOROCCO AITA 30 KUUNDA ZANZIBAR HEROES YA KOMBE LA MAPINDUZI

Image
KOCHA Hemed Suleiman ‘Morocco’ ameita wachezaji 30 kuunda kikosi cha timu ya Taifa ya Zanzibar itakayoshiriki michuano ya Kombe la Mapinduzi inayotarajiwa kuanza Januari 3, mwakani. Makipa; Ahmed Ali Suleiman ‘Salula’ (Uhamiaji), Suleiman Said Abraham (KVZ FC), Yakoub Suleiman Ali (JKT Tanzania). Mabeki: Salum Khamisn Salum ‘Gado’ (JKT Tanzania), Abdallah Said Ali ‘Laso’ (KMC), Sued Juma Hussein ‘Aguero’ (JKU), Adeyum Saleh Ahmed (Geita Gold), Abdulhalim Abdallah Juma (Chipukizi United), Ibrahim Ame ‘Varane’ (Mashujaa), Abdulrahman Seif Bausi (JKT Tanzania), Abdallah Kheri ‘Sebo’ (Azam FC), Mukrim Issa Abdallah ‘Miranda’ (Coastal Union), Abdulmalik Adam Zakaria (Mashujaa), Laurian Omar Makame (Fountain Gate). Viungo: Khalid Habib Iddi (Singida Black Stars), Abdulaziz Makame ‘Bui’ (Geita Gold), Abdallah Yassin Kulandana (Fountain Gate FC), Hassan Nassor Maulid (JKT Tanzania), Suleiman Saleh Abdallah (KVZ FC), Feisal Salum Abdallah ‘Fei Toto’ (Azam FC), Hassan Haji Ali ‘Cheda’ (Mas...

YANGA SC 3-2 MASHUJAA FC (LIGI KUU YA NBC TZ BAEA)

Image
 

DUBE APIGA HAT TRICK YANGA YASHINDA 3-2 DHIDI YA MASHUJAA MWENGE

Image
MABINGWA watetezi, Yanga SC wameibuka na ushindi wa mabao 3-2 dhidi ya Mashujaa FC katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara leo Uwanja wa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni, KMC Complex, Mwenge Jijini Dar es Salaam. Nyota imemng’aria mshambuliaji wa Kimataifa wa Zimbabwe, Prince Dube Mpumelelo aliyefunga mabao yote matatu dakika za saba, 21 na 53, wakati mabao ya Mashujaa yamefungwa na David Ulomi dakika ya 45 na Idrisa Stambuli dakika ya 62. Kwa ushindi huo, Yanga inafikisha pointi 30 na kurejea nafasi ya tatu, ikizidiwa pointi moja na watani, Simba SC baada ya wote kucheza mechi 12 na wote wapo nyuma ya Azam FC yenye pointi 33 za mechi 15. Kwa upande wao Mashujaa baada ya kupoteza mchezo wa leo wanabaki na pointi zao 19 za mechi 15 sasa wakibaki nafasi ya saba.

SIMBA SC 2-0 KEN GOLD (LIGI KUU YA NBC TZ BARA)

Image
 

ATEBA APIGA ZOTE MBILI SIMBA SC YAICHAPA KEN GOLD 2-0 MWENGE

Image
TIMU ya Simba SC imeibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Ken Gold ya Mbeya  katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara baada ya   jioni ya leo Uwanja wa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni, KMC Complex, Mwenge Jijini Dar es Salaam. Mabao yote ya Simba SC leo yamefungwa na mshambuliaji wake Mcameroon, Christian Leonel Ateba Mbida dakika ya 34 kwa penalti na dakika ya 44 akimalizia kazi nzuri ya beki Mburkinabe, Valentin Nouma. Kwa ushindi huo, Simba inayofundishwa kocha raia wa Afrika Kusini Fadlu Davids inafikisha pointi 31 katika mchezo wa 12, ingawa inabaki nafasi ya pili, ikizidiwa pointi mbili na Azam FC, ambayo pia imecheza mechi tatu zaidi. Kwa upande wao Ken Gold walio chini ya Kocha Omar Kapilima hali inazidi kuwa mbaya wakikamilisha mechi 15 za mzunguko wa kwanza mkiani, wakibaki na pointi zao sita.

