Posts

Showing posts from July, 2024

MSHERY AONGEZA MKATABA WA KAZI YANGA HADI 2027

Image
KİPA wa akiba wa Yanga, Abutwalib Hamad Mshery (25) ameongeza mkataba wa miaka mitatu wa kuendelea kuichezea klabu hiyo hadi mwaka 2027. VIDEO YA UTAMBULISHO WA MSHERY KUONGEZA MKATABA YANGA

KIBABAGE AJITIA KITANZI YANGA SC HADI MWAKA 2027

Image
BEKİ wa kushoto, Nickson Clement Kibabage (23) ameongeza mkataba wa miaka mitatu kuendelea kuichezea klabu ya Yanga hadi mwaka 2027. VIDEO: UTAMBULISHO WA KIBABAGE KUONGEZA MKATABA YANGA SC

SIMBA SC YASAJILI ALIYEKUWA ANACHEZA LİGİ YA AFRİKA KUSINI

Image
KLABU ya Simba imemtambulisha beki wa kati mzawa, Abdulrazack Mohamed Hamza (21) kutoka SuperSport United ya Afrika Kusini kuwa mchezaji wake mpya wa tano kuelekea msimu ujao. Hamza ni mchezaji aliyeibukia Mbeya City mwaka 2020, kabla ya kuhamia KMC mwaka 2021 na Namungo FC 2022 ambayo ilimuuza SuperSport mwaka jana. Wachezaji wengine waliosajiliwa Simba ni beki mzawa, Lameck Elias Lawi (18) kutoka Coastal Union, winga Mzambia, Joshua Mutale (22) kutoka Power Dynamos ya Zambia na washambuliaji Mganda, Steven Mukwala (24) kutoka Asante Kotoko ya Ghana na Muivory Coast, Jean Charles Ahoua (22) kutoka Stella Club d'Adjamé ya kwao.

KASSIM MANARA: KIPAJI KILICHOIBUKIA YANGA NA KUTAMBA ULAYA

Image
 

KAPTENI NONDO MWAMNYETO AJITIA KITANZI JANGWANI HADİ 2026

Image
NAHODHA, beki Bakari Nondo Mwamnyeto ameongeza mkataba wa miaka miwili wa kuendelea na majukumu katika klabu ya Yanga hadi mwaka 2026. VIDEO: UTAMBULISHO WA MWAMNYETO KUONGEZA MKATABA YANGA SC

SIMBA SC YASAJILI KIUNGO MUIVORY COAST ‘DOGO’ WA MIAKA 22 TU

Image
KLABU ya Simba imeendelea kujiimarisha kuelekea msimu ujao baada ya kumtambulisha kiungo mshambuliaji Muivory Coast, Jean Charles Ahoua (22) kutoka Stella Club d'Adjamé ya kwao, Abidjan. Huyo anakuwa mchezaji wa nne mpya baada ya beki mzawa, Lameck Elias Lawi (18) kutoka Coastal Union, winga Mzambia, Joshua Mutale (22) kutoka Power Dynamos ya Zambia na mshambuliaji, na mshambuliaji Mganda, Steven Mukwala (24) kutoka Asante Kotoko ya Ghana.

CHAMA AWAAGA RASMI SIMBA NI KUJITAMBULISHA YEYE SASA NI YANGA

Image
KIUNGO Mzambia, Clatous Chota Chama ameandika wraka wa kuiaga klabu ya Simba kupitia akaunti yake ya Instagram baada ya kujiunga na mahasimu, Yanga. “Miaka sita iliyopita nilikuja kama mgeni. Mkanipa nafasi na changamoto ya kuwa toleo bora zaidi kwangu. Tuliiteka ardhi hii kwa pamoja, tukajitanua hadi sehemu nyingine za Afrika, na mengine ni historia. Baada ya miaka sita ya furaha kubwa, kiburi, na malengo, hatima zetu zilizounganishwa zinachukua mkondo tofauti. Sina chochote, isipokuwa heshima kwa kila mmoja wenu kwa upendo na sapoti mliyonipa miaka yote na hakuna anayeweza kubadilisha historia tuliyotengeneza pamoja. Wanasema; “Show haijaisha mpaka ‘Mama Kibonge’ aimbe nami ninaamini wimbo huo una thamani kwaenu. Nawatakia kila la kheri na tutaendelea kuonana,” ameandika Chama sambamba na kujitambulisha kama mchezaji wa Yanga katika akaunti yake hiyo. Chama (33), ambaye amekuwa mchezaji muhimu wa timu ya Taifa ya Zambia tangu mwaka 2015 anajiunga na Yanga baada ya kuitu

