KIUNGO Mzambia, Clatous Chota Chama ameandika wraka wa kuiaga klabu ya Simba kupitia akaunti yake ya Instagram baada ya kujiunga na mahasimu, Yanga. “Miaka sita iliyopita nilikuja kama mgeni. Mkanipa nafasi na changamoto ya kuwa toleo bora zaidi kwangu. Tuliiteka ardhi hii kwa pamoja, tukajitanua hadi sehemu nyingine za Afrika, na mengine ni historia. Baada ya miaka sita ya furaha kubwa, kiburi, na malengo, hatima zetu zilizounganishwa zinachukua mkondo tofauti. Sina chochote, isipokuwa heshima kwa kila mmoja wenu kwa upendo na sapoti mliyonipa miaka yote na hakuna anayeweza kubadilisha historia tuliyotengeneza pamoja. Wanasema; “Show haijaisha mpaka ‘Mama Kibonge’ aimbe nami ninaamini wimbo huo una thamani kwaenu. Nawatakia kila la kheri na tutaendelea kuonana,” ameandika Chama sambamba na kujitambulisha kama mchezaji wa Yanga katika akaunti yake hiyo. Chama (33), ambaye amekuwa mchezaji muhimu wa timu ya Taifa ya Zambia tangu mwaka 2015 anajiunga na Yanga baada ya kuitu