VINICIUS MWANASOKA BORA WA MWAKA WA FIFA, ANCELOTTI KOCHA BORA

Image
MSHAMBULIAJI wa Kimataifa wa Brazil na klabu ya Real Madrid ya Hispania, Vinícius Junior ameshinda Tuzo ya Mwanasoka Bora wa Mwaka ya 2024 ambayo alikabidhiwa na Rais wa Shirikisho hilo la Soka la Kimataifa, Gianni Infantino katika hafla iliyofanyika Jijini Doha nchini Qatar usiku wa jana. Naye kiungo wa Kimataifa wa Hispania na klabu ya Barcelona, Aitana Bonmatí ameshinda Tuzo ya Mwanasoka Bora wa Kike wa Mwak aya FIFA kwa mara ya pili mfululizo. Ukawa usiku mzuri pia kwa Mtaliano, Carlo Ancelotti aliyeshinda Tuzo ya Kocha Bora wa Kiume na kukabidhiwa na Kocha wa zamani wa Arsenal, Arsene Wenger. WASHINDI WOTE WA TUZO ZA FIFA 2024: • Mchezaji Bora wa Kike – Aitana Bonmatí • Mchezaji Bora wa Kiume – Vinícius Junior • Kipa Bora wa Kike – Alyssa Naeher • Kipa Bora wa Kiume – Emiliano Martínez • Kocha Bora wa Kike – Emma Hayes • Kocha Bora wa Kiume – Carlo Ancelotti • Tuzo ya Marta – Marta • Tuzo ya Puskas - Alejandro Garnacho KIKOSI BORA CHA WACHEZAJI 11:  Emiliano Ma...

AZAM FC WAIPIGA FOUNTAIN GATE 2-0 NA KUJITANUA KILELENI LIGI KUU

Image
WENYEJI, Azam FC wametanua mbawa kileleni mwa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara baada ya ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Fountain Gate katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara leo Uwanja wa Azam Complex, Chamazi Jijini Dar es Salaam. Mabao ya Azam FC yamefungwa na winga Mgambia, Gibril Sillah dakika ya 31 na mshambuliaji Msenegal, Alassane Diao dakika ya 90’+1 na kwa ushindi huo wanafikisha pointi 33 katika mchezo wa 15 na kuendelea kuongoza Ligi Kuu. Azam FC ipo mbele ya Singida Black Stars inayofuatia kwa pointi zake 30 za mechi 14, Simba SC pointi 28 na mabingwa watetezi, Yanga pointi 27 baada ya wote kucheza mechi 11. Kwa upande wao Fountain Gate baada ya kupoteza mechi ya leo wanabaki na pointi zao 20 kufuatia kucheza mechi 14 na wanabaki nafasi ya sita.

TABORA UNITED YAAMBULIA SARE KWA COASTAL UNION, 1-1 ‘KWA MWINYI’

Image
WENYEJI, Tabora United wamepunguzwa kasi baada ya kutoa sare ya kufungana bao 1-1 na Coastal Union katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi mjini Tabora. Costal Union ilitangulia kwa bao la Jeremier Ntabwe dakika ya Dk 45’+2, kabla ya Banele Junior kuisawazishia Tabora United dakika ya 56. Kwa matokeo hayo, Tabora United inafikisha pointi 25, ingawa inabaki nafasi ya tano na Coastal Union inafikisha pointi 17, nayo inabaki nafasi ya 10 kwenye ligi ya timu 16.