UHOLANZI NA UTURUKI ZAKAMILISHA ROBO FAINALI EURO 2024

Image
TIMU za Uholanzi na Uturuki zimefanikiwa kutinga Robo Fainali za Kombe la Mataifa ya Ulaya ‘Euro 2024’ baada ya kuzitoa Romania na Austria jana nchini Ujerumani. Ilianza Uholanzi kuitandika Romania 3-0, mabao ya washambuliaji, Cody Mathès Gakpo wa Liverpool dakika ya 20 na Donyell Malen wa Borussia Dortmund mawili dakika ya 83 na 90 Uwanja wa Allianz Arena. Jijini Münich. Naye beki wa Al-Ahli  ya Saudi Arabia, Merih Demiral alifunga mabao yote, dakika ya kwanza na ya 59, Uturuki ikiichapa Austria 2-1 Uwanja wa Red Bull Arena, Jijini Leipzig.  Bao la kufuatia machozi la Austria lilifungwa na winga wa SC Freiburg, Michael Gregoritsch dakika ya 66 na sasa Uturuki itakutana na Uholanzi katika Robo Fainali Jumamosi Uwanja wa Olympia Jijini Berlin. Robo Fainali nyingine ni Ijumaa Hispania na Ujerumani na Ureno Ufaransa, wakati England na Uswisi nazo pia zitaumana Jumamosi.

DIARRA AONGEZA MKATABA WA KUENDELEA KUDAKA YANGA HADI 2027

Image
KİPA wa Kimataifa wa Mali, Djigui Diarra ameongeza mkataba wa miaka mitatu utakaomfanya aendelee kuwa mchezaji wa timu ya Wananchi hadi mwaka 2027. GONGA KUTAZAMA VIDEO UTAMBULISHO WA MKATABA MPYA WA DJIGUI DIARRA

AZAM FC YAMNUNUA ‘MOJA KWA MOJA’ KIPA MSUDAN NA KUMSAINISHA MIAKA MIWILI

Image
KLABU ya Azam FC imemnunua moja kwa moja na kumsainisha mkataba wa miaka miwili kipa wa Kimataifa was Sudan, Mohamed Mustafa kutoka El Merreikh ya Sudan. Hatua hiyo inafuatia kazi nzuri ya kipa huyo kufuatia kusajiliwa kwa mkopo mwezi Januari akiisaidia Azam FC kumaliza nafasi ya pili kwenye Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara na Kombe la CRDB la Shirikisho la Soka Tanzania (TFF). GONGA KUTAZAMA PICHA ZAIDI

SIMBA SC YASAJILI MSHAMBULIAJI MGANDA WA ASANTE KOTOKO

Image
KLABU ya Simba imemtambulisha mshambuliaji wa Kimataifa wa Uganda, Steven Mukwala (24) kutoka Asante Kotoko ya Ghana, ambaye aliibukia Vipers SC kabla ya kupelekwa kwa mkopo Maroons FC, zote za kwao, Uganda. Steven Mukwala anakuwa mchezaji mpya wa tatu Simba SC baada ya beki mzawa, Lameck Elias Lawi (18) kutoka Coastal Union ya Tanga na winga Mzambia, Joshua Mutale kutoka Power Dynamos ya kwao. Kikosi cha Simba kinatarajiwa kuingia kambini wiki hii nchini Misri kujiandaa na msimu mpya, ambao utafunguliwa kwa Tamasha la Simba Day Agosti 3 Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam.

SIMBA SC YAMTAMBULISHA WINGA MZAMBIA JOSHUA MUTALE

Image
KLABU ya Simba imemtambulisha winga wa Kimataifa wa Zambia, Joshua Mutale kutoka Power Dynamos ya kwao kuwa mchezaji wake mpya wa pili kuelekea msimu ujao baada ya beki Lameck Lawi kutoka Coastal Union ya Tanga.

WAWILI WANAOCHEZA ULAYA WAONGEZWA TWIGA STARS KUIVAA TUNISIA

Image
KOCHA wa timu ya soka ya taifa ya wanawake, Twiga Stars, Bakari Nyundo Shime ameongeza wachezaji wawili kikosini kuelekea michezo miwili ya kirafiki ya Kimataifa mwishoni mwa wiki hii. Hao ni Malaika Meena (pichani juu) wa klabu ya Wake Forest University ya Uingereza na Victoria Maselle (pichani chini) wa Nasa TopHat Soccer Academy ya Georgia ambao wataungana na wenzao wengine 20 wanaoingia kambini leo kujiandaa na michezo ya kirafiki dhidi ya Tunisia na Botswana. 

CLATOUS CHOTA CHAMA MCHEZAJI WA KWANZA MPYA YANGA SC

Image
KLABU ya Yanga imemtambulisha kiungo Mzambia, Clatous Chota Chama kuwa mchezaji wake mpya wa kwanza kielekea msimu ujao. Chama (33), ambaye amekuwa mchezaji muhimu wa timu ya Taifa ya Zambia tangu mwaka 2015 anajiunga na Yanga baada ya kuitumikia Simba SC kws vipindi viwili kuanzia mwaka 2018 Aliwasili Simba SC mwaka 2018 akitokea Lusaka Dynamos ya kwao, akacheza hadi mwaka 2021 alipouzwa RS Berkane ya Morocco, kabla ya kurejea Msimbazi mwaka 2022 na sasa anahamishia huduma zake Jangwani. Kisoka Chama aliibukia ZESCO United ya kwao mwaka 2016, kabla ya kuhamia Al Ittihad ya Mısri mwaka 2017 ambako alicheza kwa miezi kadhaa na kurejea Zambia kujiunga na Lusaka Dynamos.