ADEMOLA LOOKMAN NA BABRA BANDA NDIO WANASOKA BORA AFRIKA 2024

Image
MSHAMBULIAJI wa Atalanta ya Italia, Mnigeria, Ademola Lookman ameshinda Tuzo ya Mwanasoka Bora wa Mwaka Afrika kwa wanaume. Lookman amewaangusha Ronwen Williams, kipa Muafrika Kusini wa Mamelodi Sundowns, mshambuliaji, Serhou Guirassy wa Guinea na Borussia Dortmund, Simon Adingra wa Ivory Coast na Brighton & Hove Albion na beki Achraf Hakimi wa Morocco na Paris Saint-Germain. Anakuwa Mnigeria wa pili mfululizo kushinda Tuzo hiyo baada  Victor James Osimhen anayecheza kwa mkopo Galatasaray ya Uturuki kutoka Napoli ya Italia – hii ikiwa mara ya kwanza kwa nchi hiyo kubeba mtawalia Tuzo hiyo tangu kupokezana kwa Nwankwo Kanu (1996) na Victor Ikpeba (1997), karibu miongo mitatu sasa imepita. Naye mshambuliaji Mzambia, Barbra Banda anayechezea klabu ya Orlando Pride ya Marekani ameshinda Tuzo ya Mwanasioka Bora wa Kike Afrika dhidi ya ndugu wawili wa Malawi, Tabitha na Temwa Chawinga, Sanaa Mssoudy wa Morocco, Chiamaka Nnadozie wa Nigeria.  WASHINDI WOTE TUZO ZA CAF 2024...

KMC YAICHAPA PAMBA 1-0 BAO LA HANCE DAKIKA ZA JIOONII

Image
BAO la dakika ya 88 la beki Hance Masoud Msonga limeipa KMC ushindi wa 1-0 dhidi ya Pamba Jiji katika mchezo wa  Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara Uwanja wa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni, KMC Complex, Mwenge Jijini Dar es Salaam. Kwa ushindi huo, KMC inafikisha pointi 18 na kupanda kwa nafasi mbili hadi ya tisa, wakati Pamba Jiji inabaki na pointi zake 12 nafasi ya 13 baada ya wote kucheza mechi 14. NAYO Singida Black Stars imeibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya wenyeji, Tanzania Prisons katika mchezo mwingine wa Ligi Kuu ya leo Uwanja wa Sokoine Jijini Mbeya. Mabao ya Singida Black Stars yamefungwa na kiungo Mtogo, Marouf Tchakei dakika ya 48 na beki mzawa, Kennedy Wilson Juma dakika ya 62. Kwa ushindi huo, Singida Black Stars inafikisha pointi 30 na kupanda nafasi ya pili ikizidiwa tu wastani wa mabao na Azam FC baada ya wote kucheza mechi 14. Hali inazidi kuwa mbaya kwa Tanzania Prisons ikibaki na pointi zake 11 za mechi 14 na kushuka kwa nafasi moja zaidi hadi ya ...

SINGIDA BLACK STARS YAICHAPA TANZANIA PRISONS 2-0 SOKOINE

Image
TIMU ya Singida Black Stars imeibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya wenyeji, Tanzania Prisons katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara leo Uwanja wa Sokoine Jijini Mbeya. Mabao ya Singida Black Stars yamefungwa na kiungo Mtogo, Marouf Tchakei dakika ya 48 na beki mzawa, Kennedy Wilson Juma dakika ya 62. Kwa ushindi huo, Singida Black Stars inafikisha pointi 30 na kupanda nafasi ya pili ikizidiwa tu wastani wa mabao na Azam FC baada ya wote kucheza mechi 14. Hali inazidi kuwa mbaya kwa Tanzania Prisons ikibaki na pointi zake 11 za mechi 14 na kushuka kwa nafasi moja zaidi hadi ya 15 kwenye ligi ya timu 16.

KIBU DENNIS SHUJAA…SIMBA YAIKANDA SFAXIEN 2-1 ‘KWA MKAPA’

Image
WENYEJI, Simba SC wametoka nyuma na kushinda 2-1 dhidi ya CS Sfaxien ya Tunisia katika mchezo wa mwisho mzunguko wa kwanza Kundi A Kombe la Shirikisho Afrika leo Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam. Shujaa wa Simba SC leo ni kiungo mshambuliaji, Kibu Dennis Prosper aliyefunga mabao yote mawili, dakika ya saba akimalizia pasi ya kiungo Muivory Coast, Jean Charles Ahoua na dakika ya 90’+9 akimalizia pasi ya kiungo mzawa, Yusuph Ally Kagoma. Mshambuliaji Mtunisia, Hazem Haj Hassen alianza kuifungia CS Sfaxien dakika tatu akitumia makosa ya beki Mcameroon, Che Fondoh Malone Junior kumrejeshea pasi fupi kipa wake, Mguinea Moussa Camara akaunasa mpira njiani na kufunga. Kwa matokeo hayo, Simba SC inafikisha pointi sita katika mchezo wa tatu na kujiweka sawa nafasi ya pili ikizidiwa wastani wa mabao tu na vinara, CS Constantine ya Algeria ambao wamecheza mechi mbili na wote wapo mbele ya Bravos do Maquis ya Angola yenye poimto tatu. Mabingwa wa zamani wa Kombe la Shirikisho w...

NAMUNGO FC YATOKA NYUMA KWA MABAO MAWILI NA KUICHAPA KEN GOLD 3-2 SOKOINE

Image
TIMU ya Namungo FC imetoka nyuma kwa mabao mawili na kushinda 3-2 dhidi ya wenyeji, Ken Gold katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara leo Uwanja wa Sokoine Jijini Mbeya. Ken Gold walitangulia kwa mabao ya Mishamo Daudi dakika ya pili na Joshua Ibrahim dakika ya tisa, kabla ya Namungo kuzinduka kwa mabao ya mkongwe, Erasto Nyoni dakika ya 24 kwa penalti na 90’+3 na Fabrice Ngoy dakika ya 36. Kwa ushindi huo, Namungo FC inafikisha pointi 13 na kusogea nafasi ya 12 kutoka ya 15, wakati Ken Gold inaendelea kushika mkia kwenye ligi ya timu 16 ikibaki na pointi zake sita baada ya timu zote kucheza mechi 14.

YANGA YAOKOTA POINTI YA KWANZA LIGI YA MABINGWA, 1-1 NA MAZEMBE LUBUMBASHI

Image
BAO la dakika ya 90'+4 la mshambuliaji Mzimbabwe, Prince Dube Mpumelelo limeinusu Yanga kupoteza mechi ikipata sare ya 1-1 na wenyeji, Tout Puissant Mazembe katika mchezo wa mwisho wa mzunguko wa kwanza Kundi A Ligi ya Mabingwa Afrika Uwanja wa TP Mazembe Jijini Lubumbashi, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC). TP Mazembe walitangulia kwa bao la mshambuliaji kinda wa umri wa miaka 20, Cheick Oumar Abdallah Fofana dakika ya 41 akimfunga kipa raia mwenzake wa Mali, Djigui Diarra ambaye hakurejea kipindi cha pili nafasi yake ikichukuliwa Khomeiny Abubakar. Kwa matokeo hayo, Mazembe wanafikisha pointi mbili wakibaki nafasi ya tatu kwenye kundi hilo, wakati Yanga inayookota pointi ya kwanza leo inaendelea kushika mkia baada ya mechi tatu za awali - wote wakiwa nyuma ya Al Hilal Omdurman ya Sudan yenye pointi sita na MC Alger ya Algeria yenye pointi nne. Al Hilal Omdurman watakuwa wageni wa MC Alger kukamilisha mechi zao tatu za mzunguko wa kwanza kuanzia Saa 4:00 usiku wa leo Uw...

MAKAMBO AFUNGA MABAO MAWILI TABORA UNITED YAICHAPA AZAM FC 2-1

Image
WENYEJI, Tabora United wameibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Azam FC katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi mjini Tabora. Mabao yote ya Tabora United leo yamefungwa na mshambuliaji kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), Heritier Ma Olongi Makambo moja kila kipindi akimc hambua kipa namba moja wa timu ya taifa ya Sudan kwa kichwa dakika ya 37 na 68. Kwa upande wao, Azam FC bao lao pekee lilifungwa na beki wa Kimataifa wa Mali, Yoro Mamadou Diaby dakika ya 71 kwa kichwa akimtungua kipa Hussein Salum Masalanga 'Buffon'. Kwa ushindi huo, Tabora United wanafikisha pointi 24 katika mchezo wa 14, ingawa wanabaki nafasi ya tano wakizidiwa pointi tatu na Singida Black Stars ambao pia wana mechi moja mkononi. Pamoja na kupoteza mchezo wa leo, Azam FC wanaendeleza kuongoza Ligi Kuu wakibaki na pointi zao 30 kufuatia kucheza mechi 14, mbele ya Simba SC yenye pointi 28 na mabingwa watetezi, wenye pointi 27 baada ya wote kucheza mechi ...

FOUNTAIN GATE YAICHAPA COASTAL UNION 3-2 TANZANITE KWARAA

Image
WENYEJI, Fountain Gate wameibuka na ushindi wa mabao 3-2 dhidi ya Coastal Union katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara leo Uwanja wa Tanzanite Kwaraa, Babati mkoani Manyara. Mabao ya Fountain Gate yamefungwa na kiungo wa Kimataifa wa Burundi, Elie Mokono Eldhino mzaliwa wa Kinshasa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) dakika ya 16, mshambuliaji William Edgar dakika ya 47 na kiungo Mghana, Nicholas Gyan kwa penalti dakika ya 54. Kwa upande wao Coastal Union mabao yao yamefungwa na kiungo Lucas Almeida Kikoti dakika ya 44 kwa mkwaju wa penalti pia na mshambuliaji Maabad Maulid Maabad dakika ya 79. Kwa ushindi huo, Fountain Gate wanafikisha pointi 20 katika mchezo wa 13 na kupanda kwa nafasi mbili hadi ya sita, wakati Coastal Union inabaki na pointi zake 16 za mechi 13 pia nafasi ya tisa.

KMC NA MASHUJAA NGOMA NGUMU MWENGE, ZAGAWANA POINTI KWA SARE YA 0-0

Image
WENYEJI, KMC wametoka suluhu na Mashujaa FC ya Kigoma katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara Uwanja wa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni, KMC Complex, Mwenge Jijini Dar es Salaam. Katika mchezo huo mkali na wa kusisimua, timu zote zilishambuliana kwa zamu na sifa ziwaendee makipa wa timu zote mbili za mabeki wao – kama si lawama kwa safu za ushambuliaji kukosa makali leo. Kwa matokeo hayo, KMC inafikisha pointi 15 katika mchezo wa 14 ingawa inabaki nafasi ya 11, wakati Mashujaa FC inafikisha pointi 18 katika mchezo wa 13, nayo inabaki nafasi ya sita.

SINGIDA BLACK STARS YAIBANJUA DODOMA JIJI 2-1 BAO ZOTE KAPIGA RUPIA

Image
TIMU ya Singida Big Stars imeibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Dodoma Jiji FC katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara leo Uwanja wa CCM LITI mjini Singida. Mabao yote ya Singida Big Stars yamefungwa na mshambuliaji wa Kimataifa wa Kenya, Elvis Baranga Rupia dakika ya nane na 15, wakati bao pekee la Dodoma Jiji limefungwa na mshambuliaji mzawa, Yasin Mohamedi Mgaza 58. Kwa ushindi huo, Singida Big Stars inafikisha pointi 27 katika mchezo wa 13, ingawa inabaki nafasi ya nne ikizidiwa tu wastani wa mabao na Yanga ambayo ina mechi mbili mkononi na wote wapo nyuma ya Azam FC yenye pointi 30 za mechi  13 na Simba SC yenye pointi 28 za mechi 11. Kwa upande wao Dodoma Jiji baada ya kichapo cha leo wanabaki na pointi zao 16 za mechi 14 sasa nafasi ya 10.    

KAGERA SUGAR YAAMBULIA SARE KWA NAMUNGO, 1-1 KAITABA

Image
WENYEJI, Kagera Sugar wamelazimishwa sare ya kufungana bao 1-1 na Namungo FC katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba mkoani Kagera. Mabao yote yalifungwa na viungo washambuliaji, Hassan Salum Kabunda akianza kuifungia Namungo dakika ya 60, kabla ya Mganda Peter Lwasa kuisawazishia Kagera Sugar dakika nne baadaye. Kwa matokeo hayo, Kagera Sugar inafikisha pointi 14 katika mchezo wa 11 na inabaki nafasi ya 14, wakati Namungo FC inafikisha pointi 10 katika mchezo wa 13, nayo inabaki nafasi ya 15 kwenye ligi ya timu 16.

PAMBA JIJI YAWABANA JKT TANZANIA, MECHI YAISHA KWA SARE YA 0-0 MBWENI

Image
WENYEJI, JKT Tanzania wamelazimishwa sare ya bila mabao na Pamba Jiji ya Mwanza katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara jioni leo Uwanja wa Meja Jenerali Mstaafu Michael Isamuhyo, Mbweni Jijini Dar es Salaam. Pamoja na kucheza ugenini, Pamba Jiji inayofundshwa na kocha mzoefu, Freddy Felix Minziro ilifanikiwa kuwadhibiti JKT na kuondoka na pointi moja katika vita yao ya kuepuka kushuka Daraja. Kwa matokeo hayo, JKT Tanzania inafikisha pointi 17 na kusogea nafasi ya saba, ikiizidi wastani wa mabao Fountain Gate baada ya wote kucheza mechi 12, wakati Pamba Jiji inafikisha pointi 12 katika mchezo wa 14 na kupanda kwa nafasi moja hadi ya 12. Mechi nyingine ya Ligi Kuu inaendelea muda huu Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba baina ya wenyeji, Kagera Sugar na Namungo ya Ruangwa mkoani Lindi.

M-BET, HALOPESA KUWAZAWADIA MASHABIKI WA SOKA KUPITIA KAMPENI YA AMSHA AMSHA

Image
MASHABIKI wa soka wa Tanzania, sasa wanaweza kujishindia zawadi mbalimbali ikiwa pamoja na fedha kupitia kampeni ya  Amsha Amsha iliyozinduliwa na kampuni ya michezo ya kubashiri ya M-Bet Tanzania na Halotel. Meneja Masoko wa M-Bet, Levis Paul aliema kuwa mbali ya zawadi ya fedha ya Sh50,000 kwa washindi wawili kwa siku, pia mashabiki wa soka wanaweza kujishindia fedha taslimu, simu janja, na televisheni za kisasa. Paul alisema kuwa kampeni hiyo imelenga kuwazawadia wateja wao ambapo pia wanaweza kushindia fedha kwa kubashiri matokeo ya mechi katika ligi mbalimbali duniani. Meneja Masoko wa Kampuni ya michezo ya kubashiri ya M-BET Tanzania, Levis Paul (kushoto) na Afisa Masoko wa HaloPesa Aidat Lwiza wakionyesha kifurushi kilichojaa zawadi ambazo watazawadiwa wateja wao kupitia kampeni ya Amsha Amsha “Washindi wawili wa kila siku watajishindia Sh50,000, ambapo jumla ya Sh6,000,000 zimetengwa kwa kipindi hiki cha sikukuu,” alisema Paul.  Aliongeza kuwa kila mwish...

YANGA SC YAMSAJILI BEKI WA ZAMANI WA SIMBA ISRAEL PATRICK MWENDA

Image
KLABU ya Yanga imetangaza kumsajili kiungo anayeweza kucheza nafasi za ulinzi hususan beki wa kulia, Israel Patrick Mwenda (24) kutoka Singida Black Stars. Mwenda aliyezaliwa Mwanza anakwenda kuungana na nyota watatu, kipa Abdutwalib Mshery na mabeki Kibwana Shomari na Dickson Job aliocheza timu ya taifa katika Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika kwa vijana chini ya umri wa miaka 17 mwaka 2017 nchini Gabon. Kisoka Mwenda aliibukia Alliance FC ya Mwanza kuanzia timu ya vijana mwaka 2019 kabla ya kuhamia KMC mwaka 2020 ambako baada ya msimu mmoja akasajiliwa na vigogo, Simba SC alikocheza hadi Agosti mwaka huu alipohamia Singida Black Stars.

SIMBA SC WACHAPWA 2-1 NA CONSTANTINE ALGERIA

Image
WENYEJI, CS Constantine wametoka nyuma na kushinda 2-1 dhidi ya Simba SC katika mchezo wa Kundi A Kombe la Shirikisho Afrika Uwanja wa Mohamed-Hamlaoui mjini Constantine, Algeria. Beki na Nahodha Mohamed Hussein ‘Tshabalala’ alianza kuifungia Simba dakika ya 24 kwa shuti la mbali kutoka upande wa kushoto wa Uwanja bao ambalo lilidumu hadi mapumziko. Dakika moja baada ya kuanza kipindi cha pili beki Abdulrazack Mohamed Hamza alijifunga akijaribu kuokoa shambulizi la kona na kuipatia CS Constantine bao la kusawazisha, kabla ya mshambuliaji Brahim Dib kuwafungia wenyeji bao la ushindi dakika ya 50. Kwa ushindi huo, CS Constantine wanafikisha pointi sita na kuendelea kuongoza Kundi A, wakati Simba wanabaki na pointi zao tatu sawa na Bravos do Maquis ya Angola ambao leo wameifunga CS Sfaxien ya Tunisia 3-2 Uwanja wa Novembro 11 mjini Luanda. CS Sfaxien baada ya kupoteza mechi zote mbili za kwanza pamoja na ile waliyofungwa 1-0 na CS Constantine wiki iliyopita Jijini Tunis wanashika m...

YANGA YACHAPWA 2-0 TENA LIGI YA MABINGWA AFRIKA

Image
WENYEJI, MC Alger wameibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Yanga katika mchezo wa Kundi A Ligi ya Mabingwa Afrika usiku wa Jumamosi Uwanja wa Julai 5, 1962 Jijini Algiers nchini Algeria. Mabao ya MC Alger yamefungwa na beki Ayoub Abdellaoui dakika ya 64 na mshambuliaji Soufiane Bayazid dakika ya 90'+5. Hicho kinakuwa kipigo cha pili mfululizo kwa Yanga ambayo ilianza michuano hiyo vibaya baada ya kuchapwa mabao 2-0 na Al Hilal nyumbani, Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam, wakati MC Alger inapata ushindi wa kwanza kufuatia isare ya bila mabao ugenini na TP Mazembe Uwanja wa TP Mazembe Jijini Lubumbashi, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC). Mchezo mwingine wa Kundi A utafuatia Jumapili usiku, Al Hilal Omdurman watakuwa wenyeji wa TP Mazembe kuanzia Saa 4:00 usiku Uwanja wa Cheikha Ould Boidiya Jijini Nouakchott, Mauritania.​

AZAM FC YAWACHAPA IRINGA 4-0 KOMBE LA TFF CHAMAZI

Image
WENYEJI, Azam FC wamefanikiwa kutinga Hatua ya 32 Bora Kombe la Shirikisho la Soka Tanzania (TFF). Michuano inayodhaminiwa na benki ya CRDB baada ya ushindi wa mabao 4-0 dhidi ya Iringa SC leo Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam. Mabao ya Azam FC yamefungwa na kiungo Mkongo, Yanick Litombo Bangala dakika ya 25, beki Mcolomboa, Yeison David Fuentes Mendoza dakika ya 45’+1, Sospeter Bajana dakika ya 65 na Daud Said dakika ya 74.

SALIBOKO AFUNGA MAWILI KMC YAICHAPA BLACK SIX 5-0 KOMBE LA CRDB

Image
WENYEJI, KMC wamefanikiwa kutinga Hatua ya 32 Bora Kombe la Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), michuano inayodhaminiwa na benki ya NBC baada ya ushindi wa mabao 5-0 dhidi ya Black Six leo Uwanja wa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni, KMC Complex, Mwenge, Dar es Salaam. Mabao ya KMC yamefungwa na Daruesh Saliboko mawili, dakika ya tatu na la penalti dakika ya 17, Hance Masoud dakika ya 13, Rashid Chambo dakika ya 47 na Ally Shaaban dakika ya 79.

SHABIKI WA YANGA NA MAN UNITED ASHINDA MILIONI 20 KUPITIA KASINO YA LEONBET

Image
SHABIKI wa klabu ya Yanga na Manchester United, Bright Mwakasege ameshinda Sh20 million kupitia kasino maarufu ya  LEONBET  kwenye mchezo pendwa wa Aviator.   Ushindi huu wa Mwakasege ambaye ni mkazi wa Dar es Salaam, umetokana na dau lake la Sh200 tu kwa kupata odds au multiplier x100000 – kitu ambacho ni nadra sana kutokea katika mchezo huu wa  Aviator  maarufu kama kindege.    Akizungumza baada ya ushindi, Bright alisema kuwa awali alifikiri amejishindia Sh2 milioni tu na hiyo ilitokana na uharaka wake wa kuangalia kiasi cha fedha alichoshinda. Mshindi wa mchezo wa aviator wa kasino ya LEONBET, Bright Mwakasege akiwa katika pozi mara baada ya kukabidhiwa fedha Sh20 milioni alizoshinda kwa dau la sh200 tu   “Niliangalia haraka haraka, nikajua ni Sh2 milioni. Hata hivyo, kaka yangu alipopitia tena ushindi huo, aliniambia kuwa nimeshinda Sh20 milioni. Hapa nikajaa na furaha zaidi baada ya kufahamu kuwa amepata bahati kubwa ya kushinda zawadi...

YANGA SC YABORESHA BENCHI LA UFUNDI, YAONGEZA KOCHA WA FITNESS

Image
KLABU ya Yanga imemtambulisha Adnan Behlulovic raia wa Bosnia-Herzegovina 'Super Papa Adi' kuwa Kocha wake mpya wa Fitness akiungana na Mmorocco, Taibi Lagrouni kuongeza nguvu kwenye idara ya utimamu wa mwili kwa wachezaji wa timu hiyo. Behlulovic (43) ni beki wa zamani wa kushoto aliyecheza klabu mbalimbali nchini kwao, Bosnia-Herzegovina ikiwemo Baton Sarajevo na za madaraja ya nchini nchini Ujerumani ikiwemo, SV Eintracht Ahaus.

JKT TANZANIA YASONGA MBELE KOMBE LA TFF BAADA YA KUICHAPA IGUNDA UTD 5-1

Image
TIMU ya JKT Tanzania imefanikiwa kwenda Hatua ya 32 Bora Kombe la Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), michuano inayodhaminiwa na benki ya CRDB baada ya ushindi wa mabao 5-1 dhidi ya Igunga United jioni ya leo Uwanja wa Meja Jenerali Mstaafu Isamuhyo, Mbweni, Dar es Salaam. Mabao ya JKT Tanzania yamefungwa na Wilson Nangu dakika ya 12, Nahodha John Bocco dakika ya 14, Mohamed Bakari mawili dakika ya 16 na 30 na Danny Lyanga dakika ya 68, wakati bao pekee la Igunga United limefungwa Joel Loya dakika ya 58. 

KAGERA SUGAR YAAMBULIA SULUHU KWA PRISONS KAITABA

Image
WENYEJI, Kagera Sugar wametoa sare ya bila mabao na Tanzania Prisons katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara usiku huu Uwanja wa Kaitaba, Bukoba mkoani Kagera. Kwa matokeo hayo, Kagera Sugar inafikisha pointi 10, ingawa inabaki nafasi ya 14 ikizidiwa pointi moja na zote, Pamba Jiji na Tanzania Prisons zinazofuatana nafasi ya 12 na 13 baada ya wote kucheza mechi 13.

NDUGU WA MALAWI WAWANIA TUZO YA MWANASOKA BORA WA KIKE AFRIKA

Image
WANASOKA wawili ndugu wa Malawi, Tabitha na Temwa Chawinga wameingia kwenyen orodha ya mwisho ya wachezaji wanaowania Tuzo ya Mwanasoka Bora wa Mwaka Mwanamke barani Afrika – wakichuana na Sanaa Mssoudy wa Morocco, Chiamaka Nnadozie wa Nigeria na Barbra Banda wa Zambia zitakazotolewa Desemba 16 Jijini Marrakech, Morocco. Tabitha anayechezea Olympic Lyon ya Ufaransa baada ya awali kuchezea PSG na Inter Milan na Temwa anayechezea Kansas City Current ya Marekani aliyojiunga nayo mwaka huu akitokea Wuhan Jianghan kufutaia awali kuchezea Kvarnsvedens IK ya Sweden – wote ni washambuliaji. Katika orodha ya mwisho ya wanaowania Tuzo za CAF kwa Wanawake kwa mwaka 2024 iliyotolewa leo, Tuzo ya Mwanasoka Bora wa Kike Anayecheza Afrika imekutanisha wachezaji watatu wa AS FAR Rabat ya Morocco ambao ni Doha El Madani, Khadija Er-Rmichi na Sanaâ Mssoudy wanaochuana na nyota wawili wa TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), Merveille Nanguji na Lacho Flora Marta. Mnigeria, Chiamaka...